CHADEMA yataka Tanganyika irudishwe

si kweli kwamba hautaki muungano tatizo ni muungano wa kulazimishana watu wengi wanapenda muungano lakini on mutual respect and benefits.. mimi naunga muunga uwe moja "one country" well managed na katiba inayotoa fursa sawa

Anayefikiria kuuvunja muungano ni mtu aliyekata tamaa tu na hajaelimishwa vizuri...after all those years lililo bora ni kwenda mbele zaidi

watu kama wewe na wengine ni kuwaacha na kuwapuuza sisi tunaanagalia mbele zaidi na vizazi vijavyo..

hakuna ambacho ni kero za muungano ambazo haziwezi kupata ufumbuzi hakuna kabisaa ila ni type ya viongozi tulio nao zenj na bara ambao hawafanyi maamuzi kwa manufaa ya watu
 

Utaukubalije muungano ambao unauona ni wa kulazimishana? Ndiyo maana kuna umuhimu wa kuwa na referendum. Wenye nchi waulizwe kwa dhati kama wanautaka huu muungano. Kama wakiukubali, ndiyo tuanze kuangalia namna gani tunaweza kuishi pamoja kwa kuheshimiana.

Hizo mnazoita kero za muungano haziwezi kushughulikiwa katika hali ya sasa hivi ambapo hakuna mwenye uhakika kama muungano wenyewe unakubalika.

Mimi ndiyo maana nikasema tujifunze kwa Czechoslovakia na si Yugoslavia. Czechoslovakia walifanya referendum, upande mmoja ukakataa muungano, wakakaa wakagawana walicholuwa nacho na mpaka sasa hivi Czech Republic na Slovakia zinadunda. Yugoslavia walikataa kusikiza manung'uniko ya Slovenia, wakataka kulazimisha muungano. Matokeo yake ni umwagaji wa damu, uharibu wa nchi yenyewe na chuki inayoendelea hadi leo! Mwenye macho haambiwi tazama.

Amandla..........
 
Mnyika matatizo yenu yamewashinda utaweza ya Muungano
 
referendum OK
lakini chama kinaweza kuja na agenda ya kwamba tunataka serikali ya Tanganyika kinadanganya wananchi as if watanaganyika waote tunataka serikali hiyo? huo ndio ugonjwa wao chadema.

Hakuna cha umwagaji damu labda kama wewe unapenda kuona damu inamwagika...lol unapenda kubashiri shari

kero za muungano wakati mwingine ni siasa zaidi kuliko uhalisia ndio maana nilisema hapo juu kwamba kuna viongozi wa zenj na bara huo unakuwawaga mtaji wa kisiasa hakuna mwenye nia ya dhati kabisa kumaliza tatizo ..maana kwa mtazamo wangu ni jambo dogo sana.
 
wajamani mnakana chimbuko la mababu na mabibi kiasi hiki huku mkiwa macho makavu ,binafsi watu kama hawa nawaita makatili wa nafsi zao na jamii zao ,akhsante wana Chadema ,Mungu ibariki TANGANYIKA isimame tena .
 
Mbona zanzibar ipo na serikali yake wahy sisi, Kuna tafiti kibao zilifanyika na kuona kuwa Muungani wetu inapaswa urekebishwe na pia uwe na serikali mbili na kila upande ufaidi matunda yake
 
hivi kuna tunachofaidi kwas uwepo wa muungano zaidi ya kuwaenzi waasisi wetru?......ila kumbukeni dhambi ya ubaguzi itatufuata..........
 

Usijidanganye. Zanzibar imemwagwa damu mara ngapi? Sisi bara huko Tarime, Karatu, Dar es Salaam n.k. kote damu imeishamwagika. Hatuna tofauti na jirani zetu wa Kenya, Uganda, Burundi, DRC n.k. Tukifanya mashara tutaivuna hiyo shari. Ndiyo maana wengine tunasema kuwa kuna umuhimu wa ku-legitimise huu Muungano mapema iwezekanavyo kwa referendum iliyo wazi na ya haki. Tunaogopa nini kuwauliz wananchi kama wanautaka huu muungano? Canada walifanya makelele ya Quebec yalipozidi na sasa wametulia maana wananchi wa Quebec waliulizwa na wakasema wanataka kubaki katika Canada moja. Mchezo ukaisha!

Amandla.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…