CHADEMA iseme inataka nini kwa Wabunge 19 Viti Maalum

CHADEMA iseme inataka nini kwa Wabunge 19 Viti Maalum

mkalamo

JF-Expert Member
Joined
Sep 7, 2013
Posts
340
Reaction score
359
Miezi zaidi ya mitano sasa inaelekea huku kukiwa na mvutano baina ya CHADEMA na Wanachama wake 19, walio Bungeni kwa sasa.

Chama hicho kila kinapojitokeza hadharani kinaeleza kuwa Wanachama hao wamefukuzwa hivyo hawana sifa ya kuwa wabunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano.

Wanasema sababu ya kufukuzwa kwao, ni kwenda tofauti na msimamo wa chama wa kutotambua matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020.

Kwamba maazimio na matamanio ya chama hicho ni kubaki wakati wote bila kutambua matokeo ya jumla yaliyowapatia nafasi yoyote ya kiuongozi, kimapato na uwakilishi baada ya oktoba mwaka jana.

Lakini katikati ya hoja yao hiyo, msimamo wao huo haugusi ruzuku zilizotokana na uchaguzi huo. Msimamo wao huo hauwahusi madiwani na Mbunge mmoja waliopata kutokana na Uchaguzi huo.

Na kila wakiulizwa sababu ya kuruhusu madiwani na Mbunge mmoja kuwa halali, na kuwaharamisha wabunge 19, nafasi zilizotokana na uchaguzi huo, huwezi pata jibu sahihi.

Sana sana watakueleza kuwa wamekiuka maagizo ya chama, na ukiuliza ni maagizo gani watakwambia msimamo wa chama ni kutotambua matokeo yoyote ya uchaguzi wa 2020 na kila kilichookana nacho.

Ukiwauliza madiwani na mbunge mmoja nafasi yao ikoje kwenye msimamo huo, watakuambia wao wamechaguliwa na wananchi kwa kura halali ambazo chama kimesusia kwa msisitizo wa kutopeleka viti maalum, yaani ni vurugu tupu maelezo yao.

Kwa msingi huo sasa hata wafuasi na wanachama wa chama hicho hawajui usaliti wa wabunge 19 ni upi na uhalali wa mbunge mmoja na madiwani walioruhusiwa kuapa ni upi. Katikati ya sintifahamu hiyo, watanzania tukaona wameomba fursa ya kukutana na Rais Samia kwa ajili ya kutafuata muafaka.

Watu makini mfano Absalom Kibanda alipowashauri kama wapo radhi kutafuta muafaka waanze na sakata la wanachama wao 19,matusi yakawa mengi, huku hoja ikiwa utaongeaje na wasaliti waliokubali matokeo ya 2020 kinyume na msimamo wa chama.

Jana Mnyika kahojiwa na chombo cha habari anasema ruzuku ya chama hicho haitokani na nafasi ya ubunge wa viti maalum walivyopata chama chake. Hili ni sawa kabisa nami naunga mkono, sasa swali langu kwao je wameanza kutambua uhalali wa matokeo ya 2020?

Je, wamechukua na wanatumia ruzuku iliyotokana na matokeo wasiyokubaliana nayo?

Au wanataka tuamini/niamini yale yanayosemwa katika korido za ofisi mbali mbali za chama hicho, kwamba shida si uhalali wa matokeo, bali shida ni kwanini majina yaliyotakiwa kwenda kutoka kwa baadhi ya viongozi nje ya vikao vya bawacha hayajawekwa katika umafia mzima wa kupeleka majina bungeni.

Au niamini kuwa msimamo wa walioingia bungeni kukataa kuchangia 100m kwa kila mmoja baada ya kuapishwa ndiyo sababu?

