Chaguo la Serikali mbili mbele kuna Giza nene

Chaguo la Serikali mbili mbele kuna Giza nene

Kabengwe

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2009
Posts
240
Reaction score
47
Nimekuwa kimya nikisikiliza kila wadau wanapotoa na kujenga hoja zao za ama serikali mbili au serikali tatu; binafsi nakosa mantiki ya nini hasa makundi haya yanachopigania; ila kama wote tunalenga kuuimarisha Muungano na kuijenga Tanzania iliyo bora zaidi na yenye mshikamano, nadhani sote tuko upande mmoja na tunafikiria jambo ambalo ni zuri kupindukia.


Kumbe kama ni hivyo kwa mwenye kuielewa maantiki hiyo hangelisita kupigia chapio kuwe na Serikali moja yenye kutunza maslahi ya pande zilizounda Muungano wa serikali hii.


Lakini mimi kwa uelewa wangu ninaangalia mambo mawili muhimu katika matukio ya nchi yetu hii:
I. Mwaka 1962 vyama vingi vya siasa vilifutwa kwa maslahi yaliyokuwepo enzi hizo. Na Marehemu Baba wa Taifa Mwl JK Nyerere aliekuwa Kiongozi wa Nchi yetu alikubaliana na uamuzi wa kuwa na chama kimoja tu cha siasa na kulisimamia hilo kwa umakini na ukamilifu wote. Mwaka 1989 wakati wananchi na hasa wanachama wa CCM wakihojiwa kuanzishwe vyama vingi vya siasa ama hapana, iliezwa matokeo yalikuwa asilimia 80 walisema hapana na waliokubali kuwe na vyama vingi vya siasa wakawa 20% tu. Lakini uhalisia wa kisiasa uliokuwepo wakati huo mwaka 1989 ulikuwa tofauti na matokeo ya kura. Mwalimu aliwaeleza Watanzania akiwafumbua macho kuwa pamoja na wingi wa Wana CCM waliokataa kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa, aliwaambia "hilo kwa sasa HALIEPUKIKI, kwani sababu zilizoifanya nchi iwe na mfumo wa chama kimoja za mwaka 1962 hazipo tena na hazibebi uzito wowote kwa enzi za wakati huo". Matokeo yake mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulianza.


II. Sikumbuki mwaka ila nakumbuka kipindi Fulani kulifumuka kundi ndani ya Bunge lililojiita G8. Hawa G8 walikuwa watetezi wa kuanzishwa upya serikali ya Tanganyika. Kundi hili lilikemewa sana na Baba wa Taifa Mwl JK Nyerere akidai kuwa walikuwa hawana uhahali wowote wa kudai kitu kama kile na kwamba walikiuka kuilinda katiba ya nchi kama walivyokuwa wameapishwa. Nami nasema Mwl alikuwa sahihi 100% kwa kuwakemea hao, kwani hao walifumuka tu pasipo utaratibu maalumu uliondaliwa wa kwenda na hoja ya jambo nyeti kama hilo.


Leo hii yeyote anayekataa kudai muundo bora kabisa wa serikali ya Tanzania baada ya Rais kuunda chombo cha kuandaa katiba mpya ya nchi yetu ambacho ndio utaratibu Mwalimu alikuwa anaueleza kuwa haukuwepo, atakuwa haitendei haki Tanzania. Tume ya mabadiliko ya Katiba imekuja na mapendekezo bora kabisa yaliyotoka kwa wananchi na yaliyofanyiwa utafiti wa kina ya muundo ulio bora kabisa wa serikali yetu. Mimi binafsi ninaamini kuwa Mwl angekuwepo leo kwa utaratibu huu uliofanyika hangesita katika kumuunga mkono Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mhe Jaji Warioba kwa kutofautiana na wajumbe wengi wa Chama cha Mapinduzi; Kama ilivyokuwa kwa vyama vingi na chama kimoja.


Bado naamin Mwalimu aliyekuwa mmojawapo wa waasisi wa Muungano baina ya Tanganyika na Zanzibar pamoja na Mzee wetu Marehemu Sheikh Amri Abeid Amani Karume mwaka 1964; Kama alivyowafumbua macho Watanzania mwaka 1989 wakati ule ili tuwe na vyama vingi vya siasa ama la, leo pia angewafumbua macho tena Watanzania mara baada ya rasimu ya pili kukabidhiwa na angewaambia "Wenzetu wanaoenda bunge la Katiba wachague moja kati ya haya, Serikali moja ama Serikali tatu" hiyo ni kulingana na UZITO wa hoja za Wananchi walizozitoa mbele ya Tume.


Mimi nimelonga ya kwangu, lakini chaguo la serikali mbili MBELE kuna giza NENE.


Kabengwe@jamiiforums.com
 
Kabengwe
Naomba kwanza niweke kumbu kumbu sawa kuwa vyama vingi vilifutwa 1965 kama nipo sahihi.

