chegreyson
JF-Expert Member
- Nov 23, 2011
- 974
- 434
Natanguliza shukurani zangu kuchangia hoja ya katiba mpya hususani kuhusiana na chama cha siasa cha CHADEMA.
Nimeamua kwa makusudi kabisa kuanzisha hoja hii ili hisitoria ije ihukumu.Kimsingi hoja ya katiba mpya ilianzishwa na wanaharakati miaka mingi wakati wa vuguvugu la vyama vingi.CHADEMA iliichukuwa hoja hii kama mtaji wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.Chadema ilikwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa wao wangeunda serikali ,KATIBA MPYA ingepatikana katika siku 100 za serikali ya CHADEMA.Hoja ya kwanza inaanzia hapo, Hivi mchakato wa siku 100 demokrasia gani ingechukuwa mkondo katika mazingira hayo.Hili watu hawataki kujadili ana kwa makusudi ama kwa kuogopa kujadili udiktenda ambao ungetokana na kuburuza Watanzania ndani ya siku 100 za kupata katiba.
Baada ya wanaharati na vyama vya siasa kuishinikiza serikali na chama tawala, Rais Kikwete alisoma alama za nyakati na kukubali mchakato wa katiba mpya,hata kama kwenye ilani yao hili halikuwa hoja.
Wakati wa mchakato wa kupeleka bungeni mswaada wa katiba mpya CHADEMA WAKARUKIA KUPITIA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE CHINI YA ANNA MAKINDA ,KUWA MSWAADA HUU UJE KWA HATI YA DHARURA.
Hati hii ilishinikizwa na Mshemiwa Zitto nailinukuliwa kwenye ansadi, pale Spika alipolieleza bunge kuwa Zitto Kabwe ndiye aliyekuwa ametoa pendekezo la hati ya dharura,kwa madai kuwa lilikuwa na uharaka ,hivyo lisingeweza kusubiri taratibu za kawaida za kibunge.
Kama kawaida hili la CHADEMA KULAZIMISHA HATI YA DHARURA halizungumzwi ana kwa makusudi ama kuficha makosa ambayo yalifanywa na CHADEMA lakini anayebebeshwa lawama amekuwa bubu.
Baada ya serikali kuleta mswaada huu kwa hati ya dharura, Chadema wakawa wa kwanza kupinga mswaada kusomwa ama kupelekwa kwa hati ya dharura ,safari kupitia kwa Mwenyekiti Mbowe.
Baada ya hapo yanayoendelea si hoja yangu kwab sasa.
Hoja yangu ya msingi ni kuwa chadema ndio waliolibiruza benge kupeleka mswaada kwa hati ya dharura, nakwa ujanja wakajinasua na CCM wao kawalala usingizi wa pono na kupokwa hoja.
Naomba kutoa hoja.
Nimeamua kwa makusudi kabisa kuanzisha hoja hii ili hisitoria ije ihukumu.Kimsingi hoja ya katiba mpya ilianzishwa na wanaharakati miaka mingi wakati wa vuguvugu la vyama vingi.CHADEMA iliichukuwa hoja hii kama mtaji wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2010.Chadema ilikwenda mbali zaidi kwa kusema kuwa wao wangeunda serikali ,KATIBA MPYA ingepatikana katika siku 100 za serikali ya CHADEMA.Hoja ya kwanza inaanzia hapo, Hivi mchakato wa siku 100 demokrasia gani ingechukuwa mkondo katika mazingira hayo.Hili watu hawataki kujadili ana kwa makusudi ama kwa kuogopa kujadili udiktenda ambao ungetokana na kuburuza Watanzania ndani ya siku 100 za kupata katiba.
Baada ya wanaharati na vyama vya siasa kuishinikiza serikali na chama tawala, Rais Kikwete alisoma alama za nyakati na kukubali mchakato wa katiba mpya,hata kama kwenye ilani yao hili halikuwa hoja.
Wakati wa mchakato wa kupeleka bungeni mswaada wa katiba mpya CHADEMA WAKARUKIA KUPITIA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE CHINI YA ANNA MAKINDA ,KUWA MSWAADA HUU UJE KWA HATI YA DHARURA.
Hati hii ilishinikizwa na Mshemiwa Zitto nailinukuliwa kwenye ansadi, pale Spika alipolieleza bunge kuwa Zitto Kabwe ndiye aliyekuwa ametoa pendekezo la hati ya dharura,kwa madai kuwa lilikuwa na uharaka ,hivyo lisingeweza kusubiri taratibu za kawaida za kibunge.
Kama kawaida hili la CHADEMA KULAZIMISHA HATI YA DHARURA halizungumzwi ana kwa makusudi ama kuficha makosa ambayo yalifanywa na CHADEMA lakini anayebebeshwa lawama amekuwa bubu.
Baada ya serikali kuleta mswaada huu kwa hati ya dharura, Chadema wakawa wa kwanza kupinga mswaada kusomwa ama kupelekwa kwa hati ya dharura ,safari kupitia kwa Mwenyekiti Mbowe.
Baada ya hapo yanayoendelea si hoja yangu kwab sasa.
Hoja yangu ya msingi ni kuwa chadema ndio waliolibiruza benge kupeleka mswaada kwa hati ya dharura, nakwa ujanja wakajinasua na CCM wao kawalala usingizi wa pono na kupokwa hoja.
Naomba kutoa hoja.