SoC01 Changamoto: Malezi ya Watoto/Mtoto yatima

SoC01 Changamoto: Malezi ya Watoto/Mtoto yatima

Stories of Change - 2021 Competition

flulanga

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2016
Posts
4,860
Reaction score
6,390
Yatima kwa tafsiri ni mtoto aliyefiwa na wazazi wote wawili yaani baba na mama muda huo huo umri wake ukawa chini ya miaka 18.

Habari ndugu zangu, uzi wangu utaelezea hadha wapitiazo watoto yatima kimalezi na makuzi au watoto waliotelekezwa na wazazi wao (sio wote wanapitia ila naamini ni wengi).

Kama wewe ni kati ya watu waliopewa/kuachiwa jukumu la kulea mtoto/watoto wa ndugu yako basi unaweza kujifunza kitu hapa.

Twende pamoja sasa;

Mimi nikijana kwa majina naitwa Henerico. Ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto watatu. Mama yangu alijaaliwa kuzaa mara mbili yaaani mimi ndio wakwanza na wadogo zangu wawili wanaonifuata ni mapacha yaaani Kulwa na Doto wote hawa ni wanaume.

Kwa upande wangu mimi kama mtoto wa kwanza kwa mama yangu baba yangu aliikataa mimba yangu kwa mujibu wa maelezo ambayo nayasikia toka nikiwa mtoto. Wadogo zangu pia wenyewe wana baba yao ila hawajaishi nae alipozaa tu na mama yangu baba yao aliondoka na hakujulikana kaenda wapi kwa hiyo wote tukabaki na malezi ya upande wa mama.

Kwa bahati mbaya me nikiwa na umri wa miaka 6 na wadogo zangu wakiwa na miaka 3 mama yangu alifariki dunia. Kwa wakati huo sikuona kama kuna shida au sikuhisi kama uyatima umeingia bali niliona ni kitu cha kawaida nadhani ni kutokana na umri wangu ulikuwa bado mdogo ila kumbukumbu kichwani kwangu bado ninazo mpaka msiba ulivyoendeshwa. Msiba ulipita na maisha mengine yakaendelea tukiwa tunaishi na bibi yetu na mama zetu wadogo na wakubwa.

Mwaka mmoja baada ya msiba niliweza kupelekwa shule darasa la kwanza, bibi yangu na mama zangu wakubwa ndio walikuwa wahusika wakubwa.

Mpaka naanza shule nilikuwa bado sijaona pengo la mama. Nilipofika darasa la tatu ndio nilitambua pengo la mama lipo wapi.

Nilikuwa nafanya mafundisho ili nibatizwe na mafundisho niliyafanya kwa muda wa miaka mitatu toka nikiwa darasa la kwanza mpaka nilipofika darasa la tatu ndio nilikuwa nahitajika nibatizwe. Kwa bahati mbaya nilikuwa sijalipa hela ya zaka mpaka ile siku ambayo usiku wake ndio nilikuwa nahitajika nibatizwe mpaka kufikia saa 10 jioni bado sijapata hela ya zaka, mda huo katekista ananiambia 'ujalipa hela ya zaka uwezi kubatizwa', nikifikiria mafundisho nimefanya kwa muda wa miaka mitatu halafu leo hii nisibatizwe aiseee NILILIA.... Bibi yangu angekuwa na hela angenipatia ila wakati huo na yeye alikuwa hana pesa. Nikienda kwa mama zangu wakubwa wanatupiana mpira ukienda kwa huyu anakwambia nenda kwa yuleeee... NILIMWAGA CHOZI na ndiyo siku hiyo nilipoanza maombolezo ya mama yangu.

Ilipofika jioni mama yangu mkubwa alipojihakikishia nimekosa kwa ndugu wote ndipo aliponipatia pesa (7,500) nikaenda chapu kulipia nikarudi nyumbani kujiandaa kwenda ibadani kubatizwa. Ila hapo macho yamenivimba kwa kulia na kiukweli nisingebatizwa ile siku nilikuwa najiandalia safari niende ovyo nikawe mtoto wa mtaani.

Usiku wa ubatizo ulipofika nilikutana na msimamizi wangu wa ubatizo nikiwa nimevaaa yale majaketi makubwa ili kuficha shati langu la ndani, lilikuwa limechanika, yeye hakutambua lile koti kubwa vile nimelivaa la nini, Akaniamuru nilivue, nilipolivua ndipo alipogundua kuwa nimelivaa koti kwasababu gani Ikabidi awe mpole akaniambia basi nilivae tu!! Ibada ya ubatizo ilienda vizuri. Tukarudi nyumbani kuendelea na maisha.

Ile usiku wa ubatizo hadi leo naikumbuka jinsi wenzangu walivyokuwa wamependeza, wanapiga picha na kuvishwa mataji na ndugu zao. Huwa nacheka sana na kuuona Ukuu wa Mungu maana kwa wakati huo wala sikuwa na akili ya kuwaza au akili ya kutamani wenzangu walivyopendeza, akili yangu yote iliwaza nibatizwe.

