Chama cha skauti Tanzania na historia ya utumwa

Chama cha skauti Tanzania na historia ya utumwa

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
1697425421115.png
BARUA YA CHAMA CHA SKAUTI TANZANIA MKOA WA DAR ES SALAAM NA HISTORIA YA UTUMWA

Barua hiyo hapo chini inajieleza inakotoka na kichwa cha habari ndiyo hicho.

Wanafunzi watakuwa na safari ya kutembelea magofu ya kale Kunduchi na kujifunza historia ya utumwa na historia ya Waarabu waliotawala Pwani ya Kunduchi.

Si tabu kuelewa watakachoelezwa vijana wetu kwani historia hii ni maarufu hakuna asiyeijua.

Ushauri wangu ni kuwa katika ratiba hiyo yao waongeza na kulizuru kaburi la Mzee Mshume Kiyate ambae kazikwa Kunduchi kwenye makaburi ya kale.

Wawaonyeshe vijana wetu kaburi la Mzee Mshume Kiyate na waeleze historia yake na mchango wake katika kupigania uhuru wa Tanganyika akiwa bega kwa bega na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere hadi uhuru kupatikana mwaka wa 1961.

Naamini historia hii ni muhimu katika kujenga uzalendo kwa hawa vijana wetu wadogo kuliko propaganda za Waarabu na Utumwa.

Historia ya Waarabu na Utumwa inafahamika.
Historia isiyofahamika ni hii ya Mzee Kiyate Mshume.

1697425277173.png

1697425322588.png

1697425353012.png


1697425420716.png

1697425458094.png
 
Shikamoo mzee.

Ni kwanini utumwa umeutaja kama propaganda?
 
Shikamoo mzee.

Ni kwanini utumwa umeutaja kama propaganda?
Kwa sababu wale waliokua wakiwabebesha pembe za Ndovu na kuwauza Babu zako na Bibi zako wazaa Bibi na Babu hawakua waarabu bali ni story za kutunga za wazungu ili kuwakosanisha na waarabu,
 
Shikamoo mzee.

Ni kwanini utumwa umeutaja kama propaganda?
Cast...
Maharaba.
Siku zote historia ya Tanzania imekuwa ikiandikwa kwa kutiwa propaganda.
Unajua maana ya propaganda?:

information, especially of a biased or misleading nature, used to promote a political cause or point of view.
"he was charged with distributing enemy propaganda"
 
Kwa sababu wale waliokua wakiwabebesha pembe za Ndovu na kuwauza Babu zako na Bibi zako wazaa Bibi na Babu hawakua waarabu bali ni story za kutunga za wazungu ili kuwakosanisha na waarabu,

[emoji28][emoji28][emoji28],walikua wachina? Utamtetea uwezavyo ila historia ya utumwa barani afrika haiwezi kamilika bila uwepo wa dalali mkuu waarabu.
 
Kwa sababu wale waliokua wakiwabebesha pembe za Ndovu na kuwauza Babu zako na Bibi zako wazaa Bibi na Babu hawakua waarabu bali ni story za kutunga za wazungu ili kuwakosanisha na waarabu,
Lakini unajua kua hakuna sehemu wazungu wakajisema wao ni wasafi kwenye hiyo biashara?

Kuna waarabu walishiriki na kuna waliopinga kuna wazungu walishiriki na kuna waliopinga
 
Lakini unajua kua hakuna sehemu wazungu wakajisema wao ni wasafi kwenye hiyo biashara?

Kuna waarabu walishiriki na kuna waliopinga kuna wazungu walishiriki na kuna waliopinga
Hapana sisi waislamu wa kisiwani huku kisiwa ndui na chakechake ambi nakwambia mwarabu hakuwahi kutuuza ni story tu uzushi wa wazungu yakhee
 
Cast...
Maharaba.
Siku zote historia ya Tanzania imekuwa ikiandikwa kwa kutiwa propaganda.
Unajua maana ya propaganda?:

information, especially of a biased or misleading nature, used to promote a political cause or point of view.
"he was charged with distributing enemy propaganda"
Mzee wetu unamaanisha soko la watumwa Zanzibar halikuwepo ni habari za kutungwa na wazungu
 
Mzee Mud Said wewe ni kafiri tu mbele ya waarabu wote haijalishi wa hapa Tanganyika au popote as long wewe ni mbantu ni kafiri tu, na hata ujipendekeze vipi kwao wewe ni kafiri tu. Ukweli mchungu
 
Mzee wetu unamaanisha soko la watumwa Zanzibar halikuwepo ni habari za kutungwa na wazungu
T14,
Soko la Watumwa lilikuwapo Zanzibar na lilikuwapo Mikindani na hili la Mikindani nimeliona kwa macho yangu ni soko ambalo David Livingstone alilishuhudia.

Lakini hebu soma hapo chini:

''Key facts about the transatlantic slave trade Between 1662 and 1807 British and British colonial ships purchased an estimated 3,415,500 Africans. Of this number, 2,964,800 survived the 'middle passage' and were sold into slavery in the Americas.''
 
T14,
Soko la Watumwa lilikuwapo Zanzibar na lilikuwapo Mikindani na hili la Mikindani nimeliona kwa macho yangu ni soko ambalo David Livingstone alilishuhudia.

Lakini hebu soma hapo chini:

''Key facts about the transatlantic slave trade Between 1662 and 1807 British and British colonial ships purchased an estimated 3,415,500 Africans. Of this number, 2,964,800 survived the 'middle passage' and were sold into slavery in the Americas.''
Kwahiyo mkuu hilo soko la watumwa Zanzibar lilijengwa na Waingereza, wamiliki na wachuuzi wa watumwa soko hilo ni Waingereza na wanunuaji ni Waingereza vilevile.
 
Tuacheni mahaba ya kipumbavu. Mbele ya hao watu weupe sisi ni vikatuni. Kuwa kwenye dini zao zisitufanye tukawa mataahira. Waarabu na wazungu wote wameshiriki jinai ya utumwa kikamilifu wakishirikiana na watawala na wafanyabiashara washenzi wa kiafrika zama hizo. Huku kwetu kabila lililoshiriki kuuza waafrika wenzao ni wanyamwezi.
 
Tuacheni mahaba ya kipumbavu. Mbele ya hao watu weupe sisi ni vikatuni. Kuwa kwenye dini zao zisitufanye tukawa mataahira. Waarabu na wazungu wote wameshiriki jinai ya utumwa kikamilifu wakishirikiana na watawala na wafanyabiashara washenzi wa kiafrika zama hizo. Huku kwetu kabila lililoshiriki kuuza waafrika wenzao ni wanyamwezi.
Anawanyenyekea sana waarabu yeye anaona waarabu walitufanyia mambo mema
Wakati hao waarabu,wazungu wahindi
Wachina wote wanatuburuza

Ova
 
T14,
Soko la Watumwa lilikuwapo Zanzibar na lilikuwapo Mikindani na hili la Mikindani nimeliona kwa macho yangu ni soko ambalo David Livingstone alilishuhudia.

Lakini hebu soma hapo chini:

''Key facts about the transatlantic slave trade Between 1662 and 1807 British and British colonial ships purchased an estimated 3,415,500 Africans. Of this number, 2,964,800 survived the 'middle passage' and were sold into slavery in the Americas.''
Unawanyenyekea sana waarabu naona

Ova
 
Back
Top Bottom