Chagga Day: Tuikumbuke siku hii kwa rejea za Rajabu Ibrahim Kirama na Muro Mboyo 1800

Chagga Day: Tuikumbuke siku hii kwa rejea za Rajabu Ibrahim Kirama na Muro Mboyo 1800

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
CHAGGA DAY

TUIKUMBUKE SIKU HII KWA KUREJEA KATIKA MAISHA YA RAJABU IBRAHIM KIRAMA NA BABA YAKE MURO MBOYO KATIKA MIAKA YA 1800

Chagga Day ni siku iliyokuwa ikiadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 10 Novemba na kwa hakika ilikuwa sikukuu kubwa sana.

Sherehe zikifanyika Chagga Council Kiborloni.

Wachagga toka zama hizo walijihisi na kujiona ni taifa na ardhi yao yote ni nchi kamili.

Nchi yenye mipaka yake ya kueleweka.

Wenye lugha moja lau kama makabila yao ni mengi na yakiishi sehemu mbalimbali chini ya mlima.

Ulikuwa wakati wa watawala (Mangi) mfano wa Mangi Ndeseruo Mamkinga wa Machame na wale waliomfuata katika kiti hicho Shangali Ndeseruo na Abdiel Shangali.

Pamoja na hawa watawala wenye sifa alikuwapo Muro Mboyo, Jemadari wa majeshi ya Mangi Ndeseruo Mamkinga, Muro Mboyo na mwanae Rajabu Ibrahim Kirama.

Hii ilikuwa kutokea miaka ya katikati ya 1800 kuingia 1900.

Kilimanjaro uliwaongezea Wachagga mapenzi kwa nchi yao kwa ajili ya ule uzuri wake.

Mlima umesimama ukiinamia ardhi yote; hasa unapokuwa haujafunikwa na mawingu kwani kuna siku Wachagga huamka na wasiuone mlima.

Wachagga wanaamini bila Mlima Kilimanjaro hakuna Wachagga.

Na hakika kabisa unaweza mtu ukafikiria na kusema kuwa, Mlima Kilimanjaro ni nembo ya matumaini makubwa wa ustawi wa Wachagga.

Mlima pia ni sawa na alama inayomuonesha rafiki au adui, walipo Wachagga.

Ikiwa una haja nao na unawatafuta iwe kwa kheri ama kwa shari.

Kwa anayekuja, kokote anapotokea iwe kutoka pwani ya mbali za ardhi ya Wachagga; au nyuma ya mlima, kutokea Kenya, Mlima Kilimanjaro utaonekana umesimama hausogei pale ulipo.

Na kila unapoukaribia ndipo unapozidi kujidhihirisha ukubwa na uzuri wake.

Umuhimu wa Muro Mboyo ilikuwa kuona kuwa yeye bila shaka ndiye alikuwa na mengi ya kuhadithia katika historia ya Machame ni kuwa aliishi akashuhudia kwa macho yake mwenyewe taratibu nguvu za utawala wa ukoo wa Mangi Shangali nchini kwake Machame ukipotea na utawala mpya wa wakoloni Wajerumani ukiingia Uchaggani pote.

Bila shaka mabadiliko haya yalimsababishia Muro Mboyo simanzi kwa kukumbuka historia ya nguvu ya ukoo wake, wa majemadari wa vita, ukipotea na kuchukuliwa na wageni kutoka mbali kwenye nchi ambayo hakupata kuijua wala kuisikia.

Wageni hawa wakaja na utawala mpya na silaha mpya za vita zenye nguvu kubwa ya kuua na kuangamiza kutoka mbali.

Wageni hawa kutoka Ulaya pia wakawaeleza kuwa Mungu wa Wachagga si Mungu ila Mungu wa kweli ni Yesu Kristo wa Nazareth.

Si yule Mungu wao aishie Mlima Kilimanjaro kwenye vilele vya Kibo na Mawenzi.

Muro Mboyo alimweleza mwanaye Kirama historia hii ya Wachagga kama njia moja ya kufuta aibu iliyomgubika yeye binafsi na kwa hakika Wachagga wote ya kujikuta wao ni taifa lililo chini ya utawala wa taifa jingine la watu weupe.

Muro Mboyo hakuwa tena na majeshi ya kuongoza yakimfuata nyuma vitani kulinda utawala wa Shangali.

Muro Mboyo kuikumbuka historia ya wazee na kumuhadithia mwanae Rajabu Kirama ilikuwa moja ya njia ya kupata faraja na kurejesha heshima yake na ya watu wake kama vile kusema kuwa na sisi tulikuwa taifa kama wao Wajerumani.