Baada ya ile siku ya ubatizo ndipo nilipoanza kutambua thamani ya mama. Toka siku hiyo nilianza kuwa namlilia mama yangu, sikuwa naamani tena moyoni mwangu, maisha ya upweke ndipo yalipoanzia hapo. Nilianza kujiona ni mtoto mwenye mapungufu makubwa sana tofauti na watoto wenzangu.

Nilimaliza darasa la saba kiugumu sana maana shule nilianza kuichukia sana.

Kabla sijamaliza shule alikuja mtoto wa mama yangu mkubwa tukaungana nae darasa moja alitokea kijijini, tukawa tunaishi kwa bibi na watoto wengine wa mama zangu wakubwa pamoja na wadogo zangu. Ila kiukweli maisha hayakuwa mazuri sana wala mabaya sana. Tukafaulu shule moja mimi na huyo ndugu yangu yaaani kidato cha kwanza.

Ulipofika muda wakufanya maandalizi ya kwenda shule ndipo ilikuwa kimbembe sasa. Mama yangu mkubwa anashindwa kumpeleka mtoto wake shule kwasababu yangu mie, jamii itamuonaje ampeleke mtoto wake shule halafu mimi nibaki kitaaa!! Mama yangu mkubwa alipitia kipindi kigumu sanaa nilitamani nimwambie ampeleke tu kwanza mwenzangu ambae ni mtoto wake mimi nisiwe sababu ya mwenzangu kutokwenda shule ila nikabaki na mgogoro na nafsi yangu nikawa najiona na hatia yaani sikupenda niwe chanzo cha mwenzangu asiende shule. Ila nashukuru Mungu mwisho wa siku walijipiga piga na wote tukaenda shule. Wabarikiwe kwa hilo. Japo nilisoma huku najiona kabisa ni mzigo kwa ndugu zangu.

Maisha yalisonga na masomo yalisonga ila changamoto zilikuwa zipo nyingi sanaaa. Mtoto wa mama yangu mkubwa alikuwa hapendi shule, alikuwa anaenda shule kutimiza wajibu tu. Kwahiyo nilipokuwa nahitaji kusoma twisheni ilibidi niwe namtumia huyu mwenzangu kwa kumbembeleza amwambie mama yake ambaye ni mama mkubwa kuwa tunataka tusome twisheni atulipie ikawa ndio maisha yangu ya uchawa kwa ndugu yangu ili maisha yaende. Ila mwisho wa siku alinigomea kuwa chawa wake. Ikabidi twisheni iishie hapo ila bado nikawa nikiwa na shida ya mahitaji ya shule nilikuwa nasubiria mpaka mwenzangu nae apate shida kama yangu yaaani nikawa naishi kwa kusafiria nyota. Nilikuwa sipendi kuonekana mimi ndio na mahitaji mengi kuliko mtoto wake.

Wadogo zangu muda huo nasoma na wenyewe pia walikuwa wanasoma ila kwa bahati mbaya wadogo zangu walikuwa watukutu sana toka wakiwa wadogo, walikuwa hawapendwi kutokana na tabia zao. Kuna siku nilimsikia mama yangu mkubwa anawaambia 'kamtafuteni baba yenu' niliumia sana..., niliingia ndani nililia sana nikafikiria baba yao hata hawamjui inakuwaje wanatamkiwa kauli kama ile? Nilikosa majibu zaidi niliishia kulia tu!! Ila hakuna aliyejua kama nililia.

Nilimaliza shule vizuri. Na kwa bahati mbaya matokeo yalipotoka hayakuwa mazuri. Na moja kwa moja niliyaanza maisha rasmi maana pale nyumbani nilipachukia kwa hiyo nilihitaji kuwa na maisha yangu.

Katika malezi niliyolelewa kwa kiasi fulani ndio matokeo ya maisha yangu ya sasa Kama vile;
  • kutojiamini,
  • hasira na chuki,
  • kutokufanya vizurii katika masomo,
  • kuathirika kisaikolojia,
  • Kuathiri mwenendo mzima wa maisha ya baadae hasa kifamilia.

Walezi/wazazi fanyeni hivi ili kupunguza watoto wa mitaani;

- Walezi/wazazi tunapoamua kulea watoto/mtoto ambae sio wako tujitahidi kuweka usawa na hata kama msipoweka usawa basi mjitahidi msioneshe moja kwa moja. Hii hali iliniathiri kwa kiasi fulani nakupelekea kuichukia shule.

- Wazazi/walezi tuchungeni kauli zetu sio vizurii kuwaropokea watoto kauli tata ambazo zitampelekea mtoto maumivu na kutamani kujitenga na nyumbani. Hali hii ilipelekea mdogo wangu kuhasi nyumbani na kuwa mtoto mitaani.

