Mtanzania umesema kweli na ninaamini kuna mambo machache ambayo mwandishi asiyachukulie at face value au kuyakubali tu. Kwa mfano Rais aliposema "watu hawali mapanki" au pale aliposema "BAE ni kampuni ya Serikali ya Uingereza" waandishi hawana budi kuangalia kauli hizo na kuhakikisha ukweli wake. Mtu anaposema fulani ni mwanachama wa chama fulani ni bora uhakikishe anachosema ni sahihi. Nakubaliana na wewe 100% kwamba ni jukumu la wale wanaoandika habari au maoni to be as accurate as humanly possible especially ambapo ni rahisi kuverify certain information.
Nina tatizo hata hivyo na mahitimisho yako kadhaa.
Kudai kuwa habari nzima ni uongo mtupu nafikiri ni exaggeration of the first order. Nadhani umeweza kuonesha ni yapi ambayo factually are just simply wrong. Hayo yanayohusiana na facts ni rahisi kuyaweka sawa. Kama hili:
Nadhani hapa itakuwa ni maneno yako against maneno yao; kwanini tuamini kuwa vita hivyo havipo? aidha kwa sababu havipo au kwa vile umesema havipo?
Hapa inabidi watu waamini "sources" zako ambazo ni unnamed na hatujui zina maslahi gani katika pande zinazohusika. How balanced are you sources? Maana hilo gazeti na wenyewe wanasema wana "sources" zao hapo hapo Mbeya. Kwanini sources zako ziaminike zaidi ya sources zao?
Hili nadhani ni kweli kabisa; lakini it is the nature of the beast. Siasa ni moves, counter moves na moves na anti-moves! Jinsi gani waandishi wanashikiri katika michezo hii ya kisiasa? Nadhani ni sehemu yenyewe ya siasa. Kuna uhusiano wa ajabu sana kati ya vyombo vya habari na wanasiasa siyo Tanzania tu bali dunia nzima.
Wenzako wanasema kipo, wewe unasema hakipo. Mmoja wenu hayuko sahihi. Ni nani? time only will tell. Umesema Prof. hana mpango wa kugombea you might be very right, lakini ukweli wa kauli hiyo utaonekana 2010, kabla ya hapo ni jambo la probability tu. Sasa akigombea 2010 unaweza ukasema in 2008 hakuwa na mpango huo..
Of course, siasa ndivyo ilivyo. Labda kuna mambo hayapaswi kuwa hivyo (in a perfect world where personal interests are not at play) lakini katika ulimwengu ambao maslahi, matamanio, chuki, hasira, kinyongo, ushabiki, mapenzi nk vipo, utakutana na watu wa namna hiyo.
Don't be too harsh.
Mwanakijiji,
Nafikiri unajua garbage IN garbage OUT, ukijenga nyumba kwa foundation mbovu, nyumba nzima inakuwa mbovu. Hiyo makala imejengwa kwa foundation mbovu sana. Ukweli ulioko kwenye hiyo makala ni ule ambao tayari tunaujua na hakuna jipya hapo zaidi ya uzushi.
Kwanza hilo la kwamba Dr. Mwakyembe ni mjumbe wa NEC sio kweli.
Pili, nguvu ya Mwandosya kule Mbeya ni kubwa mno kiasi kwamba huyo Mwenyekiti hawezi hata siku moja kuandaa kwenye mkutano ajenda ya kumjadili prof. kwa kutumia vigezo vya mitaani. Huyo Mulla hana ubavu huo kabisa. Wanaweza kumjadili Prof. Kama kuna jambo kweli amelifanya lakini sio kwa
kutumia haya maneno ya mitaani. Kwa yeyote anayeijua Mbeya vizuri anajua hilo.
Tatu, prof. Mwandosya sio mjinga, ni mtu mwenye ueleo na ambaye anajua siasa za CCM na kikomo chake. Kama CCM waliweza kumtupa Malecela bila sababu za msingi, yeye prof. atakuwa na uwezo gani wa kupambana na rais aliyeko madarakani? Labda mwandishi angesema Prof. anataka kuhama chama lakini sio ndani ya CCM. Prof. kufanya hivyo itakuwa ni kujimaliza kisiasa
na sidhani kama yuko tayari kwa hilo.
Nne, toka uchaguzi wa NEC umeisha, prof. Mwandosya amekuwa kimya na kuweka nguvu yake kwenye uongozi wa nchi na sio siasa za ugomvi za Mbeya. Sijasikia hata mahali popote wakiandika Mwandosya anatembelea mkoa huu au wilaya hii. Sasa ataanza kampeni ofisi kwake au nyumbani kwake?
Ushauri wa bure ni kwa Wabunge kuacha kulialia na kuweka nguvu zote kwenye ku deliver kwenye majimbo yao. Magazeti yanaweza kukujenga lakini pia yanaweza kukubomoa.
Huyo Lowassa wanayemsema, kama ana nguvu si angejiokoa yeye asivuliwe kuwa PM?