kifupi kirefu
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 539
- 3,507
Unaweza ukaishi kwa mfalme bila amani. Unaweza kuishi kwa mfalme ukawa na hofu hata ya majirani wema wanaoendelea na shughuli zao. Unaweza ukapata fursa ya kumshauri mkubwa akabaki kuwashambulia majirani wanaojiendeleza.
Ndivyo walivyo vijana wa chama tawala, muda walionao wangewekeza kushauri serikali iliyopo madarakani wangeiponya serikali na jamii kwa ujumla.
Naangalia huko mitandaoni vijana wa CCM wote wamekuwa Wana ACT-Wazalendo. Tunajiuliza hizi argument zitajenga madarasa, barabara na zahanati?
Maisha yanaenda kasi sana, kila siku zinavyokwenda ndivyo chama tawala kinapopoteza watu wenye nia yakuwekeza akili zao kuikwamua nchi.
Ukimya wa CHADEMA uwe fundisho kwenu kwamba, busara na makuzi waliyonayo vijana wa CHADEMA pamoja na uwezo wao wakujenga hoja ndivyo vinavyowafanya waaminike na si uwezo wao wakuandika uzushi mitandaoni.
Ndivyo walivyo vijana wa chama tawala, muda walionao wangewekeza kushauri serikali iliyopo madarakani wangeiponya serikali na jamii kwa ujumla.
Naangalia huko mitandaoni vijana wa CCM wote wamekuwa Wana ACT-Wazalendo. Tunajiuliza hizi argument zitajenga madarasa, barabara na zahanati?
Maisha yanaenda kasi sana, kila siku zinavyokwenda ndivyo chama tawala kinapopoteza watu wenye nia yakuwekeza akili zao kuikwamua nchi.
Ukimya wa CHADEMA uwe fundisho kwenu kwamba, busara na makuzi waliyonayo vijana wa CHADEMA pamoja na uwezo wao wakujenga hoja ndivyo vinavyowafanya waaminike na si uwezo wao wakuandika uzushi mitandaoni.