- Wazazi tujitahidi kuwafundisha watoto wetu ili upendo, pindi wachanganikapo na watoto wengine ambao wazazi wao hawapo basi waweze kuishi nao bila ubinafsi. Hii ilinitokea mimi, ilifikia hatua mtoto wa mama yangu mkubwa ananiambia 'usitumie kitu fulani kwani kanunua mama yako?' Hali hii inaweza pelekea mtoto kujizira nakupelekea hata kujizuru au kwenda mitaani.

- Walezi tujitahidi kuwa na moyo wa kutoa mahitaji kwa watoto yatima, kutimiza ndoto zao. Tukifanya hivyo mtoto atajihisi na thamani wala hawezi kuwaza yeye ni yatima, hawezi kutamani maisha ya kwenda kuishi mitaani. Mfano mimi nilipokosa hela ya kutoa zaka kanisani nibatizwe, nilijisemea katika moyo wangu 'nisipobatizwa basi bora niende ovyoo'.

HITIMISHO; Wazazi tuombe sana MUNGU atujaalie uhai mrefu na tujiepushe na visababishi ambavyo vitapelekea kufupisha uhai wetu au kupunguza umri wetu wa kuishi duniani ili tulee watoto wetu.
Uyatima sio mzuri, mwanao unavyomlea usifikirie na mwingine atamlea hivyo, atamvumilia kama vile wewe unavyomvumilia hapana sio rahisi hasa kwenye hizi familia zetu za kipato cha chini.

Tuishi kwa maangalizo pindi pale tunapopata nafasi basi tujitahidi kuwekeza kwa watoto wetu upendo, elimu, na rasilimali ambazo zinaweza kuja kuwafaa badae endapo kama kifo kitabisha hodi.

MWISHO.

WENU MTIIFU HENERICO.
 
Upvote 7
hicho cha Mtoto mie niliishi na chawa pamoja na utititri kuku, nikiwa na shangazi yangu!!! na jiulize nyumba ya nani??? ya Baba yangu mzazi!!.. .Mama hakupenda tuishi ivo na alikuja kutuchukua kwa nguvu tukaenda mjinii...

Ajili ya kujimwambafy Baba akachukia kwa kile kitendo!! kuwa amedharauliwa ..alicho kifanya Baba baaada ya week moja ya kuishi nae mjini akaturudisha kijijini kwa lazimaaa!......kufika kule tukaishi na maisha yakawa magumu mara dufu!!

Kuanzia kula, kulala na uniform za shule Mtoto wa kike lkn sare matakoni imechanika hana hata chupi ulikuwa ni udhalili wa hali ya juu sana! kwa hali km ile ya kuchekwa ilibidi tujitenge na wengine!! tukajifunza kushona viraka kwa lazima kwa msaada wa jirani!.....

kadri hali ilivokuwa mbaya tukajifunza kufanya vibarua na biashara kwa siri kubwa km hivi tukiagizwa majembe shuleni sisi tulikuwa haturudi nayo nyumbani!! tunayaficha hukohuko!! au tunaiba majembe tunaficha vichakani lengo

ni ili tukafanye vibarua vya kilimo kwenye mashamaba ya watu kwa siri!..na tulikuwa tuna fanya vizuri zaidi hata kwa kurudia rudia ili siku nyingine watupe kazi lkn kwa masharti kuwa wasiseme nyumbani kuwa tunafanya vibarua!!

Kweli tulipata hela si kawaida!! tulicho kifanya sasa!! ni kuwa shule ilipo fungwa tulienda likizo kwa hela yetu Mama hakuamini kwa umri ule wa miaka 8 niliweza fanya bishara....lkn Baba yeye aliamini nauli ile tumepewa na Mama kwa njia anazo jua yeye!

safari za kwenda kwa wazazi zilitusaidia sana kwani maisha yali badilika kwa kiasi!........kwa kuwa kwa upande wa lishe ilikuwa ni Duni mnoo!...siku tunakula vizuri ni baba yetu aje!...au japo mgeni akija chakula kizuri kitapatikana!

Mbona hiyo yako mwana cha mtoto...yaani utishie kukataa shule??mweee?? .... unapigiwa makofi kabisaa wewe shujaa una akili......sasa utaenda kuchunga mifugo kutwa nzima na kulima kila siku asubuhi!...hutaki huliii......

Yaani kwetu sisi kwenda shule ilikuwa ni Bonge la shushuuuu!!...umepona kilimo....umepona kuchunga...kuteka maji hovyo ujaze pipa, haya na mifugo usumbufu mara mbung'o mara jua, mara mvua mweee!...unanuka jasho! nilichukia hayooo!!

Lkn drsani aaah!! unakaa unatulia kivulini potelea kwa mbali usile kutwa nzima lkn uko kivulini! kisa unasoma daaa nilipenda kweli shule!
 
hicho cha Mtoto mie niliishi na chawa pamoja na utititri kuku, nikiwa na shangazi yangu!!! na jiulize nyumba ya nani??? ya Baba yangu mzazi!!.. .Mama hakupenda tuishi ivo na alikuja kutuchukua kwa nguvu tukaenda mjinii...

