Chalamila: Rais Nyusi atapata kiwanja Dar na tutamsimamia wakati wa ujenzi

Chalamila: Rais Nyusi atapata kiwanja Dar na tutamsimamia wakati wa ujenzi

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Chalamila ameyasema hayo katika ufunguzi wa maonesho ya biashara Dar Saba Saba ambako Rais Nyusi wa Msumbiji alikuwa mgeni rasmi;

"Sisi wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam kama ambavyo tunayo hamu wewe kuendelea kuwa mkazi wa Dar es Salaam, usiende tena kuishi mkoa mwingine. Nitumie nafasi hii tena kumkaribisha kwa dhati Mh. Rais Nyusi na tunamuhakikishia kwamba Dar es Salaam ni mji salama na atapata kiwanja hapa Dar es Salaam, na tutamsimamia wakati wa ujenzi.

"Lakini pia nimeambiwa kule Zanzibar kama anahitaji kuwa na eneo la kujenga kiwanda atapata ule mkoa wa Kusini katika wilaya ya Kati katika kijiji cha Dungu ambako limeandaliwa eneo kubwa sana kwaajili ya masuala ya uwekezaji. Kwahiyo Mh. Nyusi tunakukaribisha sana, wala usiogope, Tanzania ni ya kwako."


Wakuu, kwani Rais wa nchi nyingine anaweza kupewa zawadi ya kiwanja kama hivi tena na Mkuu wa Mkoa?

 
Mkoa wa "kusini" ndiyo mkoa Gani hapa Tanzania?

Au anamaanisha kusini magharibi, Zanzibar?
 
"Lakini pia nimeambiwa kule Zanzibar kama anahitaji kuwa na eneo la kujenga kiwanda atapata ule mkoa wa kusini katika wilaya ya kati katika kijiji cha Dungu ambako limeandaliwa eneo kubwa sana kwaajili ya masuala ya uwekezaji".

Team mama mlimkosoa sana Jiwe kuendelea kwao,ila nyie mnarudia yaleyale ya jiwe Kila kitu kupeleka kwao.

Tena inasemekana watu wa "kamera" wamepigwa mkwara mzito kuchukua chukua picha na kusambaza "umbea". Hatutaki mambo ya mwenda zake Kila mtu ajue kwamba Dunia nzima ilikuwa anakujenga chato.
 
Huyo raisi anaongea kiswahili cha kibongo, alikijulia wapi?
Amesoma primary na secondari Nachingwea na bagamoyo Kaole pake ..kwenye makambi wapigania uhuru....anajua mambo mengi ya Tanzania walirudi kwao miaka kati kati 1975 huko....akija kijana mdogo .....anajua kiswahili choote....hata Mnangagwa wa Zim.....
 
Back
Top Bottom