Kwa miaka mingi Chagga Day ilibaki kuwa siku ya kukumbuka Taifa la Wachagga na sikukuu hii ilimalizikia na Paramount Chief Thomas Marealle baada ya Tanganyika kuwa nchi huru.

Picha: Mangi Shangali Ndeseruo, Rajabu Ibrahim Kirama, Chief Abdiel Shangali na Mangi Mkuu Thomas Marealle.

Screenshot_20201110-231728.jpg
IMG-20200926-WA0113.jpg
Screenshot_20201110-232630.jpg
Screenshot_20201110-232826.jpg
 
Mohamed Said,

Batafuta hotuba ya Mangi Thomas Marealle aliyoitoa UN.

Kaama unayo katika makabrasha yako naomba utuwekee katika jukwaa letu.
 
kitali,

Umesema kweli siijui historia ya Wachagga ila kidogo tu ya Rajabu Ibrahim Kirama aliyeingiza Uislam Uchaggani na nimeandika kitabu cha maisha yake.

Nje ya hapa sina nikijuacho.
 
Earl Seaton na Sosthenes Maliti kwenye kitabu chao cha Tanzania Treaty Practice 1972 wameandika kwamba, kuna kipindi machifu wa Uchagani walisaini mkataba na Sultani wa Zanzibar ili wawe chini ya utawala wake (Suzerain).

Hii ilifanyika hata kabla ya mkutano wa Berlin wa mwaka 1884-1885. Tatizo lilitokea pale ambapo balozi wa Sultani huku bara aliyeitwa Ahmed Salim kushirikiana na Wajerumani kama Dr Carl Peters na Dr Karl Jhulke kusema kwamba Zanzibar haikuwahi kuwa na madai yoyote huku Tanganyika.

Baada ya mkutano wa Berlin, Sultan wa Zanzibar akisaidiwa na Uingereza aliandaa barua za madai ambazo zilipinga Ujerumani kujitwalia baadhi ya maeneo ya huku bara akidai kwamba hata kabla ya Wajerumani kusaini mikataba na machifu wa huku bara, Zanzibar ilikuwa tayari imeshasaini hiyo mikataba.

Hili walilimaliza kwa njia za kidiplomasia na makubaliano. Kama Zanzibar ingefanikiwa kutawala baadhi ya maeneo ya huku bara, nadhani Uislamu ungefika kwa kiwango kikubwa sana maeneo ya Kaskazini sehemu kama Kilimanjaro na Arusha.
 
julaibibi,

Ingawa yeye kanifanyia ujuvi hapana faida kwetu sote mie nimrejeshee ujuvi.

Nimemjibu kiungwana huenda akajirudi na kujifunza tabia njema.
 
kitali,

Umesema kweli siijui historia ya Wachagga ila kidogo tu ya Rajabu Ibrahim Kirama aliyeingiza Uislam Uchaggani na nimeandika kitabu cha maisha yake.

Nje ya hapa sina nikijuacho.
Sasa hizo habari za kirama kuongoza jesh la shangali umeipata wap.
 
Kitali,
Nimefanya utafiti Machame Nkuu.

Nakujibu nikiamini unatafuta elimu.
Shangali na mandara wap na wap chief. Shangali huyu wa juz. Na kwa taarifa yako mi kijijin kwetu kulikuwepo babu wa 1880 ameenda uarabun miaka 1915 akarud akiwa muislam aliyesomea kabisa ndie aliyeacha hiyo dini kwetu. Alikufa 1990. So fanya utafit upya japo unajiita mwanahistoria nadhan historia ya waislam.
 
Shangali na mandara wap na wap chief. Shangali huyu wa juz. Na kwa taarifa yako mi kijijin kwetu kulikuwepo babu wa 1880 ameenda uarabun miaka 1915 akarud akiwa muislam aliyesomea kabisa ndie aliyeacha hiyo dini kwetu. Alikufa 1990. So fanya utafit upya japo unajiita mwanahistoria nadhan historia ya waislam.
Kitali,
Sijui kwa nini umehamaki sifahamu ni kitu gani kimekuudhi katika kitabu changu.

Lakini naona hii imekuwa kama kawaida kila unapotoka utafiti mpya.

Mwaka wa 1988 gazeti la Africa Events (London) lilichapa makala yangu, "In Praice of Ancestors," paliingia taharuki kubwa gazeti lote likakusanywa lisisomwe.

Ikafatia barua kali kwenye gazeti hilo kujibu makala yangu.

Sasa hapa naona na wewe umefuata hali ile ile umeghadhibika unanishambulia.

Angalau basi ungekuwa unaijua historia hii ukanisahihisha pale nilipokosea.

