Mzee wa Twitter
JF-Expert Member
- Nov 5, 2023
- 1,483
- 2,392
Hakika kutokana na kiti cha urais kukaniwa na ccm ni wazi ccm itatumia mbinu zote kuhakikisha inashinda uchaguzi huo kama hayati magufuli alivyoukania urais na kuamua kuuvuruga ule uchaguzi ili ashinde na kweli alishinda na dunia nzima iliupinga uchaguzi ule.
Kuthibitisha hilo ni makataa ya ccm juu ya upatikanaji wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi huo ni ushahidi tosha kuwa ccm imekikania kiti cha urais.
Niwashauri chadema kama kweli wanataka kushiriki uchaguzi tena bila katiba mpya wala tume huru ya uchaguzi basi washiriki kugombea ubunge na udiwani suala la kugombea urais kwanza wao kwa wao litawakosanisha pili ccm ipo tayari kuuvuruga uchaguzi na uwe na dosari nyingi ili mradi mgombea wao ameshinda.
Chadema pelekeni nguvu kubwa kwa wagombea ubunge na udiwani naamini mtapata wabunge na madiwani.
Kuthibitisha hilo ni makataa ya ccm juu ya upatikanaji wa katiba mpya na tume huru ya uchaguzi huo ni ushahidi tosha kuwa ccm imekikania kiti cha urais.
Niwashauri chadema kama kweli wanataka kushiriki uchaguzi tena bila katiba mpya wala tume huru ya uchaguzi basi washiriki kugombea ubunge na udiwani suala la kugombea urais kwanza wao kwa wao litawakosanisha pili ccm ipo tayari kuuvuruga uchaguzi na uwe na dosari nyingi ili mradi mgombea wao ameshinda.
Chadema pelekeni nguvu kubwa kwa wagombea ubunge na udiwani naamini mtapata wabunge na madiwani.