Ajili ya kujimwambafy Baba akachukia kwa kile kitendo!! kuwa amedharauliwa ..alicho kifanya Baba baaada ya week moja ya kuishi nae mjini akaturudisha kijijini kwa lazimaaa!......kufika kule tukaishi na maisha yakawa magumu mara dufu!!

Kuanzia kula, kulala na uniform za shule Mtoto wa kike lkn sare matakoni imechanika hana hata chupi ulikuwa ni udhalili wa hali ya juu sana! kwa hali km ile ya kuchekwa ilibidi tujitenge na wengine!! tukajifunza kushona viraka kwa lazima kwa msaada wa jirani!.....

kadri hali ilivokuwa mbaya tukajifunza kufanya vibarua na biashara kwa siri kubwa km hivi tukiagizwa majembe shuleni sisi tulikuwa haturudi nayo nyumbani!! tunayaficha hukohuko!! au tunaiba majembe tunaficha vichakani lengo

ni ili tukafanye vibarua vya kilimo kwenye mashamaba ya watu kwa siri!..na tulikuwa tuna fanya vizuri zaidi hata kwa kurudia rudia ili siku nyingine watupe kazi lkn kwa masharti kuwa wasiseme nyumbani kuwa tunafanya vibarua!!

Kweli tulipata hela si kawaida!! tulicho kifanya sasa!! ni kuwa shule ilipo fungwa tulienda likizo kwa hela yetu Mama hakuamini kwa umri ule wa miaka 8 niliweza fanya bishara....lkn Baba yeye aliamini nauli ile tumepewa na Mama kwa njia anazo jua yeye!

safari za kwenda kwa wazazi zilitusaidia sana kwani maisha yali badilika kwa kiasi!........kwa kuwa kwa upande wa lishe ilikuwa ni Duni mnoo!...siku tunakula vizuri ni baba yetu aje!...au japo mgeni akija chakula kizuri kitapatikana!

Mbona hiyo yako mwana cha mtoto...yaani utishie kukataa shule??mweee?? .... unapigiwa makofi kabisaa wewe shujaa una akili......sasa utaenda kuchunga mifugo kutwa nzima na kulima kila siku asubuhi!...hutaki huliii......

Yaani kwetu sisi kwenda shule ilikuwa ni Bonge la shushuuuu!!...umepona kilimo....umepona kuchunga...kuteka maji hovyo ujaze pipa, haya na mifugo usumbufu mara mbung'o mara jua, mara mvua mweee!...unanuka jasho! nilichukia hayooo!!

Lkn drsani aaah!! unakaa unatulia kivulini potelea kwa mbali usile kutwa nzima lkn uko kivulini! kisa unasoma daaa nilipenda kweli shule!
Yote Kwa yote, kuachwa na wazazi ukiwa bado mdogo, ni kama dunia Kuwa juu ya mabega, hakuna cha yeyé alikuwa na afadhali, kwamba wewe ilikuwa ni zaidi...Hakuna yatima ni yatima tuu..
 
Yote Kwa yote, kuachwa na wazazi ukiwa bado mdogo, ni kama dunia Kuwa juu ya mabega, hakuna cha yeyé alikuwa na afadhali, kwamba wewe ilikuwa ni zaidi...Hakuna yatima ni yatima tuu..
Ni kujiendekeza tu!!! ili waonewe huruma!! Dunia ni nzuri sana hasa ukimjua Mungu tena km huyo yatima ndo Mungu atamtizama kwa jicho la karibu sana...tumeona wengi waliishi maisha mazuri mara dufu!! wewe siyo yatima wa kwanza!! wangapi wana wazazi walevi??

wangapi wametelekezwa tena ni afadha;i ya yatima ukipima maisha yao!
 
Pole kwa uliyoyapitia na ongera kwakuyavumilia yote hadi hapa ulipo sasa
Maisha tunayoishi yanachangamoto nyingi na vikwazo pia ambavyo wasababishi ni sisi wanadamu sababu ya chuki, wivu, na majivuno tuliyonayo hakuna anayetamani shida nashukuru umetusihi tujitahidi kuzihepuka
Kama tukijitahidi kuuishi upendo maisha yatakuwa na furaha sana
 
Hakuna sababu watu wanayoipataga kama niliishi kwa ndugu nikateswa nini nini sjui weee jamani maisha haya kuna wanaoachwa hata pa kulala hamna sembuse hata wewe ulisona tuition na bado uka fail.