Nitarejea
 
Nadhani kupitia maswali yafuatayo mleta mada na wengine wenye hisia kama zake ikimjumuisha "Ndugai the Great Gogo man" watapata kitu cha kujifunza;

a) Unaposema mvutano wa CHADEMA na wabunge 19 una maana ipi? b)Hivi unatambua wapo bungeni kwa sifa zipi za kikatiba zenye kukidhi kuiwakilisha CHADEMA?

c) Je! Unautambua uhalali wa mchakato uliokuwepo ndani ya chama uliopekea wao kuingia bungeni na kuhalalisha uwakilishi wa nafasi wanazodai za ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya CHADEMA?

d) Hivi unatambua kwa nini walikata rufaa kupinga kuvuliwa kwao uanachama?
 
Mwenyekiti ana majina yake, m'beleji ana majina yake, robart amsterdam ana majina yake na pia katibu mkuu ana majina yake. Sasa tatizo ni kwamba hao wote majina yao hayakupita na badala yake yamepita ya Mdee ambae amewazidi mbinu vigogo wa chama chake.

Ndio maana sasa kila siku unasikia kelele za hao wabunge waliochaguliwa na Mdee na hasa lawama nyingi amepewa Mdee kutokana na sababu hizo nilizokuambia hapo juu.
 
Nia kuu ya cdm ni wafukuzwe ili wapate aibu
Hii ndio furaha yao wanayotaka
 
Nadhani kupitia maswali yafuatayo mleta mada na wengine wenye hisia kama zake ikimjumuisha "Ndugai the Great Gogo man" watapata kitu cha kujifunza;
a) Unaposema mvutano wa CDM na wabunge 19 una maana ipi? b)Hivi unatambua wapo bungeni kwa sifa zipi za kikatiba zenye kukidhi kuiwakilisha CDM?
c) Je! Unautambua uhalali wa mchakato uliokuwepo ndani ya chama uliopekea wao kuingia bungeni na kuhalalisha uwakilishi wa nafasi wanazodai za ubunge wa viti maalum kwa tiketi ya CDM?
d) Hivi unatambua kwa nini walikata rufaa kupinga kuvuliwa kwao uanachama?
Majibu ya maswali yako yote yapo kwenye mada niliyoweka labda uwe mvivu wa kudadavua mambo
 
Lazaro Nyalandu alimgaragaza Tundu Lisu kwenye kura za kamati kuu.!

Huyu mzee wa MIGA ,mwanasheria a Acacia anaaminika na nani sasa kama hadi kamati kuu anashindwa kura??
Lisu ni debe tupu
 
Hela zinawauma hela michango na makato ya kila mwisho wa mwezi. Wanataka kuweka wao ili nusu ya mshahara waupate wao kama chama,ukute akina dada wa bavicha wameshatia masaini ya kukubali hilo jambo
 
Matumizi mabaya ya kodi zetu, watoke huko hili swala sio la chama ni mambo ya Taifa.
 
Tena hao covid hawaoni hata aibu ,kusutwa na kina Nape!
 
Katika hao wabunge wa Chadema Ndugai hana nyumba ndogo kweli?,maana sio kwa mishipa ya shingo inayomtoka kuwatetea.
 
Matumizi mabaya ya kodi zetu, watoke huko hili swala sio la chama ni mambo ya Taifa.
Je chama kinatambua mchakato mzima wa uchaguzi uliozaa bunge kama haitambui mchakato kwanini mchague watu wa kutoka wakati bunge zima hamlitambui?
 
Katika hao wabunge wa Chadema Ndugai hana nyumba ndogo kweli?,maana sio kwa mishipa ya shingo inayomtoka kuwatetea.
Unataka kutuaminisha kuwa hizo nafasi huwa wanazipata kwa kuwekwa nyumba ndogo na vigogo? Kuna madai ya wale wabunge wa kike wa CHADEMA waliounga mkono juhudi kipindi cha mwendazake kuwa viongozi wa CHADEMA huwa watoa hizi nafasi za viti maalumu kwa rushwa za ngono na 10% kwenye malipo yao ya ubunge.
 
Back
Top Bottom