Chaguzi za vyuo vikuu ni CHADEMA dhidi ya CCM

Dawa ya magamba ni kuwabana kila kona!! Tunaandaa wabunge na madiwani!!:horn:
 

Mkuu umeua! Isipokuwa majambazi wakichaguana nani aingie ndani kupora na nani abaki nje kulinda "usalama" huo tuwaachie CCM.


Hapa naona jambazi mmoja atatoa rushwa kwa mwenzie ili aingie ndani kupora na baadaye amzike mwenzie
 
Kamanda Mouddy,nimekupata vilivyo!iliyobaki ni kuhakikisha mtandao imara wa CDM kwenye vyuo maana magamba wamebaki kurithishana inatakiwa ifike mahali kila wanapogusa kijana wakute ni CDM.Dogo sijakuona kijiweni posta Moshi siku nyingi ni mpambano wa academics?Pambana mzee.Kama wanagawana kila kitu lazima tutoke kwa kupambana,mwisho wao unakuja soon!
 

Hapo SMUCCO nina wasiwasi maana jamaa wa Mwaka jana aliwasaliti wanafunzi wenzake mwaka jana aliwasaliti wenzake walipo dai haki. Hili lilipelekea wanafunzi kusimamishwa mwaka. Mimi shuhuda maana nilikuwa Kibosho wakati wa tukio.
 
Big up sana, siku zote vijana ndi nguzo kuu ya mabadiliko, tuendelee kuikataa ccm na mambo yake yote kila kona.
 
Pia mwaka jana pale CBE DOM rais alikua ni mchadema damu damu. Na mwaka huu bila shaka nimchadema yupo ikulu.
 
Siasa zinaanzia chuo kikuu, hata wanasiasa wengi wameibukia chuo kikuu. Fuatilia historia. Kwa mfano Makerere na Mwalimu.
 
sio vyuoni na mashuleni tu mwana hata huku msikitini sasa tunabadilika hadi raha tukitoka magharibi kama shekh kaiponda cdm tunaanzisha muhadhara mwingine nje wa kueleza mazuri ya cdm.
ghorofa ninayofanyakazi ina wafanyakazi zaidi ya 200 lakini naapa niliewai kumuona anaiponda cdm ni mmoja tu anaitwa asuu ambaye ni mlinzi wa getini . na baada yakuchunguza kwamakini nikagundua kuwa ni mgambo kwahiyo dili za kulinda mitihani ya wanafunzi na masherehe sherehe ata zikosa akijiunga na cdm, lakini sasa naapa tena nimempa darasa ameelewa amechukua kadi na sasa ni mwanachama jasiri namuongeaji mkubwa wa kuikubali cdm sasa nakaa kwaraha sana nikitazama kulia vidole viwili juu kushoto viwili juu, nyuma mbele mameneja wenzangu wafanyakazi wa kati mpaka walinzi wa getini chadema mwanzo mwisho
pipoooooooooz
 
Kamanda siyo vyuo tu nimeshudia chaguzi za shule za seondari na msingi zikiendeshwa kwa misingi ya uchadema na uccm na ccm wamekuwa wagigalagazwa viluvyo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…