CHADEMA wanapenda sana kuwaonea TBC, wengine wenye makosa sawa sio tu kuwafukuza bali hata kulalama hamjawahi

CHADEMA wanapenda sana kuwaonea TBC, wengine wenye makosa sawa sio tu kuwafukuza bali hata kulalama hamjawahi

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Hassan.jpg
Pichani ni marehemu Marine Hassan Marine akisindikizwa na askari kutoka kwenye viwanja vya kampeni Jangwani mwaka 2010 baada ya wapenzi na mashabiki wa CHADEMA wenye jazba kulalama na kumzonga kufuatia matangazo ya moja kwa moja ya TBC kukatika hewani.

August 4, 2020 kulikuwa na mkutano mkuu CHADEMA, TV stations karibu zote hawakushughulishwa na walau kulifanya mubashara pia zilijitokeza online media chache nadhani hazikuzidi tatu waliojitoa kurusha tukio hilo, Mwananchi aliondoka na sauti aidha kwa bahati mbaya au maksudi.

Livestream ya hotuba ya Lissu kwenye Digital Mwananchi iko censored?

Pia August 5, 2020 ITV Superbrand Afrika Mashariki kwenye mkutano mkuu wa ACT Wazalendo, alikaribishwa Tundu Lissu kwenye mkutano huo na punde alivyoanza kuongea, ITV waondoka na sauti aidha kwa maksudi au bahati mbaya lakini pamoja na yote hawajawahi kusumbuliwa wala kufungishiwa virago kwenye majambo yoyote yahusuyo CHADEMA.

ITV siyo sahihi kutoa sauti ya Hotuba ya Tundu Lissu katika Mkutano wa ACT-Wazalendo

Pia nimesahau kidogo muktadha lakini nakumbuka ITV walilipwa na CHADEMA kurusha jambo fulani mubashara, tukio lilipopata moto walianza kuondoka na sauti na baadae kutokomea moja kwa moja kusikojulikana.

Si lengo kusimama na TBC kwa matatizo yake ya uhanahabari na CHADEMA au upinzani kwa ujumla, lakini CHADEMA inaikalia sana kooni TBC kwa matatizo ambayo wengine wanayafanya lakini hawachukui hatua kama ambazo wanazichukua kwa TBC.

Vyombo habari vya binafsi vilitakiwa kuwa huru zaidi kufanya 'coverage' ya upinzani kwa sababu mmiliki wake sio serikali ambayo inaongozwa na chama cha Mapinduzi lakini pamoja na makosa yao, mnaenda kumshikia bango mtu ambaye structure yake ya ufanyaji kazi tayari imembana hata akipenda apindue meza hatoweza. Mnyonge mnyongeni...
 
Bavicha huwa wanatamba Mbowe ni tajiri tangu enzi za Nyerere lakini kila unapofika uchaguzi Chadema huwa hoi sana kipesa kwenye kampeni!!

Mfano uzinduzi wa kampeni leo ni hovyo kabisa na ni dhahiri chadema hawana pesa.

Je utajiri wa Mbowe una manufaa gani kwa Chadema??
 
Nyie CCM mnategema 10% ya ununuzi wa ndege si ndio? Nyie pesa kuja lqanachama anatoa mfukoni mfukoni mwake au ni zilizo pigwa kwenye manunuzi ya ndege
Bavicha huwa wanatamba Mbowe ni tajiri tangu enzi za Nyerere lakini kila unapofika uchaguzi Chadema huwa hoi sana kipesa kwenye kampeni!!

Mfano uzinduzi wa kampeni leo ni hovyo kabisa na ni dhahiri chadema hawana pesa.

Je utajiri wa Mbowe una manufaa gani kwa Chadema??
 
Mkapa alikiri mwaka 2000 alipora billion 200 kwenye mabenki ili wazitumie kwenye kampeni.
 
Back
Top Bottom