Huna moja ulijualo lakini unataka kufanya mjadala na mimi niliyefanya utafiti na kuandika kitabu.

Ukisoma kitabu kitakupeleka nyuma miaka kwenye historia ya koo mbili zilizotawala Machame kwa nafasi za Mangi na Jemadari wa Vita.

Utasoma historia ya ukoo wa Ndesaruo Mamkinga na ukoo wa Nkya.

Hawa ndiyo wazee wa akina Shangali na Muro Mboyo.

Muro Mboyo akiwa Jemadari wa Ndesaruo Mamkinga alikimbilia Old Moshi kwa Rindi Mandara kutafuta hifadhi baada ya mtafaruku baina yake na Mangi.

Aliyekuwa Muislam ambae wewe hata jina lake hulijui ni Ngulelo mtoto wa Ndesaruo Mamkinga na hakuupatia Arabuni bali Kismayu Somalia.

Hawa wote ni ukoo wa Shangali.

Mjukuu wa Ngulelo yu hai yuko Nkuu na ni bi mkubwa wa heshima hapo kijijini na ni Muislam.

Upande wa baba yake ndiyo hawa akina Nkya.

Mama yake ni dada wa Chief Shangali aliyesilimishwa na Rajabu Ibrahim Kirama akamuoa.

Naijua vyema historia ya koo hizi mbili.

Soma kitabu kitakufunza mengi.

Haipendezi kufaja mjadala kama huu ukiwa katika hali ya ujinga.
 
Shangali ndie mangi wa mwisho pale machame na mandara ni wa miaka ya 1880 huko so hicho unachozungumza sio kweli. Mi pia ni mzaliwa wa koo za mangi chief sio kila tafiti ni za kweli. Wala unaemsemea kasoma somali wala humjui unapewa stor unazotaka ili uandike kinachokufurahisha.
 
Shangali ndie mangi wa mwisho pale machame na mandara ni wa miaka ya 1880 huko so hicho unachozungumza sio kweli. Mi pia ni mzaliwa wa koo za mangi chief sio kila tafiti ni za kweli. Wala unaemsemea kasoma somali wala humjui unapewa stor unazotaka ili uandike kinachokufurahisha.
Kitali,
Kipi ninachozungumza ambacho si kweli?

Hapa hujasema lolote la kueleweka.

Mimi nafahamu Abdiel Shangali ni Mangi wa mwisho Machame na ukisoma kitabu utaona nimeandika changamoto nyingi zilizowakuta watawala baada ya kuingia Wajerumani.

Nina historia ya urafiki mkubwa baina ya Muro Mboyo na Mjerumani Bruno Gutmann kutoka Liepzig Mission.

Nenda Kidia Mission Old Moshi kasome na kashuhudie.

Gutmann kamkuta Muro Mboyo Old Moshi yuko uhamishoni tena kamkuta mtu mwenye nafanikio makubwa sana katika kilimo na ufugaji.

Gutmann akikisema Kichagga utadhani kazaliwa nacho kiasi Wachagga wakampachika jina wakamwita "Babu wa Wachagga."

Gutmann aliweza kuwabatiza wazee wote maarufu pale Old Moshi ila Muro Mboyo.

Lakini katika kutaka kumfurahisha rafiki yake, Muro alimpa ardhi ambayo Gutmann alijenga kanisa.

Mangi Meli ananyongwa na Wajerumani mbele ya watu wake Muro yuko Old Moshi.

Muro Mboyo alirudi nyumbani kwake Nkuu na alisilimu na jina alilochagua ni Ibrahim na aliyemsilimisha ni mwanae mtoto wa mke wake Makshani mwanamke kutoka Kibosho na ndiye mama yake Rajabu Ibrahim Kirama.

Rajabu Kirama amelelewa na Mangi Sina hadi alipokuwa mkubwa ndiyo akaenda kumtafuta baba yake Old Moshi.

Mzee Rajabu alipofariki mwaka wa 1962 akiwa na miaka zaidi ya 100 alimwachia mwanae Salim hazina kubwa sana ya nyaraka na nyaraka hizi zikatunzwa na wajukuu hadi zikanifikia mimi.

Baadhi ya nyaraka hizi zimeandikwa kwa mkono na nyingine kwa mashine na humu utawasoma akina Petro Njau, Joseph Merinyo, Chief Thomas Marealle, Chief Abdiel Shangali, Gavana George Stewart, Al Habib Sayyid Omar bin Sumeit, Sheikh Hassan bin Ameir Sultani Sayyid Khalifa bin Haroub na wengine wengi.

Ndugu yangu punguza hasira kisome kitabu na ukiwa utakuta makosa nifahamishe tufanye masahihisho kwani kazi yoyote ya mikono ya binadamu haiwezi kukosa makosa.
 
