CHADEMA: Awamu ya Sita imeimarisha Uhuru wa Kujieleza nchini

kalacha mateo

Senior Member
Joined
Sep 27, 2021
Posts
119
Reaction score
240
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) imeipongeza serikali kwa kuanza kuboresha mazingira ya haki za Binadamu ikiwemo uhuru wa kujieleza na kutoa maoni. Hayo yalisemwa na Chama hiko wakati wa maadhimisho ya siku ya haki za binadamu kupitia Tamko la kimataifa la Haki za kibinadamu (UDHR) ambayo hufanyika Desemba 10.

Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa wa CHADEMA, Mch Peter Msigwa, alibainisha kuanza kuimarika kwa uhuru wa kujieleza na kutoa maoni alipozungumza wakati wa kongamano hilo lililofanyika mjini Iringa. Alisema Serikali duniani kote ina wajibu wa kuhakikisha inalinda haki za raia wake, ikiwemo haki ya kuishi, kukusanyika, kutoa maoni na nyinginezo.

Mch Msigwa alisema hali ya kujieleza hapo nyuma ilikuwa siyo ya kuridhishwa lakini kwa sasa mambo yameanza kubadilika katika ki[indi hiki cha Serikali ya awamu ya sita.


 
Uhuru upi wa kujieleza na kutoa maoni ulioimarishwa ikiwa mpaka leo bado wanafanyia mikutano yao vyumbani?
 
Watu wanataka vitendo tushajieleza vya kutosha.
vitendo gani vya kupiga watu risasi? haki za binaadam hazipimwi na madaraja wala ndege. ni haki ambazo tunazipata kwasababu ni binaadamu
 
10 December 2022
LIVE: KONGAMANO LA CHADEMA

Peter Msigwa, William Mungai, John Heche, Susan Kiwanga, Joseph Mbilinyi a.k.a SUGU wafuguka katika kongamano WEWE NA CHADEMA tarehe 10 December 2022 Iringa, Tanzania

Tundu Lissu, Godbless Lema washiriki kupitia mtandao katika kongamano hilo lililorindima kwa mafanikio makubwa nyanda za juu kusini na kudhihirisha CHADEMA imezidi kujiimarisha kama chama cha kisiasa chenye ushawishi mkubwa Tanzania bila kujali vyama.
Source : millard ayo
 
CHADEMA YAZUNGUMZIA DHANA YA KUJINASUA TOKA KWA 'MKOLONI', HUKU MATENDO YA KIKOLONI BADO YAMEBAKI MPAKA LEO HII TANZANIA

 
MIAKA 61 YA UHURU, ADUI UMASIKINI WA MAJI SAFI BADO ANATUGARAGAZA

 
Uhuru upi wa kujieleza na kutoa maoni ulioimarishwa ikiwa mpaka leo bado wanafanyia mikutano yao vyumbani?
Na wakiandamana mita kumi tu tokea hapo wanadakwa
 
vitendo gani vya kupiga watu risasi? haki za binaadam hazipimwi na madaraja wala ndege. ni haki ambazo tunazipata kwasababu ni binaadamu
Hiyo haki unayoitaka unataka upewe ili uzungumzie Diamond na Ali kiba au unataka hiyo haki kwa ajiri ya kukosoa na kudai maendeleo? Wakati wa JK inasemekana hiyo haki ilikuwepo ya kutosha ila mpaka mwisho JK akabaki kuonekana dhaifu kutokana na jinsi alivyokuwa akiendesha serikali kishkaji.
Ndio maana nasema tushaongea sana hivyo tunahitaji vitendo na sio kuachia watu waongee tu halafu hakuna anayesikiliza na kutekeleza inabaki kama kelele tu mwishoni wanaitwa upinzani ikulu kunywa chai basi mchezo umeisha.
 
Nionavyo mimi chadema inahitaji fikra mpya zitakazoendana na matakwa ya wananchi kwa sasa. Ni dhahiri mitizamo na sera zilizoing'arisha chadema ndizo alizokuwa akizitumia JPM wakati wa utawala wake na wao viongizi wa chadema hawakumuelewa kabisa wakaishia kumkosoa kila kukicha.

Leo hii chadema hawawezi kuzirudia zile sera na itikadi kwa kutumia viongozi wale wale maana watahisi ni kama wanaunga mkono yale aliyokuwa akifanya JPM hivyo watazidi kuwachanganya wafuasi wao. Ukifuatilia kwa makini utagundua chadema ya kabla 2015 na hii ya sasa ni chadema mbili tofauti kabisa nahisi ni kwa sababu ya kuondoka kwa Dr Slaa
 
Ndani kabisa kwenye nafsi yako,unakielewa ulichokiandika?πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…