Kwa fikra zangu LISU kiti hakimfai kwasasa kwasababu anajazba ya kuongea. Anapaswa kujifunza mengi sana kwa mwenyekiti wake. Akiona kitu hakikosaw anaongea kwa kupitiliza bila nukta nirahisi sana mtu km huyu kufanya maamuzi yakukurupuka. Watu wengi wanaomuona anafaa wanahisi atawaongoza vyema kwenye maamuzi magumu. Nikweli ila kwa asilimia kubwa tunafikiria mfano wa maandamano labda kudai kwa nguvu haki yetu. Watanzania wanahisi wanahitaji mtu km huyo. Muangalie HECHE au LEMA wakiongea mbele ya waandishi au akihojiwa ghafla halaf fananisha na press za LISU. Kuna utofauti mkubwa wa HEKIMA.
Ukweli nikwamba watanzania sisi niwaoga kupitiliza nnauhakika hakuna kauli ya kiongozi yoyote wa upinzan ataweza kutushawishi kudai haki kwa kutumia nguvu mfano maandamano.
Kuna wakati itafika tu mwisho na bila kauli ya kiongozi yoyote watu wataingia barabarani. Kwahyo km waTz tunaimani hili Lisu ataliweza tunapaswa tufikirie zaidi kupitia mfano wa maandamano ya juzijuzi yalioitishwa na FAM ila hatukuweza kutoka.
Watanzania hatuko tayari kwa lolote
Hatuko tayari kuambiwa fanya hili ila tutakuja kufanya bila kusukumwa na yoyote siku isiyokuwa na jina.
Wamuache FAM amalizie muda aliosema huku akiandaliwa mtu mwingine aidha huyo Lisu ama mwengine.