ligendayika
JF-Expert Member
- Aug 31, 2012
- 1,183
- 198
Nimekua nitembelea shule za msingiWilaya ya Songea vijijini na kugundua kuwa shule zote zonazotoa chkula cha mchana zina mahudhurio mazuri ya wanafunzi na pia wanafunzi wake wanautayari mkubwa wa masomo hasa shule za kata za madaba na wino. Hata hivyo kata hizo pia zina wazazi ambao wana mwamko mkubwa juu ya elimu hivyo kuchangia chakula na michango mingine ya shule ni jambo la kawaida kwao. Swala kama hilo halipo katika kata nyingine hasa muhukuru ambako wananchi hawana mwamko wa elimu hivyo kutoona umuhimu wa kuchangia maswala ya elimu na utoro wa wanafunzi maeneo hayo ni mkubwa na ufauru wa kata hiyo ni wa chini. Naiomba serikari ilione hili na kuamua kuweka sheria ya wazazi kichangia chakula cha wanafunzi wa shule za msingi.