Mimi nina mifano hai kabisa na kuishi na watoto wa ndugu ninalea vijana na mabint wa ndugu, nimeolewa mm na mume wangu tunalea na watoto wa ndugu pia na wadogo wa mume wangu mwanzoni mdogo wa mr tulimuuliza atakaa home hadi lini aseme anataka kufanya nn twna baada ya kuona anashinda ktk tv muda woote kakaa sebulen na remote

Nilivyokaa nae chini akaniambia shem nataka ni risit sabab kijijin mama wa kambo alikua hanipendi so sikusoma vizuri, huyu ana share mama na mr alilelewa kwa babake mzazi naa mama yake wa kambo, ikabidi niongee na mr tuka mrudisha shule karisiti awamu tatu hakupata credit na alipewa everything akawa analazimisha aende form 5 huku anarisit nikakataa sabab kashindwa kupata credit hana mzigo atazipata akiwa na mzigo wa wa 5.

Nikamwambia chagua ujuzi wowote ule uwe nao kwanza kama kushona,udereva n.k akachagua driving tukajipanga akapelekwa veta kusoma ili akiroka hapo aende nit chuo kufanya mtihan wa driving veta akafail mitihan 2 yeye tu.

Akapangiwa ajiandae airudie akasepaaa hakutaka hata kurudia na juzjuz katuambia hataki driving sabab anaogopa kuendesha gari[emoji23].alivyokataa mr akampeleka kusimamia mifugo na akamuwekea vijana wa kazi yeye ndo awe msimamizi

Alichofanya alihakikisha katimua wafanyakazi wote akasema wanamsumbua ataweza hata akiwa peke yake, ikabidi mbuzi akapeleka kwa wamasai kwa makubaliano maalumu na kuku alizobaki nazo sasa zilivyoanza kutaga akaona kaanza shika pesa kibùri kikaanza matanuzi yakaanza ikawa kila siku anasema kuku wamegongwa na nyoka mara nimeibiwa kuku 70 kumbe anauza mara hivi

Kumbe ameshampa mimba mtu na kuzaa nae kwa pesa ndogo tu aliyoanza shika mwishon tuliuza kuku zilizobakia kwa hasira bado kuna vitu ana simamia ila hajawahi kujifunza hadi leo.kijana kama huyu na chance zoote alizopewa kesho atakuja kulaumu nimeishi kea bro hakunisaidia.jamani kuishi na ndugu ambae si mzazi wako jua kua kile anakupatia ni msaada tu si jukumu lake hivyo ni kua na moyo wa shukurani hata kwa kidogo unachopewa.

Dogo tumemuacha dunia mnyooshe ila tukiona kanyooka kama ruler kuna mtaji tutampa kama last chance kwake.niongezee hapo manda ya kuku yupo nayo hapohapo kila tukienda ukikuta leo kaweka kuju wa tatu mwez ujao ukienda hujuti kuku woote kala/kauza ila tunaona siku tukienda tukakuta kajiongeza kuanza na kidogo na tukaona anajikongoja ndo hapo atapopewa mtaji ajiongeze.

Namalizia hivi, Kuishi na ndugu ni lawama sana labda kama hajawahi ishi nao na pia ndugu mnaoishi kwa watu msijicompee na watoto wa wenye nyumba hamuwezi ishi sawa hata huyo baba na mama mwenye nyumba ni jukumu lake kuwalea wanawe ila wewe ni msaada tu anakupatia
Yatima kwa tafsiri ni mtoto aliyefiwa na wazazi wote wawili yaani baba na mama muda huo huo umri wake ukawa chini ya miaka 18.

Habari ndugu zangu, uzi wangu utaelezea hadha wapitiazo watoto yatima kimalezi na makuzi au watoto waliotelekezwa na wazazi wao (sio wote wanapitia ila naamini ni wengi).

Kama wewe ni kati ya watu waliopewa/kuachiwa jukumu la kulea mtoto/watoto wa ndugu yako basi unaweza kujifunza kitu hapa.

Twende pamoja sasa;

Mimi nikijana kwa majina naitwa Henerico. Ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto watatu. Mama yangu alijaaliwa kuzaa mara mbili yaaani mimi ndio wakwanza na wadogo zangu wawili wanaonifuata ni mapacha yaaani Kulwa na Doto wote hawa ni wanaume.

Kwa upande wangu mimi kama mtoto wa kwanza kwa mama yangu baba yangu aliikataa mimba yangu kwa mujibu wa maelezo ambayo nayasikia toka nikiwa mtoto. Wadogo zangu pia wenyewe wana baba yao ila hawajaishi nae alipozaa tu na mama yangu baba yao aliondoka na hakujulikana kaenda wapi kwa hiyo wote tukabaki na malezi ya upande wa mama.

Kwa bahati mbaya me nikiwa na umri wa miaka 6 na wadogo zangu wakiwa na miaka 3 mama yangu alifariki dunia. Kwa wakati huo sikuona kama kuna shida au sikuhisi kama uyatima umeingia bali niliona ni kitu cha kawaida nadhani ni kutokana na umri wangu ulikuwa bado mdogo ila kumbukumbu kichwani kwangu bado ninazo mpaka msiba ulivyoendeshwa. Msiba ulipita na maisha mengine yakaendelea tukiwa tunaishi na bibi yetu na mama zetu wadogo na wakubwa.