Pili, serikali mbili haziwezekani kwa sasa kutokana na mabadiliko ya mazingira, kutoka yale ya 1964 na sasa

Tatu, tume zote zilizoundwa kwa miaka 20, zaidi ya 5 hakuna hata moja iliyosimama na mfumo wa sasa.

Nne, tume ya Warioba imeundwa na Rais wa chama tawala. Kila hatua tume iliyopitia rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM alifahamishwa, naye kuifahamisha kamati kuu ya chama chake.

Wajumbe wa tume ni watu waliochaguliwa kwa sifa za weledi wao. Hatutegemei kama kuna utafiti mwingine uliogharim serikali unaoweza kuja na kitu kingine zaidi ya tume ya Warioba.

Tano,maoni ni ya wananchi na si kikundi . Inashangaza kama wapo watakaodhani wana mandate zaidi ya wenye nchi.

Sita, mfumo uliopendekezwa ndio ule uliokuwa unapigiwa debe na wznz siku nyingi. Inashangaza wznz hao hao hawataki mfumo ule ule walioutaka.

Saba, serikali moja haiwezekani kwasababu mbili hazikuonyesha uwezekano huo kutokana na migogoro iliyodumu miaka 50.

Nane, hakuna namna nyingine iliyobaki ambayo inaweza ku sustain serikali 2. Kama zipo njia nyingine ni zipi hizo ambazo hazikutumika miaka 50?

Tisa, Tayari znz imeonekana kutoithamini katiba ya JMT. Kuendelea na serikali 2 ni kulea kidonda kinachotoa harufu na kupalilia njia ya kwenda kuvunja muungano kama kuna ulazima wa kuwepo.

Kumi, serikali moja haiwezekani kwasababu tayari kuna 'sisi' na wao. Kuna kujivuna kwa kutumia majina. Hali hiyo imepelekea uwepo wa mahitaji ya 'wao' ambao ni Watanganyika wanaotaka identity yao. Haiwezekani muungano ukabebwa na taifa moja.
wazungu wanasema 'it takes two to tangle'.
 
Kabengwe
Naomba kwanza niweke kumbu kumbu sawa kuwa vyama vingi vilifutwa 1965 kama nipo sahihi.

Pili, serikali mbili haziwezekani kwa sasa kutokana na mabadiliko ya mazingira, kutoka yale ya 1964 na sasa

Tatu, tume zote zilizoundwa kwa miaka 20, zaidi ya 5 hakuna hata moja iliyosimama na mfumo wa sasa.

Nne, tume ya Warioba imeundwa na Rais wa chama tawala. Kila hatua tume iliyopitia rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM alifahamishwa, naye kuifahamisha kamati kuu ya chama chake.

Wajumbe wa tume ni watu waliochaguliwa kwa sifa za weledi wao. Hatutegemei kama kuna utafiti mwingine uliogharim serikali unaoweza kuja na kitu kingine zaidi ya tume ya Warioba.

Tano,maoni ni ya wananchi na si kikundi . Inashangaza kama wapo watakaodhani wana mandate zaidi ya wenye nchi.

Sita, mfumo uliopendekezwa ndio ule uliokuwa unapigiwa debe na wznz siku nyingi. Inashangaza wznz hao hao hawataki mfumo ule ule walioutaka.

Saba, serikali moja haiwezekani kwasababu mbili hazikuonyesha uwezekano huo kutokana na migogoro iliyodumu miaka 50.

Nane, hakuna namna nyingine iliyobaki ambayo inaweza ku sustain serikali 2. Kama zipo njia nyingine ni zipi hizo ambazo hazikutumika miaka 50?

Tisa, Tayari znz imeonekana kutoithamini katiba ya JMT. Kuendelea na serikali 2 ni kulea kidonda kinachotoa harufu na kupalilia njia ya kwenda kuvunja muungano kama kuna ulazima wa kuwepo.

Kumi, serikali moja haiwezekani kwasababu tayari kuna 'sisi' na wao. Kuna kujivuna kwa kutumia majina. Hali hiyo imepelekea uwepo wa mahitaji ya 'wao' ambao ni Watanganyika wanaotaka identity yao. Haiwezekani muungano ukabebwa na taifa moja.
wazungu wanasema 'it takes two to tangle'.

Umeeleweka mkuu kazi kwao na dhamira zao
 
Nguruvi3

Asante kwa kuweka record sawasawa!

Serikali mbili itaua Muungano, kama nia ni kuboresha Muungano, then tunapaswa kuwa na serikali 3 au 1

Nauona mwisho wa CCM katika siasa za Tanzania unakaribia...
 
Nguruvi3

Asante kwa kuweka record sawasawa!

Serikali mbili itaua Muungano, kama nia ni kuboresha Muungano, then tunapaswa kuwa na serikali 3 au 1

Nauona mwisho wa CCM katika siasa za Tanzania unakaribia...

