Changamoto ujenzi wa nyumba zetu na tetemeko la ardhi

mlekulechoma

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2014
Posts
1,366
Reaction score
1,059
Naenda kwenye mada moja kwa moja!Kufuatia tetemeko la ardhi lilitokea kanda ya ziwa na kuleta madhara makubwa ikiwemo kubomoka kwa nyuma na baadhi kupoteza maisha nimebaini yafuatayo
1.Ujenzi wa nyumba zetu hauzingatii viwango.....na kwa bahati mbaya tutaogopa kulisemea hili kama kawaida yetu!ukiangalia nyumba nyingi zilizobomoka...ukichunguza kwa makini utabaini mapungufu mengi sana....hazina renta kwa mfano(angalia picha vizuri)....hapa ndo utajiuliza je taratibu za ujenzi zinazingatiwa?ukaguzi wa nyumba zinazojengwa unafanyika?vibali vya ujenzi je?
2.Nyumba nyingi zilizobomoka hasa bukoba mjini ni za zamani sana,zimechoka ni kaka magofu lakini watu bado wanayatumia!mamlaka ziko wapi?ukaguzi wa majengo haya kubaini uimara wake unafanyika?
Pamoja na mapungufu hayo hapo....bado elimu kwa umma kushusu majanga ni tatizo pia!hata upatikanaji wa taarifa kabla ya tukio ni tatizo/changamoto pia!
Swali la kujiuliza....je likitokea tena si bukoba tu bali sehemu yoyote ile Tanzania....tutaweza epuka madhara makubwa yasitokeee?na changamoto hizi za ujenzi wa nyumba zetu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…