SoC04 Changamoto ya Maji Itamalizwa Kwa "Desalination", Teknolojia Ya Kisasa Kwa Nchi Kubwa

SoC04 Changamoto ya Maji Itamalizwa Kwa "Desalination", Teknolojia Ya Kisasa Kwa Nchi Kubwa

Tanzania Tuitakayo competition threads

Ghost MVP

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2022
Posts
439
Reaction score
736
TATIZO LA MAJI LITAISHA KWA NAMNA HII

1199.jpg

Chanzo Cha Picha: Freepik
Tatizo la maji katika nchi yetu hii ya Tanzania ni changamoto kubwa inayokabili nchi, Mijini na vijijini. miundombinu ya maji safi na salama isiyo na ubora ni moja ya sababu kuu. Maeneo mengi hayana mabomba ya maji ya kutosha au yaliyopo ni madogo, na yanayotegemewa mara nyingi hayafanyi kazi ipasavyo. Vyanzo vya maji vya asili kama mito na visima vimeharibika kutokana na shughuli za kibinadamu kama ukataji miti na uchimbaji madini, Mabadiliko ya Tabia Nchi kama upungufu wa mvua, hali inayosababisha ukosefu wa maji safi kutokana na Mito mingi kukauka.

Mabadiliko ya tabianchi yameathiri upatikanaji wa maji. Ukame na mabadiliko yasiyotabirika ya hali ya hewa yamepunguza kiwango cha mvua kwa kiasi kikubwa sana, hivyo kupunguza upatikanaji wa maji. Katika baadhi ya maeneo, watu hulazimika kutembea umbali mrefu kutafuta maji, jambo ambalo linaathiri sana afya na ustawi wa jamii, hususan wanawake na watoto.

Kwa miaka Mingi tumekuwa tukiangalia Namna moja tu ya kupata maji kupitia Vyanzo vya asili kama Mito na visima ambapo vyanzo hivi vikikumbwa na adha basi maji yanakuwa ya shida na mgao, na Serikali Pamoja na wadau mbalimbali wa maji wamekuwa chini sanaa kuangalia namna nzuri ya kukabiliana na tatizo hili, Mwisho wa siku husingizia Mvua hakuna mara hiki mara kile.

Mapendekezo yangu Juu ya Janga hili la taifa, ili ifikapo 2025 basi Tanzania tuwe na Maji ya kutosha kwaajili ya matumi ni kama Yafutayo

1: Kujenga matanki makubwa na mengi ya kuhifadhi maji

2: Kutumia Technolojia ya kutakatisha maji ya Chumvi/Bahari na kuwa maji safi

---------------------------------------------------------------------

1: UJENZI WA MATANKI MAKUBWA

Ujenzi wa matanki haya makubwa ya kuhifadhi maji unaweza kusaidia kumaliza na kukabiliana na tatizo la maji nchini Tanzania kwa njia nyingi.

AdobeStock_32902779-featured.jpg

Chanzo cha Picha: Mtandaoni
Kwanza, matanki haya yanaweza kukusanya na kuhifadhi maji wakati wa mvua nyingi, hivyo kuhakikisha upatikanaji wa maji wakati wa ukame au ambacho mvua zitapotea/Kupungua. Hii itapunguza utegemezi wa vyanzo vya maji visivyoaminika na kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Pili, matanki hayo makubwa yanaweza kujengwa karibu na maeneo yenye uhaba wa maji, hasa vijijini na maeneo ya mijini yenye msongamano mkubwa wa watu na matumizi ya maji. Hii itapunguza umbali na muda unaotumiwa na watu, hasa wanawake na watoto, kutafuta maji, na hivyo kuboresha afya na ustawi wa jamii, na pia Kuchangia bei ya maji kushuka.

Tatu, matanki ya maji yanaweza kusaidia katika kuhifadhi maji safi kwa matumizi ya nyumbani, kilimo, na mifugo. Hii itaimarisha usalama wa chakula na kuleta ustawi wa kiuchumi kwa jamii, kwani maji ni rasilimali muhimu katika kilimo na ufugaji.

