Pre GE2025 CHADEMA wavurugana kanda ya Victoria, John Pambalu asusa

Pre GE2025 CHADEMA wavurugana kanda ya Victoria, John Pambalu asusa

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Etwege

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
7,207
Reaction score
17,674
Mwenyekiti wa bavicha na mgombea kiti cha uenyekiti wa Chadema kanda ya Victoria John Pambalu amemtuhumu mshindani wake bwana H Wenje kuwa alihonga wajumbe na pia alisafirisha wajumbe kutoka mikoa mbalimbali kuja Bukoba kupiga kura.

Tuhuma hizo zilimfanya Pambalu kususa na kuondoka akiwa na kundi lake na kuacha uchaguzi ukiendelea ambapo bwana Wenje alishinda kwa kura nyingi.

Akijibu tuhuma hizo bwana Wenje amemkejeli Pambalu kuwa alikuwa anajua atashindwa na hivyo kususa kwake hakumnyimi usingizi. Bwana Wenje amemtaka John Pambalu kukata rufaa kama kweli anaamini alifanyiwa rafu kwenye uchaguzi huo.

Source: Mwananchi
 
SASA MKT WA BIVICHA TENA MKT WA KANDA HAPO NDIO NINI?
 
wanaanza kuonyesha udhaifu mapema hivi na mwenyekiti hatoki kutoa tamko la chama juu ya rushwa iliyo tamalaki ndani ya chama hiki chama hakifai kushika dola
 
mnajimaliza bila kujuwa wananchi wanazidi kuwadharau wanazidi maana tayari walishaga wadharau muda mrefu
Kila Chama kama tulivyo Wanadamu changamoto hazikosekani kama ni kudharauliwa CCM ndio inayodharauliwa mpaka inafikia kuiba Kura na kuua Watu ili tu kibaki madarakani kinyume na matakwa yetu sisi Watanzania.
 
Kumekucha na makucha yake. Yalianzaga mambo kidogo kidogo hivi hivi tena yakawa yanonekana ya kawaida sana mwisho wa siku ikawa historia kwa NCCR na CUF.

CHADEMA kama mnataka yasiwakute yaliyowakuta wenzenu basi uongozi ufuatilie kwa ukaribu sana hizo tuhuma zilizotolewa kwenye uchaguzi wa kanda za Ziwa na Nyasa na mtende haki na haki ionekane imetendeka kwa wagombea wote. Mwisho jikagueni vizuri humo ndani mwenu kwenye uongozi maana mnaweza kuwapigia kelele wakina Halima bungeni kumbe hapo ndani yenu kabisa tayari wahuni washaingia mpaka "bedroom"

Ni mtizamo tu.
 
Hivi Erythrocyte yupo?!!! Mbona hajaileta hii mada uwanjani wakati ye ndo ripota mkuu wa cdm humu, au?!!!!
 
Kumekucha na makucha yake. Yalianzaga mambo kidogo kidogo hivi hivi tena yakawa yanonekana ya kawaida sana mwisho wa siku ikawa historia kwa NCCR na CUF.

CHADEMA kama mnataka yasiwakute yaliyowakuta wenzenu basi uongozi ufuatilie kwa ukaribu sana hizo tuhuma zilizotolewa kwenye uchaguzi wa kanda za Ziwa na Nyasa na mtende haki na haki ionekane imetendeka kwa wagombea wote. Mwisho jikagueni vizuri humo ndani mwenu kwenye uongozi maana mnaweza kuwapigia kelele wakina Halima bungeni kumbe hapo ndani yenu kabisa tayari wahuni washaingia mpaka "bedroom"

Ni mtizamo tu.

Nani afuatilie?
 
Back
Top Bottom