Shangali ndie mangi wa mwisho pale machame na mandara ni wa miaka ya 1880 huko so hicho unachozungumza sio kweli. Mi pia ni mzaliwa wa koo za mangi chief sio kila tafiti ni za kweli. Wala unaemsemea kasoma somali wala humjui unapewa stor unazotaka ili uandike kinachokufurahisha.
leta yako basi tusome tuone wap mzee kakosea.
ukitaka kubishana baina ya tafit lazima ulete yako.unless unataka kuleta umbea hapa.
no research no right to speak.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tafiti nyingine zinakuwa na majibu hata kabla ya utafiti
 
Shangali ndie mangi wa mwisho pale machame na mandara ni wa miaka ya 1880 huko so hicho unachozungumza sio kweli. Mi pia ni mzaliwa wa koo za mangi chief sio kila tafiti ni za kweli. Wala unaemsemea kasoma somali wala humjui unapewa stor unazotaka ili uandike kinachokufurahisha.
Wewe unaonekana una ujuaji mwingi Ila unamuattack mzee wa watu bila hata fact moja kazi kujifanya umetokea ukoo wa chief lete sasa hiyo story yako mjukuu wa chief tuone unarekebisha wapi sio kupinga in general haileti maana kabisa.
 
Shangali ndie mangi wa mwisho pale machame na mandara ni wa miaka ya 1880 huko so hicho unachozungumza sio kweli. Mi pia ni mzaliwa wa koo za mangi chief sio kila tafiti ni za kweli. Wala unaemsemea kasoma somali wala humjui unapewa stor unazotaka ili uandike kinachokufurahisha.
Wewe unaonekana una ujuaji mwingi Ila unamuattack mzee wa watu bila hata fact moja kazi kujifanya umetokea ukoo wa chief lete sasa hiyo story yako mjukuu wa chief tuone unarekebisha wapi sio kupinga in general haileti maana kabisa.
 
Kitali,
Kipi ninachozungumza ambacho si kweli?

Hapa hujasema lolote la kueleweka.

Mimi nafahamu Abdiel Shangali ni Mangi wa mwisho Machame na ukisoma kitabu utaona nimeandika changamoto nyingi zilizowakuta watawala baada ya kuingia Wajerumani.

Nina historia ya urafiki mkubwa baina ya Muro Mboyo na Mjerumani Bruno Gutmann kutoka Liepzig Mission.

Nenda Kidia Mission Old Moshi kasome na kashuhudie.

Gutmann kamkuta Muro Mboyo Old Moshi yuko uhamishoni tena kamkuta mtu mwenye nafanikio makubwa sana katika kilimo na ufugaji.

Gutmann akikisema Kichagga utadhani kazaliwa nacho kiasi Wachagga wakampachika jina wakamwita "Babu wa Wachagga."

Gutmann aliweza kuwabatiza wazee wote maarufu pale Old Moshi ila Muro Mboyo.

Lakini katika kutaka kumfurahisha rafiki yake, Muro alimpa ardhi ambayo Gutmann alijenga kanisa.

Mangi Meli ananyongwa na Wajerumani mbele ya watu wake Muro yuko Old Moshi.

Muro Mboyo alirudi nyumbani kwake Nkuu na alisilimu na jina alilochagua ni Ibrahim na aliyemsilimisha ni mwanae mtoto wa mke wake Makshani mwanamke kutoka Kibosho na ndiye mama yake Rajabu Ibrahim Kirama.

Rajabu Kirama amelelewa na Mangi Sina hadi alipokuwa mkubwa ndiyo akaenda kumtafuta baba yake Old Moshi.

Mzee Rajabu alipofariki mwaka wa 1962 akiwa na miaka zaidi ya 100 alimwachia mwanae Salim hazina kubwa sana ya nyaraka na nyaraka hizi zikatunzwa na wajukuu hadi zikanifikia mimi.

Baadhi ya nyaraka hizi zimeandikwa kwa mkono na nyingine kwa mashine na humu utawasoma akina Petro Njau, Joseph Merinyo, Chief Thomas Marealle, Chief Abdiel Shangali, Gavana George Stewart, Al Habib Sayyid Omar bin Sumeit, Sheikh Hassan bin Ameir Sultani Sayyid Khalifa bin Haroub na wengine wengi.

Ndugu yangu punguza hasira kisome kitabu na ukiwa utakuta makosa nifahamishe tufanye masahihisho kwani kazi yoyote ya mikono ya binadamu haiwezi kukosa makosa.
Mzee Allah amekujaalia busara nyingi sana.
 
Back
Top Bottom