CHADEMA wazidi kuvurugana; CHASO Iringa watoa msimamo mkali kuhusu Katiba Mpya

CHADEMA wazidi kuvurugana; CHASO Iringa watoa msimamo mkali kuhusu Katiba Mpya

PendoLyimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
969
Reaction score
1,055
CHADEMA WAZIDI KUVURUGANA VIJANA WA CHASO IRINGA NAO WATOA MSIMAMO MKALI KUHUSU SUALA KATIBA MPYA.

Katika hali isiyo ya kawaida vijana wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kutoka mkoa wa Iringa wametoa tamko kali kuhusu suala la mchakato wa katiba mpya, mchakato ambao wao kama chama ndiyo wameushikia kidedea licha ya mh Rais kuonesha nia na kwamba wampe muda kwasababu kwanza ndiyo ametoka kupokea kijiti kutoka kwa hayati Dr. John Pombe Joseph Magufuli hivyo anahitaji muda wa kutengeneza uchumi kwanza halafu suala hilo litafuata, jambo ambalo viongozi hao wa juu wa chadema wameligomea kabisa.

Vijana hao ambao wameviambia vyombo vya habari mkoani Iringa kwamba hawapingi suala la katiba mpya katika nchi yetu lakini kinachowafanya watilie mashaka vuguvugu hili ni kwamba halijawahi kuwa kipaumbele chao kuanzia katika sera zao hadi ndani ya katiba yao ya chama jambo ambalo vijana hao wa chadema wanaona kama ni suala la kisiasa lakini siyo takwa la wananchi kama chadema wenyewe wanavodai.

Katiba ya CHADEMA imepuuza vitu vingi sana ndani yake kama vile haina ukomo wa uongozi ndo maana mpaka kesho utakuta mwenyekiti wa chama hicho ni Freeman A. Mbowe pekee na hajawahi kuruhusu mtu mwingine achukua hatamu ya kuongoza chama hicho kongwe hapa nchini kilichoanzishwa tangu miaka ya 1992 huko, vilevile katiba ya CHADEMA haijawahi kuruhusu mwanachama wake yeyote kuhoji chochote kinachoamuriwa na viongozi wa ngazi za juu na kama itatokea mwanachama huyo kufanya hivyo basi ategemee kufutwa uanachama au kuitwa msaliti tuna mifano mikubwa sana ya baadhi ya viongozi kama mtakumbuka akina Zitto Zubery Kabwe, akina Kitila Mkumbo na wengine wengi lakini kwa Iringa pia kuna watu walikihama chama hicho kwasababu ya malumbano ambayo yalikuwa yanakandamiza uhuru wao wa kuongea ndani ya chama hicho

Ukiritimba, ubabe na uonevu uliokithiri ndani ya CHADEMA ni jibu tosha kabisa kwanini vijana wanaanza kutofautiana kimawazo na mwenyekiti wao jambo linalokwamisha kabisa harakati zao za kudai katiba mpya kwasababu zimekuwa ni mbio za kisiasa na wala si takwa la wananchi. Udumavu na ubovu wa katiba ya CHADEMA unawapa maswali mengi sana ambayo majibu yake ni kumfanya kiongozi fulani kuwa kama Mungu mtu na asiyeweza kubadilishwa au kupokelewa kijiti hicho cha kuongoza chama kinachojiita kina demokrasia kumbe ni udanganyifu mkubwa kazi kutafuta ajenda mfu na kuanza kuzisimamia mpaka sasa wanapoteza sifa ya kuwa chama cha watetezi na kuwa chama cha watetea matumbo yao kiufupi hawana jipya.

Siasa za hovyo zisizo kuwa na msingi, siasa ambazo haziheshimu maoni ya wanachama wake limekuwa jambo lenye kukatisha tamaa ndo maana kwa asilimia kubwa ya wanachama wake wanahoji ubora wa katiba yao kwanza kabla hawajaingia kudai katiba ya nchi. Yaani huwezi ukawa unang'ang'ana kutoa kibanzi kwenye jicho la ndugu yako wakati katika macho yako kuna boriti hapo lazima CHADEMA wajitafakari kwanza wajipange upya halafu ndipo waje kutuambia kuhusu katiba mpya.

