Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Chama kikubwa cha umoja wa wafanyakazi wa sekta ya uzalishaji magari, ndege na mashine za mashambani wamewafungulia mashitaka Donald Trump na Elon Musk wakilalamika mazungumzo yao ya jana Twitter yalihusisha kauli za kudhalilisha, kutishia na kudhoofisha wafanyakazi wanaogoma kushinikiza waajiri wao katika masuala mbalimbali yanayouhusu haki na maslahi ya wafanyakazi.
Katika sehemu ya mazungumzo hayo marefu Trump alimsifia Elon Musk jinsi ambavyo hufukuza wafanyakazi wa kampuni anazoziongoza pale ambapo huwa wanagoma kushinikiza mambo kadhaa.
Nchini Marekani inachukuliwa ni kinyume cha sheria kuwaadhibu wafanyakazi kwa sababu wamegoma au wameandamana kushinikiza maslahi yao.
Katika sehemu ya mazungumzo hayo marefu Trump alimsifia Elon Musk jinsi ambavyo hufukuza wafanyakazi wa kampuni anazoziongoza pale ambapo huwa wanagoma kushinikiza mambo kadhaa.
Nchini Marekani inachukuliwa ni kinyume cha sheria kuwaadhibu wafanyakazi kwa sababu wamegoma au wameandamana kushinikiza maslahi yao.