Mwaka mmoja baada ya msiba niliweza kupelekwa shule darasa la kwanza, bibi yangu na mama zangu wakubwa ndio walikuwa wahusika wakubwa.

Mpaka naanza shule nilikuwa bado sijaona pengo la mama. Nilipofika darasa la tatu ndio nilitambua pengo la mama lipo wapi.

Nilikuwa nafanya mafundisho ili nibatizwe na mafundisho niliyafanya kwa muda wa miaka mitatu toka nikiwa darasa la kwanza mpaka nilipofika darasa la tatu ndio nilikuwa nahitajika nibatizwe. Kwa bahati mbaya nilikuwa sijalipa hela ya zaka mpaka ile siku ambayo usiku wake ndio nilikuwa nahitajika nibatizwe mpaka kufikia saa 10 jioni bado sijapata hela ya zaka, mda huo katekista ananiambia 'ujalipa hela ya zaka uwezi kubatizwa', nikifikiria mafundisho nimefanya kwa muda wa miaka mitatu halafu leo hii nisibatizwe aiseee NILILIA.... Bibi yangu angekuwa na hela angenipatia ila wakati huo na yeye alikuwa hana pesa. Nikienda kwa mama zangu wakubwa wanatupiana mpira ukienda kwa huyu anakwambia nenda kwa yuleeee... NILIMWAGA CHOZI na ndiyo siku hiyo nilipoanza maombolezo ya mama yangu.

Ilipofika jioni mama yangu mkubwa alipojihakikishia nimekosa kwa ndugu wote ndipo aliponipatia pesa (7,500) nikaenda chapu kulipia nikarudi nyumbani kujiandaa kwenda ibadani kubatizwa. Ila hapo macho yamenivimba kwa kulia na kiukweli nisingebatizwa ile siku nilikuwa najiandalia safari niende ovyo nikawe mtoto wa mtaani.

Usiku wa ubatizo ulipofika nilikutana na msimamizi wangu wa ubatizo nikiwa nimevaaa yale majaketi makubwa ili kuficha shati langu la ndani, lilikuwa limechanika, yeye hakutambua lile koti kubwa vile nimelivaa la nini, Akaniamuru nilivue, nilipolivua ndipo alipogundua kuwa nimelivaa koti kwasababu gani Ikabidi awe mpole akaniambia basi nilivae tu!! Ibada ya ubatizo ilienda vizuri. Tukarudi nyumbani kuendelea na maisha.

Ile usiku wa ubatizo hadi leo naikumbuka jinsi wenzangu walivyokuwa wamependeza, wanapiga picha na kuvishwa mataji na ndugu zao. Huwa nacheka sana na kuuona Ukuu wa Mungu maana kwa wakati huo wala sikuwa na akili ya kuwaza au akili ya kutamani wenzangu walivyopendeza, akili yangu yote iliwaza nibatizwe.

Baada ya ile siku ya ubatizo ndipo nilipoanza kutambua thamani ya mama. Toka siku hiyo nilianza kuwa namlilia mama yangu, sikuwa naamani tena moyoni mwangu, maisha ya upweke ndipo yalipoanzia hapo. Nilianza kujiona ni mtoto mwenye mapungufu makubwa sana tofauti na watoto wenzangu.

Nilimaliza darasa la saba kiugumu sana maana shule nilianza kuichukia sana.

Kabla sijamaliza shule alikuja mtoto wa mama yangu mkubwa tukaungana nae darasa moja alitokea kijijini, tukawa tunaishi kwa bibi na watoto wengine wa mama zangu wakubwa pamoja na wadogo zangu. Ila kiukweli maisha hayakuwa mazuri sana wala mabaya sana. Tukafaulu shule moja mimi na huyo ndugu yangu yaaani kidato cha kwanza.

Ulipofika muda wakufanya maandalizi ya kwenda shule ndipo ilikuwa kimbembe sasa. Mama yangu mkubwa anashindwa kumpeleka mtoto wake shule kwasababu yangu mie, jamii itamuonaje ampeleke mtoto wake shule halafu mimi nibaki kitaaa!! Mama yangu mkubwa alipitia kipindi kigumu sanaa nilitamani nimwambie ampeleke tu kwanza mwenzangu ambae ni mtoto wake mimi nisiwe sababu ya mwenzangu kutokwenda shule ila nikabaki na mgogoro na nafsi yangu nikawa najiona na hatia yaani sikupenda niwe chanzo cha mwenzangu asiende shule. Ila nashukuru Mungu mwisho wa siku walijipiga piga na wote tukaenda shule. Wabarikiwe kwa hilo. Japo nilisoma huku najiona kabisa ni mzigo kwa ndugu zangu.