Mh Rais Samia Suluhu Hassan kwa nia njema anaomba apewe muda na atalifanyia kazi suala hilo lakini CHADEMA wamekuwa wakaidi na kushindwa hata kuheshimu mamlaka ya Taifa hili jambo ambalo limekwaza wengi sana hasa watanzania wa kawaida wanaoipenda nchi yao lakini wenye mapenzi mema kwa Rais wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rai yangu Chadema wanapoona haya mambo wanatakiwa kujitafakari siyo kuanza kutupiana mpira kuwa hizi ni propaganda bali waone ni changamoto wanazopaswa kuzifanyia kazi na siyo kuzipuuzia vinginevyo wataonekana kama chama cha kihuni na vijana hatutakubali kejeli na matusi kwa Rais wetu au mtu yeyote atakaye jaribu kuvuruga amani ya Taifa hili basi tutalala nae mbele. Ahsante.​

IMG-20210729-WA0247.jpg
 
FAKE NEWS!
Ndipo unapoona kuwa CCM wameishiwa. Nguvu zote hizo za nini? Mna jeshi, polisi, TISS and all state machinery at your disposal, sasa ujinga huu wa nini? Wanajua fundo la watanzania lililo moyoni kwa haya wanayotendewa Chadema ndiyo maana wanabuni kilaaina ya mavi!
 
Chadema hawana uhalali wa kupanua mdomo na kudai katiba mpya kwa sababu; katiba ya chama chenyewe inamfanya mwwnyekiti wa chama awe wa kudumu.

Kwa kasoro hiyo kubwa ni vyema uongozi wa chadema waanze kuonyesha mfano kwa kufanya marekebisho ya katiba yao kwanza
 
Sasa Hawa watoto wa shule,wanajua nini kuhusu maisha,hapo wanamikopo wanadaiwa,hawana uhakika wa kupata ajira,na kama ni wasomi na hawajuhi umuhimu wa Katiba,basi ni vilaza,au wameusoma upepo na wanaona hapa bora wawe chawa wa mama,huenda wakapata uteuzi.

Ila sio vibaya kupingana kwa hoja,ndio kukomaa kwenyewe,Chadema sio kama ccm ambako ukimpinga Mwenyekiti,unafukuzwa chamani,hata maisha unaweza kupoteza.
 
Chadema asilia wengi hawapendezwi na hali hii ya kumruhusu muhuni mmoja aendeshe chama kwa style anayotaka yeye, ila sasa hawawezi kufunua vinywa vyao kulisema hili kutokana na usalama wa maisha yao au matumbo yao.

Kwa sababu waliojaribu kufungua vinywa vyao kulizungumzia hili aidha waliuwawa katika mazingira ya kutatanisha kama vile Chacha wangwe, Ben saa8 au kufukuzwa chamani kama vile kina Zito na yule alieambiwa asionje sumu kwa ulimi.

Kwa kweli jamaa wengi wamemchoka na ndio sababu waliamua kwenda kumchongea kweny vyombo vya usalama na baadae kumtelekeza jela.
 
Katika hali isiyo ya kawaida vijana wa chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) kutoka mkoa wa Iringa wametoa tamko kali kuhusu suala la mchakato wa katiba mpya, mchakato ambao wao kama chama ndiyo wameushikia kidedea licha ya mh Rais kuonesha nia na kwamba wampe muda kwasababu kwanza ndiyo ametoka kupokea kijiti kutoka kwa hayati Dr. John Pombe Joseph Magufuli hivyo anahitaji muda wa kutengeneza uchumi kwanza halafu suala hilo litafuata, jambo ambalo viongozi hao wa juu wa chadema wameligomea kabisa.

Vijana hao ambao wameviambia vyombo vya habari mkoani Iringa kwamba hawapingi suala la katiba mpya katika nchi yetu lakini kinachowafanya watilie mashaka vuguvugu hili ni kwamba halijawahi kuwa kipaumbele chao kuanzia katika sera zao hadi ndani ya katiba yao ya chama jambo ambalo vijana hao wa chadema wanaona kama ni suala la kisiasa lakini siyo takwa la wananchi kama chadema wenyewe wanavodai.

Katiba ya CHADEMA imepuuza vitu vingi sana ndani yake kama vile haina ukomo wa uongozi ndo maana mpaka kesho utakuta mwenyekiti wa chama hicho ni Freeman A. Mbowe pekee na hajawahi kuruhusu mtu mwingine achukua hatamu ya kuongoza chama hicho kongwe hapa nchini kilichoanzishwa tangu miaka ya 1992 huko, vilevile katiba ya CHADEMA haijawahi kuruhusu mwanachama wake yeyote kuhoji chochote kinachoamuriwa na viongozi wa ngazi za juu na kama itatokea mwanachama huyo kufanya hivyo basi ategemee kufutwa uanachama au kuitwa msaliti tuna mifano mikubwa sana ya baadhi ya viongozi kama mtakumbuka akina Zitto Zubery Kabwe, akina Kitila Mkumbo na wengine wengi lakini kwa Iringa pia kuna watu walikihama chama hicho kwasababu ya malumbano ambayo yalikuwa yanakandamiza uhuru wao wa kuongea ndani ya chama hicho

