Pre GE2025 CHADEMA Wamekata tamaa ya Siasa na kuna uwezekano wa kushindwa kushiriki Uchaguzi wa serikali za Mitaa kwa visingizio Dhaifu.

Pre GE2025 CHADEMA Wamekata tamaa ya Siasa na kuna uwezekano wa kushindwa kushiriki Uchaguzi wa serikali za Mitaa kwa visingizio Dhaifu.

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2022
Posts
28,722
Reaction score
20,610
Ndugu zangu Watanzania,

Ni dhahiri na wazi kabisa kuwa kwa sasa CHADEMA imefika hatua imekata tamaa kabisa ya siasa hapa Nchini,imepoteza morali,hamasa,nguvu iliyokuwa nayo miaka Kadhaa iliyopita. Kwa sasa CHADEMA imepoteza na haina kabisa ushawishi kwa watanzania.haina mvuto wala nguvu ya hamasa na kuteka mioyo ya watu.

Embu jaribu kuangalia umebaki muda mfupi sana kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika November 27 Mwaka huu,lakini ukijaribu kufuatilia maandalizi ya CHADEMA huoni kitu chochote kile kinachoendelea wala kufanyika.,hakuna hata ile hamasa kama iliyokuwepo zamani ya kuwataka watu wakajiandikishe kwa ajili ya kupiga kura,hakuna ile mikutano ya hadhara kama ambavyo walikuwa wanafanya zamani enzi za Dkt Slaa.

Mitaani huku CHADEMA imesahaulika ,kufifia na kupotea katika mioyo ya watanzania.chama kimepoteza kabisa ushawishi kwa watu.hakina ile nguvu ya Umma kiliyo kuwa kikijivunia zamani.kwa sasa hakiwezi hata kushawishi watu kushinikiza jambo fulani kufanyika au kubadilishwa na serikali.kwa sababu hakina watu wa kufanya hivyo wala kuleta presha ya kushinikiza jambo.

Na hapa mnaweza kurejea suala la kufanya maandamano lilivyoshindikana na kumuacha mbowe na mkewe na mwanaye ndio waandamane ,huku vijana wote na viongozi mbalimbali akiwepo katibu mkuu wakiingia mitini na kuendelea na shughuli zao .kama ambavyo mlishuhudia Mnyika akiendelea na ratiba zake za kanisani.

Jaribu kufikiria ni sera ipi na ajenda zipi wanazosimamia CHADEMA kwa sasa? Ni sera na ajenda zipi zinazoongozwa na CHADEMA zenye kugusa hisia za watu? Ni nini wanachozungumzia CHADEMA kwa sasa chenye kugusa maisha ya watu hadi mtu ashawishike kuwaunga mkono na kupanga kuwapa kura? Ni sera na hoja ipi ya CHADEMA kwa sasa unayoweza kusema imeleta na kuteka mijadala ya kisiasa mitaani? Ni hoja ipi ambayo imetolewa na CHADEMA wakati huu na ikaungwa mkono na watu na kuwa gumzo na kugusa mioyo ya watu na kutaka serikali iifanyie kazi?

Sasa kama chama hakina sera wala ajenda wala hoja zenye mashiko na kugusa watu ,ni vipi sasa kitapata kura? Ni vipi sasa kitashindana na CCM chama chenye mizizi mirefu mpaka huko vitongojini? Ni vipi sasa CHADEMA itashindana na CCM yenye mtandao wa uongozi kila eneo hapa Nchini? Ni vipi sasa CHADEMA inaweza tunishiana Misuri katika sanduku la kura chama ambacho kimetekeleza vizuri ilani yake ya uchaguzi?

Ni vipi CHADEMA inaweza shindana na CCM hii imara na madhubuti yenye kuungwa mkono na watumishi wote wa umma,wafanyabiashara, wakulima,vijana ,akina mama,wazee,wanawake na makundi mbalimbali? Ni vipi CHADEMA inaweza kushindana na CCM hii yenye uwezo wa kuweka mawakala hata wawili wawili kila kituo Nchi nzima? Ni vipi CHADEMA hii ambayo inashindwa hata kulipia kodi ya ofisi zake mikoani iweze kushindana na CCM hii yenye nguvu ya kiuchumi na yenye kila aina ya vitega uchumi kuanzia viwanja vya michezo,fremu za maduka n.k.huku pia ikiungwa mkono na watu mbalimbali wenye uwezo mkubwa wa kiuchumi na kifedha?

Ikumbukwe ya kuwa kwa sasa CHADEMA ni dhaifu na dhoofu kuliko wakati mwingine wowote ule katika Historia ya mfumo wa vyama vingi.Haina umoja wala mshikamano na hivyo haiwezi kupanga mikakati na mipango ya pamoja .ndio maana unaona watu kama Lissu wakitoka hadharani kulalamika juu ya kuingia kwa rushwa ndani ya CHADEMA. Sasa kama chama hakina umoja ni vipi kinaweza kushinda Uchaguzi wakati ushindi unapaswa kuanzia ndani ya chama?

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
Embu jaribu kuangalia umebaki muda mfupi sana kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika November 27 Mwaka huu,lakini ukijaribu kufuatilia maandalizi ya CHADEMA huoni kitu chochote kile kinachoendelea,hakuna hata ile hamasa kama iliyokuwepo zamani
Hujaona kanga za Samia zikichomwa na bawacha nchi nzima??
 
