CHADEMA iliyoshindwa kujifanyia mageuzi inatuaminishaje tukiwapa nchi watafanya mageuzi?

Mageuzi makubwa ni kuiondoa CCM madarakani.
 
Kwa mtazamo wako ni bora kuendelea na Mkoloni CCM aliyeshindwa kuleta maageuzi kwa miaka 60 au ....!!

By the way, kuondoka kwa CCM madarakani tayari itakuwa ni Mageuzi Makubwa kabla ya lolote kufanyika.
Mimi nimependa hoja yako ya kwamba CCM kama mkoloni kwa upande wako unaona hajaleta mageuzi yoyote ktk nchi hii,kiasi kwamba kama ataondolewa akapewa mwingine anaweza kuyaleta mageuzi hayo.
Naomba kufahamu una maanisha mageuzi ya namna gani hasa?
 
Mimi nimependa hoja yako ya kwamba CCM kama mkoloni kwa upande wako unaona hajaleta mageuzi yoyote ktk nchi hii,kiasi kwamba kama ataondolewa akapewa mwingine anaweza kuyaleta mageuzi hayo.
Naomba kufahamu una maanisha mageuzi ya namna gani hasa?
Kuna wale wanaodai kuwa CCM ina wenyewe ..... watu huwa tunawadharau. Yah right. Kuna mashabiki na wale walionyuma yao ambao ndiyo wenyewe. Wale wanaofikiri bila wao Tanzania haipo. Bila wao hakuna mwingine anayeweza zaidi yao .... Mamungu watu!!

Kuondoka kwa CCM ni magauzi tosha .... sawa na KANU huko Kenya,
 
Hoja yangu mimi ninashangazwa na michango ya baadhi ya wachangiaji humu ndani wao tatizo kuu kwao ni neno ccm na rangi za kijani na njano hivyo hata watu wazuri wakiwa ccm wanawakataa na wabaya walioko chadema wanawakubali
 
Hata TANU wakati tunapata Uhuru walikuwa wadogo. Kwani CCM walizaliwa wakubwa?
 
Hata TANU wakati tunapata Uhuru walikuwa wadogo. Kwani CCM walizaliwa wakubwa?
Chadema ilipewa airtime kubwa sana zaidi ya robo karne bado hawajaonyesha ukubwa wao kushindwa tu kusimamisha wagombea nchi nzima kushindwa kupambana na hila za ccm kwa kupandikiza mamluki mle ndani kuna ifanya chadema kuwa chama kichanga miaka nenda miaka rudi.

Jambo lingine ni namna chadema inavyoshughulikia matatizo yake ya ndani hua yanakiacha chama kimegawanyika na kujeruhika hovyohovyo.
 
Na juzi hapa wameonyesha udhaifu wa ajabu eti mpinzani mwenzao anaongea jambo kwa Nia njema kuhusu mbowe badala ya kukaa kimya au kumuunga mkono wametoka na kupinga yaani Hawa jamaa wanaendekeza utoto mno!!
 
Mageuzi makubwa ni kuiondoa CCM madarakani.
Siasa inazoenda nazo chadema hazina uzito wa kuitoa ccm maana hawataki kwenda na midundo ya wananchi wao wako kivyao.
Kama mbowe angewekwa ndani akipinga tozo, kupanda kwa bei ya bidhaa, kuchelewesha pesa za kumaliza sgr, foleni ya dar, kuondolewa machinga maeneo ambayo serikali yenyewe iliwaruhusu kufanya kazi, kupanda kwa bei ya mbolea Kutoka 60000 Hadi 120000 kwa kg 50, hakika hata vipofu wangeona mbowe ni shujaa wao na chadema ni kimbilio lao. Ndio njia pekee unaweza kukipa umaarufu chama Chako.
 
Hata mkiruhusiwa kufanya mikutano ya kisiasa haita kuwa na tija ikiwa hamta tafuta hoja zinazowatesa wananchi.

Lakini pia chadema ijifunze uvumilivu wa kisiasa chadema usijifanye kama jeshi au nyumba ya ibada maana chadema imepoteza wanachama na viongozi wengi wazuri kwa kuendekeza tabia ya kushindwa kuwavumilia wale wenye mawazo tofauti.
 
Mbona CCM haijafanya mageuzi yeyote ndani ya chama chake lakini bado inaongoza nchi. Tofautisha kuongoza chama na kuongoza nchi.
 
Yani CCM ishindwe kazi lawama apewe CHADEMA. Yani CHADEMA kiwe kinabeba mizigo mizito halafu wakati wake wa kuvuna ukifika Jambazi CCM anaiba mazao ya CHADEMA. Nani anaweza kufanya biashara kichaa Kama hiyo?. Ni muda wananchi wenyewe kuona tatizo na kufanya maamuzi ya wenyewe.
 
Uvimilivu una kiasi. Uvimilivu bila kiasi ni ujinga. Lazima utofautishe wapi pa kuvumilia na wapi pa kusema ukweli. Yani Makamu mwenyekiti wa CHADEMA apigwe risasi; Msaidizi wa mwenyekiti auwawe na mwili wake usijulikane ulipo; Mwenyekiti wa CHADEMA abambikiwe kesi ya ugaidi na wabunge 19 Viti maalum wateuliwe bila baraka za chama. Nani anaweza kuvumilia, was Kwanza anayetakiwa kuwa na uvimilivu wakisiasa ni CCM. Kama CCM haina uvimilivu wa kisiasa hakuna chama Cha siasa Cha upinzani kitachokuwa na uvimilivu.
 
CCM ipo madarakani kwa sababu ni chama dola. Huwezi kutofautiana CCM na fola. Ndio maana Jaji Mkuu Ramadhani aligombea kupitia CCM; IGP Mahita aligombea ubunge huko morogoro kupitia CCM; Afande Tibaigana pia; General Mboma aligombea Mbeya Vijijini kipindi Fulani akashindwa kwa tiketi ya CCM bila kumsahau Hassy Kitine Mkurugenzi wa TISS amewahi kuwa mbunge wa CCM na mwisho Salim Jecha mwenyekiti wa Time ya uchaguzi Zanzibar aligombea urais kupitia CCM. Siku CCM ikijitenga na dola ndio utakuwa mwisho wake.
 
Kwa hizi hoja zako ilikuwaje chadema wakashinda kura million 7 kasoro
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…