Maisha yalisonga na masomo yalisonga ila changamoto zilikuwa zipo nyingi sanaaa. Mtoto wa mama yangu mkubwa alikuwa hapendi shule, alikuwa anaenda shule kutimiza wajibu tu. Kwahiyo nilipokuwa nahitaji kusoma twisheni ilibidi niwe namtumia huyu mwenzangu kwa kumbembeleza amwambie mama yake ambaye ni mama mkubwa kuwa tunataka tusome twisheni atulipie ikawa ndio maisha yangu ya uchawa kwa ndugu yangu ili maisha yaende. Ila mwisho wa siku alinigomea kuwa chawa wake. Ikabidi twisheni iishie hapo ila bado nikawa nikiwa na shida ya mahitaji ya shule nilikuwa nasubiria mpaka mwenzangu nae apate shida kama yangu yaaani nikawa naishi kwa kusafiria nyota. Nilikuwa sipendi kuonekana mimi ndio na mahitaji mengi kuliko mtoto wake.

Wadogo zangu muda huo nasoma na wenyewe pia walikuwa wanasoma ila kwa bahati mbaya wadogo zangu walikuwa watukutu sana toka wakiwa wadogo, walikuwa hawapendwi kutokana na tabia zao. Kuna siku nilimsikia mama yangu mkubwa anawaambia 'kamtafuteni baba yenu' niliumia sana..., niliingia ndani nililia sana nikafikiria baba yao hata hawamjui inakuwaje wanatamkiwa kauli kama ile? Nilikosa majibu zaidi niliishia kulia tu!! Ila hakuna aliyejua kama nililia.

Nilimaliza shule vizuri. Na kwa bahati mbaya matokeo yalipotoka hayakuwa mazuri. Na moja kwa moja niliyaanza maisha rasmi maana pale nyumbani nilipachukia kwa hiyo nilihitaji kuwa na maisha yangu.

Katika malezi niliyolelewa kwa kiasi fulani ndio matokeo ya maisha yangu ya sasa Kama vile;
  • kutojiamini,
  • hasira na chuki,
  • kutokufanya vizurii katika masomo,
  • kuathirika kisaikolojia,
  • Kuathiri mwenendo mzima wa maisha ya baadae hasa kifamilia.

Walezi/wazazi fanyeni hivi ili kupunguza watoto wa mitaani;

- Walezi/wazazi tunapoamua kulea watoto/mtoto ambae sio wako tujitahidi kuweka usawa na hata kama msipoweka usawa basi mjitahidi msioneshe moja kwa moja. Hii hali iliniathiri kwa kiasi fulani nakupelekea kuichukia shule.

- Wazazi/walezi tuchungeni kauli zetu sio vizurii kuwaropokea watoto kauli tata ambazo zitampelekea mtoto maumivu na kutamani kujitenga na nyumbani. Hali hii ilipelekea mdogo wangu kuhasi nyumbani na kuwa mtoto mitaani.

- Wazazi tujitahidi kuwafundisha watoto wetu ili upendo, pindi wachanganikapo na watoto wengine ambao wazazi wao hawapo basi waweze kuishi nao bila ubinafsi. Hii ilinitokea mimi, ilifikia hatua mtoto wa mama yangu mkubwa ananiambia 'usitumie kitu fulani kwani kanunua mama yako?' Hali hii inaweza pelekea mtoto kujizira nakupelekea hata kujizuru au kwenda mitaani.

- Walezi tujitahidi kuwa na moyo wa kutoa mahitaji kwa watoto yatima, kutimiza ndoto zao. Tukifanya hivyo mtoto atajihisi na thamani wala hawezi kuwaza yeye ni yatima, hawezi kutamani maisha ya kwenda kuishi mitaani. Mfano mimi nilipokosa hela ya kutoa zaka kanisani nibatizwe, nilijisemea katika moyo wangu 'nisipobatizwa basi bora niende ovyoo'.

HITIMISHO; Wazazi tuombe sana MUNGU atujaalie uhai mrefu na tujiepushe na visababishi ambavyo vitapelekea kufupisha uhai wetu au kupunguza umri wetu wa kuishi duniani ili tulee watoto wetu.
Uyatima sio mzuri, mwanao unavyomlea usifikirie na mwingine atamlea hivyo, atamvumilia kama vile wewe unavyomvumilia hapana sio rahisi hasa kwenye hizi familia zetu za kipato cha chini.

Tuishi kwa maangalizo pindi pale tunapopata nafasi basi tujitahidi kuwekeza kwa watoto wetu upendo, elimu, na rasilimali ambazo zinaweza kuja kuwafaa badae endapo kama kifo kitabisha hodi.

MWISHO.

WENU MTIIFU HENERICO.
 
Ni kujiendekeza tu!!! ili waonewe huruma!! Dunia ni nzuri sana hasa ukimjua Mungu tena km huyo yatima ndo Mungu atamtizama kwa jicho la karibu sana...tumeona wengi waliishi maisha mazuri mara dufu!! wewe siyo yatima wa kwanza!! wangapi wana wazazi walevi??

wangapi wametelekezwa tena ni afadha;i ya yatima ukipima maisha yao!
Kwahiyo yatima hapaswi kuonewa hata huruma, kwamba wanajiendekeza, Karma inajirudia, Muombe sana mungu vizazi vyako visipitie wanayopitia Mayatima...
 