Uwekezaji katika matanki makubwa ya maji na Ujenzi wake ni hatua muhimu kuelekea suluhisho la kudumu la tatizo la maji Tanzania, Kama ilivyo kwa Matanki ya kuhifadhi mafuta badi tuwe na matanki makubwa zaidi kwaajili yam aji kwa mikoa yenye Msongamano wa watu

2: TEKNOLOJIA YA KUTAKATISHA MAJI YA CHUMVI/BAHARI NA KUWA MAJI SAFI

Mfumo unaotumia kutakatisha maji ya bahari kuwa maji safi unaitwa "mchakato wa kusafisha maji ya bahari" au "desalination”. Teknolojia hii inajumuisha njia mbalimbali, lakini njia kuumbili ni:

resized1-1.jpeg

Chanzo cha Picha: Shutterstock
  1. Reverse Osmosis (RO) - Mfumo huu hutumia shinikizo kubwa kusukuma maji ya bahari kupitia membrani maalum inayochuja chumvi na uchafu mwingine, hivyo kutoa maji safi ya kunywa.
  2. Distillation - Njia hii inahusisha kuchemsha maji ya bahari na kukusanya mvuke wake, kisha kuupooza ili kuwa maji safi. Chumvi na uchafu mwingine huachwa nyuma kwenye mchakato wa kuchemsha.
education-six-step-process.jpg

Chanzo Cha Picha: Mtandaoni
Mbinu hizi mbili ni maarufu zaidi na hutumika katika maeneo mengi duniani kwa ajili ya kuzalisha maji safi kutoka baharini, Nchi nyingi zilizopo maeneo yenye uhaba wa maji hutumia Mfumo wa “Desalination” kama chanzo kikuu cha Maji katika taifa Nchi hizo ni kama:-

  • Saudi Arabia - Inaongoza duniani kwa uzalishaji wa maji kupitia desalination.
  • United Arab Emirates (UAE) - Ina mitambo mingi ya desalination kwa ajili ya mahitaji ya maji.
  • Kuwait - Karibu maji yote ya matumizi ya nyumbani yanatokana na desalination.
  • Qatar - Hasa inategemea desalination kwa ajili ya maji safi.
  • Bahrain - Inatumia desalination kwa kiasi kikubwa kuzalisha maji safi.
  • Oman - Ina mitambo mingi ya desalination inayozalisha maji kwa matumizi ya nyumbani na viwandani.
  • Israel - Imekuwa mstari wa mbele katika kutumia desalination kwa maji safi.
  • Australia - Maeneo kama Perth yanategemea desalination kwa maji safi.
Gharama za kufunga mfumo wa desalination zinaweza kutofautiana sana kulingana na aina ya teknolojia inayotumika, ukubwa wa mtambo, eneo la ujenzi, na mahitaji maalum ya mradi. Hata hivyo, kuna makadirio ya jumla ya gharama kwa aina mbili kuu za teknolojia ya desalination:

1. Distillation (Thermal Desalination):

  • Gharama za awali za ujenzi: Hizi zinaweza kuwa juu zaidi, kati ya $2,000(TZS 5.2M) hadi $10,000(TZS 26M) kwa kila mita moja ya ujazo wa uwezo wa uzalishaji wa maji kwa siku (m³/day) Yaani sawa Na Lita 1,000 za maji au Uniti 1.
  • Gharama za uendeshaji: Hizi zinaweza kuwa kati ya $1.00(TSZ 2000) hadi $3.00(TSZ 7,000) kwa kila mita ya ujazo ya maji inayozalishwa, kutokana na matumizi makubwa ya nishati ya mafuta au umeme.
2.Reverse Osmosis (RO):

  • Gharama za awali za ujenzi: Hizi zinaweza kuwa kati ya $1,000(TSZ 2.6M) hadi $5,000(TSZ 13M) kwa kila mita moja ya ujazo wa uwezo wa uzalishaji wa maji kwa siku (m³/day). Kwa mfano, mtambo wenye uwezo wa kuzalisha mita za ujazo 50,000 Yaani Lita Milioni 50 kwa siku unaweza kugharimu kati ya $50 milioni(TZS Bilioni 131,750,000,000) hadi $200 milioni.
  • Gharama za uendeshaji: Hizi ni kati ya $0.50 hadi $2.00 kwa kila mita ya ujazo ya maji inayozalishwa. Gharama hizi zinajumuisha nishati, matengenezo, na uendeshaji wa kila siku.
Hamburg_Desalination_Plant.jpg

Chanzo cha Picha: Mtandaoni
HIvyo Tanzania tunaweza kukabiliana na Uhaba wa maji Kwa njia hizi za Awali, Katika bajeti ya maji ukijumlisha na Wawekezaji tunaweza Kusema Bye bye kwa Uhaba wa maji Nchini.
 
Upvote 11
Back
Top Bottom