Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Dodoma Mjini umelalamikia kuwepo kwa vitendo vya hujuma katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye Daftari la Mkaazi.
Akizungumza leo, Oktoba 14, 2024, katika ofisi za CHADEMA Kanda ya Kati zilizopo jijini Dodoma, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilayani humo, Stephen Karashan, amedai kuwa wamebaini majina feki katika moja ya vituo vya uandikishaji wa wapiga kura.
Karashan ameongeza kuwa vitendo hivi vinahatarisha uadilifu wa mchakato wa uchaguzi na kuitaka serikali kuingilia kati kuhakikisha zoezi hilo linaendeshwa kwa haki na uwazi.
Uongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Dodoma Mjini umelalamikia kuwepo kwa vitendo vya hujuma katika zoezi la uandikishaji wa wapiga kura kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye Daftari la Mkaazi.
Akizungumza leo, Oktoba 14, 2024, katika ofisi za CHADEMA Kanda ya Kati zilizopo jijini Dodoma, Mwenyekiti wa CHADEMA Wilayani humo, Stephen Karashan, amedai kuwa wamebaini majina feki katika moja ya vituo vya uandikishaji wa wapiga kura.
Karashan ameongeza kuwa vitendo hivi vinahatarisha uadilifu wa mchakato wa uchaguzi na kuitaka serikali kuingilia kati kuhakikisha zoezi hilo linaendeshwa kwa haki na uwazi.