Kwahiyo yatima hapaswi kuonewa hata huruma, kwamba wanajiendekeza, Karma inajirudia, Muombe sana mungu vizazi vyako visipitie wanayopitia Mayatima...
Uwaonee huruma wewe nani>> !! Mungu aliye wafanya ivo anajua kwa nini wako ivo! usilazimishe kuwaonea huruma unajidanganya! huo ni ushetani ....utaonea huruma mpaka na mapepo weee!! jipendekeze tu!! siku likikukamata nyaa!! ndo utakumbuka maneno yangu!!
 
Hakuna sababu watu wanayoipataga kama niliishi kwa ndugu nikateswa nini nini sjui weee jamani maisha haya kuna wanaoachwa hata pa kulala hamna sembuse hata wewe ulisona tuition na bado uka fail.mimi nina mifano hai kabisa na kuishi na watoto wa ndugu ninalea vijana na mabint wa ndugu.nimeolewa mm na mume wangu tunalea na watoto wa ndugu pia na wadogo wa mume wangu mwanzoni mdogo wa mr tulimuuliza atakaa home hadi lini aseme anataka kufanya nn twna baada ya kuona anashinda ktk tv muda woote kakaa sebulen na remote nilivyokaa nae chini akaniambia shem nataka ni risit sabab kijijin mama wa kambo alikua hanipendi so sikusoma vizuri.huyu ana share mama na mr alilelewa kwa babake mzazi naa mama yake wa kambo.ikabidi niongee na mr tuka mrudisha shule karisiti awamu tatu hakupata credit na alipewa everything akawa analazimisha aende form 5 huku anarisit nikakataa sabab kashindwa kupata credit hana mzigo atazipata akiwa na mzigo wa wa 5.nikamwambia chagua ujuzi wowote ule uwe nao kwanza kama kushona,udereva n.k akachagua driving tukajipanga akapelekwa veta kusoma ili akiroka hapo aende nit chuo kufanya mtihan wa driving veta akafail mitihan 2 yeye tu.akapangiwa ajiandae airudie akasepaaa hakutaka hata kurudia na juzjuz katuambia hataki driving sabab anaogopa kuendesha gari[emoji23].alivyokataa mr akampeleka kusimamia mifugo na akamuwekea vijana wa kazi yeye ndo awe msimamizi alichofanya alihakikisha katimua wafanyakazi wote akasema wanamsumbua ataweza hata akiwa peke yake ikabidi mbuzi akapeleka kwa wamasai kwa makubaliano maalumu na kuku alizobaki nazo sasa zilivyoanza kutaga akaona kaanza shika pesa kibùri kikaanza matanuzi yakaanza ikawa kila siku anasema kuku wamegongwa na nyoka mara nimeibiwa kuku 70 kumbe anauza mara hivi kumbe ameshampa mimba mtu na kuzaa nae kwa pesa ndogo tu aliyoanza shika mwishon tuliuza kuku zilizobakia kwa hasira bado kuna vitu ana simamia ila hajawahi kujifunza hadi leo.kijana kama huyu na chance zoote alizopewa kesho atakuja kulaumu nimeishi kea bro hakunisaidia.jamani kuishi na ndugu ambae si mzazi wako jua kua kile anakupatia ni msaada tu si jukumu lake hivyo ni kua na moyo wa shukurani hata kwa kidogo unachopewa.
Dogo tumemuacha dunia mnyooshe ila tukiona kanyooka kama ruler kuna mtaji tutampa kama last chance kwake.niongezee hapo manda ya kuku yupo nayo hapohapo kila tukienda ukikuta leo kaweka kuju wa tatu mwez ujao ukienda hujuti kuku woote kala/kauza ila tunaona siku tukienda tukakuta kajiongeza kuanza na kidogo na tukaona anajikongoja ndo hapo atapopewa mtaji ajiongeze.
Namalizia hivi
Kuishi na ndugu ni laqama sana labda kama hajawahi ishi nao.na pia ndugu mnaoishi kwa watu msijicompee na watoto wa wenye nyumba hamuwezi ishi sawa hata.huyo baba na mama mwenye nyumba ni jukumu lake kuwalea wanawe ila wewe ni msaada tu anakupatia
Acha hizo weye mtoto analindwa na kusomeshwa kwa meeengi sana wewe km mlezi jitoe kwa yote!! msijifanye hamjui!! nyie mnampa msaada ili muonekane tu lkn kuna misaada mingine mnamfichia asiipate ...haya niliyaona mkwa libabaangu dogo lilikuwa lina nibania pamoja na kunipa kila kitu nikagundua faster nikampiga chini!
 
Back
Top Bottom