Ukiritimba, ubabe na uonevu uliokithiri ndani ya CHADEMA ni jibu tosha kabisa kwanini vijana wanaanza kutofautiana kimawazo na mwenyekiti wao jambo linalokwamisha kabisa harakati zao za kudai katiba mpya kwasababu zimekuwa ni mbio za kisiasa na wala si takwa la wananchi. Udumavu na ubovu wa katiba ya CHADEMA unawapa maswali mengi sana ambayo majibu yake ni kumfanya kiongozi fulani kuwa kama Mungu mtu na asiyeweza kubadilishwa au kupokelewa kijiti hicho cha kuongoza chama kinachojiita kina demokrasia kumbe ni udanganyifu mkubwa kazi kutafuta ajenda mfu na kuanza kuzisimamia mpaka sasa wanapoteza sifa ya kuwa chama cha watetezi na kuwa chama cha watetea matumbo yao kiufupi hawana jipya.

Siasa za hovyo zisizo kuwa na msingi, siasa ambazo haziheshimu maoni ya wanachama wake limekuwa jambo lenye kukatisha tamaa ndo maana kwa asilimia kubwa ya wanachama wake wanahoji ubora wa katiba yao kwanza kabla hawajaingia kudai katiba ya nchi. Yaani huwezi ukawa unang'ang'ana kutoa kibanzi kwenye jicho la ndugu yako wakati katika macho yako kuna boriti hapo lazima CHADEMA wajitafakari kwanza wajipange upya halafu ndipo waje kutuambia kuhusu katiba mpya.

Mh Rais Samia Suluhu Hassan kwa nia njema anaomba apewe muda na atalifanyia kazi suala hilo lakini CHADEMA wamekuwa wakaidi na kushindwa hata kuheshimu mamlaka ya Taifa hili jambo ambalo limekwaza wengi sana hasa watanzania wa kawaida wanaoipenda nchi yao lakini wenye mapenzi mema kwa Rais wetu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Rai yangu Chadema wanapoona haya mambo wanatakiwa kujitafakari siyo kuanza kutupiana mpira kuwa hizi ni propaganda bali waone ni changamoto wanazopaswa kuzifanyia kazi na siyo kuzipuuzia vinginevyo wataonekana kama chama cha kihuni na vijana hatutakubali kejeli na matusi kwa Rais wetu au mtu yeyote atakaye jaribu kuvuruga amani ya Taifa hili basi tutalala nae mbele. Ahsante
 
LAZIMA BAVICHA WAJE WASEME HUU SIYO WARAKA WA WANACHADEMA WATASEMA NI CCM NDIYO CHADEMA INAANZA KUGAWANYIKA TARATIIBU KWA KUKOSA MAARIFA NA MWENYEKITI WA KUDUMU MBOWE ANAYENYEA NDOO SASA HIVI KWA UGAIDI WAKE
 
CCM mmewakusanya wanywa gongo na mateja wasio zidi 8 na kuwapa tamko alafu mnawaita ni chaso wa Iringa!!!! kweli mmeishiwa kila kitu……………..
 
Kuna ukweli ambao tutazidi kuupinga silu zote lakini ndio ukweli,
Katiba ya chadema haina demokrasia hata kidogo,ni kwa sababu mwanzilishi wa chama ndiye aliyeiandaa na hajatoa fursa ya wanachama kuipitia ilikurekebisha kasoro hizo uambo ambalolitazidi kuwakatisha tamaa wanachama wake kila anayejielewa.

Kuna ukiritimba mwingi sana ndani ya chadema, mnakumbuka hata upatikanaji wa wabinge wa viti maalumu kutoka chadema?
Mnakumbuka wale wabunge walivyofunguka bungeni kuwa wanalazimika kutoa mili yao ili kupata nafasi hizo kwa mwenyekiti wao?

Mnakumbuka kuwa inabidi kila mbunge atoe % kadhaa kwa ajili ya mfuko wa chama jambo ambalo mtu hana uhuru wankuamua kufanya hivyo ama la?

Ukija kwenye jambo jingine la kawaida kabisa,hata uanachama una segregation, yaani kuna wanachama wajuu, wakati, wachini na wachi kabisa, sasa hapa tunahibiri kwa wanachama?
Maana yake ni kuwa hata rights za chama hazifanani kwa hawa watu jambo linalozidi kuonesha udhaifu wa katiba na miongozo ya chama chetu
 
Back
Top Bottom