Katu serikali moja haiwezi kuundwa kwa nchi zilizoungana ambazo nchi mojawapo imeshajitangazia kuwa na mamlaka kamili katiba yao kutamka bayana kuwa na malamlaka ya nchi rejea maoni ya Nguruvi3 hapo juu. Inachoweza kuongeleka kikaingia akilini mwangu kwa sasa ni uwepo wa:
  1. Serikali Kuu ya shirikisho
  2. Uhalalishwaji wa katiba mpya ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambayo imejipambanua kama nchi kamili
  3. Urejeshwaji wa taifa la Tanganyika ambalo lilimezwa na Tanzania na hivyo kuunda katiba yake ndani ya serikali ya shirikizo.
​
Hali halisi Watanganyika kwa sasa tumelazimishwa kudai serikali ya Tanganyika kutokana na shinikizo la serikali ya Zanzibar kujitwalia madaraka ya nchi kamili kwa kujitangazia uhuru ndani Muungano kinyume cha katiba mama ya Jamhuri ya Muungano.

Pengine ugeugeu wa wajumbe wa Zanzibar licha ya huko nyuma kudai serikali tatu, wamekuja kuona hatari ya kukatika ulaji waliokuwa wananufaika kwa mfumo tulio nao hasa nafasi za uongozi na uwakilishi bungeni. Viongozi wetu pengine tu ni kile kitu heshima tuliyozoea bila kuona halihalisi ya kinachoendelea ndani ya Muungano kwa kufumbia macho.
 
Candid Scope, kwa mantiki hiyo wajumbe wa Zanzibar wanataka kuunga mkono serikali mbili?!

Uwepo wa serikali mbili unaturudisha tulipotoka, hasa kama katiba ya Zanzibar haitafanyiwa mabadiliko.

Kwasasa sidhani kama kuidai Tanganyika kunaepukika, hasa kama Zanzibari hawataki kusurrender nchi yao kama Tanganyika tulivyofanya

Tumefikia sehemu ngumu sana kuweza kurudi kwenye serikali mbili!

Inamaana, baraza la wawakilishi likae kwasasa libadili katiba yao na Rais wao aipitishe kukubali kupunguza nguvu zake. Ni pagumu sana hapo kwasasa
 
Two wrong does not make a right. Kama Zanzibar kuwa nchi lilikuwa kosa, kuirudisha Tangayika hakutasahihi8sha kosa la Zanzibar kuwa nchi. Cha muhimu ni kuwa Zanzibar isiwe nchi na Tangayika iendelee kufa, i.e serikali moja ya Tanzania. Serikali moja or die.
 
Candid Scope, kwa mantiki hiyo wajumbe wa Zanzibar wanataka kuunga mkono serikali mbili?!

Uwepo wa serikali mbili unaturudisha tulipotoka, hasa kama katiba ya Zanzibar haitafanyiwa mabadiliko.

Kwasasa sidhani kama kuidai Tanganyika kunaepukika, hasa kama Zanzibari hawataki kusurrender nchi yao kama Tanganyika tulivyofanya

Tumefikia sehemu ngumu sana kuweza kurudi kwenye serikali mbili!

Inamaana, baraza la wawakilishi likae kwasasa libadili katiba yao na Rais wao aipitishe kukubali kupunguza nguvu zake. Ni pagumu sana hapo kwasasa
Mkuuu nakukubali umeeleza vizuri sana hoja ya kuitaka serikali ya tanganyika. Hivyo, ni swala la Zanzibar wenyewe kuchagua kusuka ama kunyoa maana wao ndio wamenzisha vagi hili kwa kuunda yao katiba mpya kwa kupuuza katiba ya Jamhuri.

Aidha wakubali kurudi ktk katiba ilozaa muungano wetu, zile kero wanazodai kila siku zitazamwe na kutolewa maelezo maana nimewasikia sana Wazanzibar wakilalamikia bara hata katika maswala yasokuwa ya muungano. Wafanye referendum, ukweli uwekwe bayana maana dunia ya leo hii ni muhimu sana UWAJIBIKAJI na UWAZi kwa viongozi wetu. Ubabaishaji na usanii ndio umetufikisha hapa tulipo maana sioni sababu kabisa ya malumbano baina yetu kuhusu serikali ngapi zinahitajika bali ni muungano gani tulofunga na kula yamini. Huu sio mkataba wala makubaliano bali ni udugu wa damu usovunjika kwa utashi wa mtu ama kundi la watu.
 
Mkuu Mkandara umeliongelea vizuri sana hili suala la serikali ngapi!

Kwamba tuna undugu wa damu na Wazanzibari, ambapo kuuvunja Muungano sio hoja kwa wajumbe takribani wote. Ila wanatafuta muundo mzuri wa serikali. Serikali mbili haiwezekan kwasasa kutokana na uwepo wa Katiba ya Zanzibar inayozuia kuwepo kwa serikali mbili.

Kutokana na hoja zetu, Jibu la Muungano wetu ni Serikali tatu kwavile serikali moja inashindikana kabisa, na serikali mbili ni mchezo wa kuigiza
 
Back
Top Bottom