Mzee wangu nimemtoa Regency a month ago alilazwa kisa sukari. It was a big blast haijawahi kutokea. Awali aliigundua miaka 5 iliyopita, akapata mitishamba ikapona. Maana alipima ikaonekana hakuna, 3 months consecutively. Akawa kajiachia anakula apendavyo. Ilivyorudi mwaka jana Nov mwishoni ndio hatari. Ilifika 21 mtu hajiwezi. Alivyofika nikamkimbiza kwa Wahindi pale.
Siku hizi sukari yake ina range 7 hata 8 haifiki. Wakati mwingine hata insulin hajichomi japo zipo nyingi tu. Na hata siku 2 zinapita hajapima sukari na wala hatetereki.
Asubuhi uji, sometimes maandazi (yasio na mafuta sana) au scones, maharage, au supu ya kuku/samaki.
Mchana dona samaki/kuku, majani mboga au dagaa na matunda anakula.
Jioni ndizi, au dona tena au chochote kisicho sukari na wanga mwingi.
Kiasi fulani ni usumbufu kuandaa chakula cha mgonjwa sukari.
Nakomaa naye kwanza kisha atarudi kwake.
Sent using
Jamii Forums mobile app