CHADEMA mnaaminisha watu kuwa mna akili sana ila maarifa ni zero, huwezi tengeneza amri kama wewe siyo mtawala

CHADEMA mnaaminisha watu kuwa mna akili sana ila maarifa ni zero, huwezi tengeneza amri kama wewe siyo mtawala

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
Msemo wa Kiswahili akili nyingi huondoa maarifa unaakisi hulka za CHADEMA katika harakati zao za kudai katiba mpya. Ni sheria ya asili (Natural Law) kwamba sheria hutengezezwa na wenye mamlaka ili kutawala waliobaki.

Mfano
1. Mungu alitengeneza mwenyewe amri kumi zake akampa musa atuletee sisi; angetuhusisha wote mpaka sasa hivi tungekuwa bado tuko amri ya kwanza neno la kwanza.

2. Waingereza walipewa kutusimamia sisi Tanganyika. Hata pale walipoamua kuondoka bado walichukua mda wao wakakaa wakatutengenezea katiba wakatutupatia tuitumie kujitawala.

3. Kenya mradi wa katiba ulikuwa wa Raila na Kibaki. Kibaki aliposhika utawala peke yake hakuigusa katiba. Raila alipofanikiwa kuungana nae kwenye utawala wakati wa mhula wa mwisho wa Kibaki ndipo walipoweza kutengeneza katiba

CHADEMA habari kwamba mamlaka inatoka kwa wananchi ni constructed law as opposed to natural law- ni maneno ya wanaharakati.
Kwa vile mnaonyesha kukosa baraka za wananchi kupitia uchaguzi ili kushika utawala - utamsubiri sana kufikia ndoto zenu za mchana za katiba mpya.

AKILI BILA MAARIFA NI BURE POLENI
 
Mimi nitaendelea kuwananga viongozi wa CHADEMA kwa silika yao ya ubinafsi. Dai la Katiba chimbuko lake linapaswa kuwa ni wananchi na si Viongozi wa kisiasa.

Katiba iliyopo inajitosheleza, kwa nyakati hizi, kwa kuwa inadumisha amani kwa misingi ya demokrasia, haki na uhuru wa kila mtu, nikinukuu Utangulizi katika Katiba ya JMT (1977) KWA KUWA SISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani:

NA KWA KUWA misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu:

KWA HIYO, BASI, KATIBA HII IMETUNGWA NA BUNGE MAALUM LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia na ujamaa.


Bunge hilo lilikuwa la wawakilishi waliochaguliwa kidemokrasia. Serikali uundwa na chama kilichoshinda Uchaguzi Mkuu, kidemokrasia. Lakini kunakuwa na ubishi wa kitoto pale walioshindwa uchaguzi, kwenye sanduku la kura, wanapodai mshindi hakuwa halali wakati Mahakama zipo kutoa haki.

ASIYEKUBALI KUSHINDWA SI MSHINDANI na viongozi wa CHADEMA watambue kuwa AVUMAYE BAHARANI NI PAPA KUMBE WENGINE WAPO
 
Laila wa Kenya ndo nani? Kaza vidole hivyo.
 
Back
Top Bottom