Kwa hiyo hizo ndio sera zitakazowapatia kura kutoka kwa Wananchi? Hiyo ni akili au Matope?
Tanzania hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Mtu asiyejitambua au anayefaidika na chaguzi hizi za kihuni tu ndio atajitokeza kushiriki huo upuuzi. Utashiriki vipi uchaguzi ambao chama kimoja kinachoshiriki wahesabu kura wote wanawajibika kwake?
 
Tanzania hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Mtu asiyejitambua au anayefaidika na chaguzi hizi za kihuni tu ndio atajitokeza kushiriki huo upuuzi. Utashiriki vipi uchaguzi ambao chama kimoja kinachoshiriki wahesabu kura wote wanawajibika kwake?
Mkisusa bado CCM tutachaguliwa na watanzania kwa kishindoo kikuu na mkishiriki bado mtashindwa kwa aibu kuu ya kufungia mwaka.kwa hiyo ni Ninyi kuchagua kusuka au kunyoa. Sisi hatuwabembelezi CHADEMA kwa lolote lile. Ila mwisho wa siku ni lazima tuwaongoze tu mtake msitake.
 
Tanzania hakuna uchaguzi, bali kuna maonyesho ya ujinga wa mtu mweusi kwenye box la kura. Mtu asiyejitambua au anayefaidika na chaguzi hizi za kihuni tu ndio atajitokeza kushiriki huo upuuzi. Utashiriki vipi uchaguzi ambao chama kimoja kinachoshiriki wahesabu kura wote wanawajibika kwake?
 
Mkisusa bado CCM tutachaguliwa na watanzania kwa kishindoo kikuu na mkishiriki bado mtashindwa kwa aibu kuu ya kufungia mwaka.kwa hiyo ni Ninyi kuchagua kusuka au kunyoa. Sisi hatuwabembelezi CHADEMA kwa lolote lile. Ila mwisho wa siku ni lazima tuwaongoze tu mtake msitake.
Narudia tena, mngekuwa na uwezo wa kushinda kihalali tungekuwa na tume huru, lakini kwakuwa mnajua hamna uwezo huo, ndio mnalazimisha muwe marefarii, washika vibendera, na makamisaa wa mchezo. Mtu mjinga tu ndio atajitokeza kushiriki huo uhuni akiita ni uchaguzi.
 
Waache wasusie waone kama tutaacha kitu mezani. Tutakula na kukomba kila kitu .na lazima tuwaongoze watake wasitake.
Yaani mnarahisishiwa ili msihangaike kuiba kura, kuachia wapinzani vilema vya maisha na vifo, mnaachiwa goli wazi, na mlivyo vilaza mtajitokeza kushangilia kuwa mmeshinda kwa kishindo😂 Ni hivi, uchaguzi hapa Tanzania ni upuuzi kama upuuzi mwingine.
 
Narudia tena, mngekuwa na uwezo wa kushinda kihalali tungekuwa na tume huru, lakini kwakuwa mnajua hamna uwezo huo, ndio mnalazimisha muwe marefarii, washika vibendera, na makamisaa wa mchezo. Mtu mjinga tu ndio atajitokeza kushiriki huo uhuni akiita ni uchaguzi.
Hata ije Tume ya uchaguzi kutoka Marekani bado CCM itapita na kushinda kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.
 
Yaani mnarahisishiwa ili msihangaike kuiba kura, kuachia wapinzani vilema vya maisha na vifo, mnaachiwa goli wazi, na mlivyo vilaza mtajitokeza kushangilia kuwa mmeshinda kwa kishindo😂 Ni hivi, uchaguzi hapa Tanzania ni upuuzi kama upuuzi mwingine.
Jaribuni kususa muone kama tutaacha kitu mezani. Tutakomba kila kitu .
 
Hata ije Tume ya uchaguzi kutoka Marekani bado CCM itapita na kushinda kwa kishindo kikuu kitakacho itetemesha Dunia nzima.
Huko mbali, kimewashinda nini kukubali tume huru ya uchaguzi? Ukitaka kujua ikija tume huru hasa ya nje nchi hampati kitu, tazama kesi zinazoendeshwa kwenye mahakama za kimataifa mnavyolambishwa mchanga. Kwa huu ushindani wa mbeleko, mtaendelea kutangazwa washindi bila kushinda. Na wajinga tu ndio watajotokeza kuwajazia watu kwenye vituo vya kura.
 
Jaribuni kususa muone kama tutaacha kitu mezani. Tutakomba kila kitu .
Hivyo vyama vishiriki visishiriki hiyo ni kimpango wao, lakini watu tunaojitambua hamuwezi kituona tukiendeka kushiriki huo upuuzi uitwao uchaguzi.
 
Hivyo vyama vishiriki visishiriki hiyo ni kimpango wao, lakini watu tunaojitambua hamuwezi kituona tukiendeka kushiriki huo upuuzi uitwao uchaguzi.
Hata usiposhiriki wewe haupunguzi kitu chochote kile
 
Yaani mnarahisishiwa ili msihangaike kuiba kura, kuachia wapinzani vilema vya maisha na vifo, mnaachiwa goli wazi, na mlivyo vilaza mtajitokeza kushangilia kuwa mmeshinda kwa kishindo😂 Ni hivi, uchaguzi hapa Tanzania ni upuuzi kama upuuzi mwingine.
Hawa watu ni wapumbavu sn
 
Kule ni kujichimbia shimo zaidi, zile ni Siasa za kishamba sana na zisizo na afya ktk mabadiliko.
Kujichimbia shimo kwa kuonyesha aliyeotoa khanga ni kiongozi muovu?
 
Baada ya kuona mwandishi ni yuleyule msifiaji wanaume wengine kila uchwao sikupenda hata kusoma!
 
Back
Top Bottom