Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Katika kipindi cha Medani za Siasa kilichorushwa hivi karibuni Star TV nilishuhudia Ado Shaibu, Katibu mkuu wa ACT akijibu swali la umilikaji wa Ofisi zao kijanja na kwa kona kona nyingi sana kutoka kwa mtangazaji Odemba. CHADEMA nao wamekuwa wakikejiliwa sana kuhusu kutomiliki jengo la Ofisi kubwa kwa muda mrefu.
Ni vyema raia wa Tanzania wenye upto mdogo wakaeleshwa vizuri kumiliki majengo ya ofisi sio kipimo cha uimara wa chama. Kenya ambako kuna ushindani mkali wa kisiasa Chama cha Jubilee cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta na UDA cha Rais wa sasa, William Ruto vyote vimepanga makao makuu yake katika majengo ya watu na wala havimiliki majengo yake binafsi.
Pia chama cha ODM cha Raila Odinga kiongozi upinzani wa muda mrefu mwaka juzi ndio walijenga ofisi yao ndogo tu kama hiyo ya Ufipa. Kumiliki au kutomilikia ofisi kwa chama hakupaswi kuwa hoja katika siasa makini za masuala mazito ya nchi.
Ni vyema raia wa Tanzania wenye upto mdogo wakaeleshwa vizuri kumiliki majengo ya ofisi sio kipimo cha uimara wa chama. Kenya ambako kuna ushindani mkali wa kisiasa Chama cha Jubilee cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta na UDA cha Rais wa sasa, William Ruto vyote vimepanga makao makuu yake katika majengo ya watu na wala havimiliki majengo yake binafsi.
Pia chama cha ODM cha Raila Odinga kiongozi upinzani wa muda mrefu mwaka juzi ndio walijenga ofisi yao ndogo tu kama hiyo ya Ufipa. Kumiliki au kutomilikia ofisi kwa chama hakupaswi kuwa hoja katika siasa makini za masuala mazito ya nchi.