Kanali_
JF-Expert Member
- Nov 18, 2018
- 6,438
- 10,180
Nimeona bandiko la ndugu yangu Yericko Nyerere akieleza sababu anazoona yeye zina mashiko za kwanini atamchagua Freeman Mbowe kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA na si Tundu Lissu. Pamoja na urefu wa bandiko hilo nimejitahidi kusoma ila mwishowe nimegundua Yericko kakubali kutumika au kulitumikia tumbo lake na si kuandika kwa kuzingatia uhalisia wa hali ya sasa ya chama chao na nini wanahitaji.
Nikuulize swali moja tu ndugu Yericko: nguvu na ushawishi wa chadema ya 2015 ni sawa na chadema ya leo?
Anguko hilo nyie wachumia tumbo hamlioni? Mmeshawahi kufanya research kujua wananchi wanakichukuliaje chama kwasasa au mnakaa maghetton na kuandika magazeti ya kupost JF?
Nikwambie: Huku mtaani chadema imepoteza mvuto na ushawishi kwa vijana na wanawake ambao ndo mtaji mkubwa kisiasa...wengi wanakiona kama chama cha wachumia tumbo na shida ilianzia kipindi kile kapokelewa Lowassa na ikawa kubwa zaidi kwenye hayo mnayoita maridhiano ambayo kiuhalisia ni maridhiano ya kuridhisha matumbo ya viongozi tu! Ilifika kipindi Chadema kikawa chama cha kupambana na watetezi halisi wa maslahi ya wananchi na si kupambana na wakandamizaji wa haki hizo! Kwasasa tumaini pekee lililobaki ndani ya Chadema ni kufumua safu nzima ya uongozi hasa kichwani kabisa (mwenyekiti) na mtu pekee anayeweza kuirejesha Chadema ilee anaweza kuwa Lissu labda na Heche ila hao wengine wote wameshaonesha udhaifu wao mbele ya dola na hawaaminiki. Mkitaka kushupaza shingo shupazeni then mtaniambia baada ya uchaguzi wa 2025.
NB: Kuna namna uongozi wa Chadema chini ya FAM unacheza huu mchezo kwa maelekezo ya Lumumba.
Nikuulize swali moja tu ndugu Yericko: nguvu na ushawishi wa chadema ya 2015 ni sawa na chadema ya leo?
Anguko hilo nyie wachumia tumbo hamlioni? Mmeshawahi kufanya research kujua wananchi wanakichukuliaje chama kwasasa au mnakaa maghetton na kuandika magazeti ya kupost JF?
Nikwambie: Huku mtaani chadema imepoteza mvuto na ushawishi kwa vijana na wanawake ambao ndo mtaji mkubwa kisiasa...wengi wanakiona kama chama cha wachumia tumbo na shida ilianzia kipindi kile kapokelewa Lowassa na ikawa kubwa zaidi kwenye hayo mnayoita maridhiano ambayo kiuhalisia ni maridhiano ya kuridhisha matumbo ya viongozi tu! Ilifika kipindi Chadema kikawa chama cha kupambana na watetezi halisi wa maslahi ya wananchi na si kupambana na wakandamizaji wa haki hizo! Kwasasa tumaini pekee lililobaki ndani ya Chadema ni kufumua safu nzima ya uongozi hasa kichwani kabisa (mwenyekiti) na mtu pekee anayeweza kuirejesha Chadema ilee anaweza kuwa Lissu labda na Heche ila hao wengine wote wameshaonesha udhaifu wao mbele ya dola na hawaaminiki. Mkitaka kushupaza shingo shupazeni then mtaniambia baada ya uchaguzi wa 2025.
NB: Kuna namna uongozi wa Chadema chini ya FAM unacheza huu mchezo kwa maelekezo ya Lumumba.