Mkalukungone mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 862
- 1,755
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati, kimekemea vikali kitendo kinachodaiwa kufanywa na Maafisa Elimu cha kuwalazimisha walimu kwenda kushiriki sherehe ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), mkoani Dodoma tarehe 05 Februari 2025.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kati, Masonga Emmanuel, Maafisa hao wamewafuata watumishi hao wa umma kwa magari na kuwapa fedha za malazi.
Soma Pia:
“Haya ni matumizi mabaya ya madaraka, kuwalazimisha watumishi wa umma kuwa na mlengo wa kisiasa na kutumia kodi za Watanzania na uhuru binafsi wa wafanyakazi kushiriki matukio ya chama kimoja kwa kutumia ushawishi wa madaraka na fedha za walipa kodi wa nchi hii”, imeeleza taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Kati, Masonga Emmanuel, Maafisa hao wamewafuata watumishi hao wa umma kwa magari na kuwapa fedha za malazi.
Soma Pia:
“Haya ni matumizi mabaya ya madaraka, kuwalazimisha watumishi wa umma kuwa na mlengo wa kisiasa na kutumia kodi za Watanzania na uhuru binafsi wa wafanyakazi kushiriki matukio ya chama kimoja kwa kutumia ushawishi wa madaraka na fedha za walipa kodi wa nchi hii”, imeeleza taarifa hiyo.