bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Chama cha Soka Afrika (CaF) inabidi waliangalie hili kwa jicho la pili na kulifanyia mabadiliko kama wanataka kwenda na Sayansi ya Mpira.
Hapa nazungumzia haya mashindano mawili kombe la Mabingwa Afrika na Kombe la shirikisho Afrika kwa kifupi hii michuano imepoteza mvuto tofauti na kipindi cha Nyuma au kulinganisha na Michuano ya Mabara Mengine ngazi ya vilabu.
La Kwanza CAF inabidi wajitangaze sana na kutafuta udhamini mnono zaidi ili ligi hizi ziwe na mvuto tena na bahati nzuri siku hizi kuna chombo kimoja cha habari kinaonyesha hii michuano Mubashara tofauti na Supersport lakini huezi kuta wakifuatilia mfano bingwa wa Kombe la Mabingwa mwaka huu Wydad Athletic Club ya Morroco baada ya kumfunga Al ahly ya Egypt wengi wetu tu hatuijui na hata humu JF Sikuona habari zozote kuhusu michezo hii Siku ya fainali hii inaonesha ni jinsi gani Caf hawatoi matangazo ya kutosha.Pia kutakua na mchezo wa Fainali kati ya Tp Mazembe na Supersports ya Afrika kusini ila mpaka sasa hakuna matangazo yoyote kuitangaza fainali hizi,hapa inabidi Caf kitengo cha Masoko na habari wajitangaze sana.
Na pili ligi fainali ya ligi hizi imekua ikichezwa kwa mfumo wa ugenini na nyumbani hili nalo naona halijakaa vizuri Caf wangetafuta Kiwanja kimoja either hata uwanja wa Taifa hapa Bongo or Kasarani pale Kenya na Kwingineko na Fainali kupigwa moja tu,hili litaongoa zile dhana kuwa timu ikiwa nyumbani inabebwa na kushuhudiwa na watu tofauti na kufanya watu wengi zaidi kuifuatilia.
Kazi kwenu Caf.
Hapa nazungumzia haya mashindano mawili kombe la Mabingwa Afrika na Kombe la shirikisho Afrika kwa kifupi hii michuano imepoteza mvuto tofauti na kipindi cha Nyuma au kulinganisha na Michuano ya Mabara Mengine ngazi ya vilabu.
La Kwanza CAF inabidi wajitangaze sana na kutafuta udhamini mnono zaidi ili ligi hizi ziwe na mvuto tena na bahati nzuri siku hizi kuna chombo kimoja cha habari kinaonyesha hii michuano Mubashara tofauti na Supersport lakini huezi kuta wakifuatilia mfano bingwa wa Kombe la Mabingwa mwaka huu Wydad Athletic Club ya Morroco baada ya kumfunga Al ahly ya Egypt wengi wetu tu hatuijui na hata humu JF Sikuona habari zozote kuhusu michezo hii Siku ya fainali hii inaonesha ni jinsi gani Caf hawatoi matangazo ya kutosha.Pia kutakua na mchezo wa Fainali kati ya Tp Mazembe na Supersports ya Afrika kusini ila mpaka sasa hakuna matangazo yoyote kuitangaza fainali hizi,hapa inabidi Caf kitengo cha Masoko na habari wajitangaze sana.
Na pili ligi fainali ya ligi hizi imekua ikichezwa kwa mfumo wa ugenini na nyumbani hili nalo naona halijakaa vizuri Caf wangetafuta Kiwanja kimoja either hata uwanja wa Taifa hapa Bongo or Kasarani pale Kenya na Kwingineko na Fainali kupigwa moja tu,hili litaongoa zile dhana kuwa timu ikiwa nyumbani inabebwa na kushuhudiwa na watu tofauti na kufanya watu wengi zaidi kuifuatilia.
Kazi kwenu Caf.