Pre GE2025 CHADEMA Sikonge: Watakaoihujumu "No reforms No election" hawatavumiliwa

Pre GE2025 CHADEMA Sikonge: Watakaoihujumu "No reforms No election" hawatavumiliwa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Sikonge, mkoani Tabora, Felix Liata, ameendelea kusisitiza msimamo wa chama hicho wa kutoshiriki uchaguzi bila kufanyika kwa mageuzi ya kisiasa na kisheria, akiwataka wanachama na viongozi kusimama pamoja katika msimamo huo.

Akizungumza Januari 31, 2025, Liata ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepoteza uhalali wa kuendelea kuongoza dola, hivyo kinachohitajika ni hatua madhubuti za kukiondoa madarakani.

“CCM tayari kilishakufa siku nyingi, hakina uhalali tena wa kuitwa chama cha siasa na kuendelea kuongoza nchi. Kilichobaki ni maamuzi magumu tu ya kukiondoa madarakani,” amesema Liata.

Aidha, amesisitiza kuwa wanachama wa CHADEMA wanapaswa kuwa na mshikamano na kuepuka migogoro ya ndani inayoweza kudhoofisha harakati za chama hicho.

“Huu si wakati wa kurushiana maneno na kuzalisha migogoro isiyo na tija. Tunapaswa kusimama pamoja kupigania haki na demokrasia kwa ari na nguvu kubwa zaidi. CHADEMA ndicho chama kilichobeba matumaini ya Watanzania,” ameongeza.

Liata pia ameonya kuwa chama hicho hakitawavumilia watu wanaotaka kuhujumu msimamo wao wa ‘No Reforms, No Election’.

“Tunahitaji ujasiri, uaminifu, na kujitoa kwa hali na mali. Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye mapambano haya. Wote wenye nia ovu dhidi ya CHADEMA tutawashughulikia,” amesisitiza.
 
Chadema makao makuu wana msimamo tofauti.
 
Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Sikonge, mkoani Tabora, Felix Liata, ameendelea kusisitiza msimamo wa chama hicho wa kutoshiriki uchaguzi bila kufanyika kwa mageuzi ya kisiasa na kisheria, akiwataka wanachama na viongozi kusimama pamoja katika msimamo huo.

Akizungumza Januari 31, 2025, Liata ameeleza kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimepoteza uhalali wa kuendelea kuongoza dola, hivyo kinachohitajika ni hatua madhubuti za kukiondoa madarakani.

“CCM tayari kilishakufa siku nyingi, hakina uhalali tena wa kuitwa chama cha siasa na kuendelea kuongoza nchi. Kilichobaki ni maamuzi magumu tu ya kukiondoa madarakani,” amesema Liata.

Aidha, amesisitiza kuwa wanachama wa CHADEMA wanapaswa kuwa na mshikamano na kuepuka migogoro ya ndani inayoweza kudhoofisha harakati za chama hicho.

“Huu si wakati wa kurushiana maneno na kuzalisha migogoro isiyo na tija. Tunapaswa kusimama pamoja kupigania haki na demokrasia kwa ari na nguvu kubwa zaidi. CHADEMA ndicho chama kilichobeba matumaini ya Watanzania,” ameongeza.

Liata pia ameonya kuwa chama hicho hakitawavumilia watu wanaotaka kuhujumu msimamo wao wa ‘No Reforms, No Election’.

“Tunahitaji ujasiri, uaminifu, na kujitoa kwa hali na mali. Hakuna atakayeachwa nyuma kwenye mapambano haya. Wote wenye nia ovu dhidi ya CHADEMA tutawashughulikia,” amesisitiza.

Wewe inaonekana umeshindwa kuelewa. No Reform No Election maana yake ni kwamba Hakuna Mabadiliko Hakuna Uchaguzi.

Hii ni tofauti kabisa na

Hakuna Mabadiliko Hakuna Kushiriki Uchaguzi.

Tafsiri yake pana ni kwamba kama Hakuna marekebisho na mabadiliko ya taratibu zinazosimamia uchaguzi, tusiruhusu uchaguzi kufanyika.
 
Back
Top Bottom