A
Anonymous
Guest
Changamoto yetu kubwa kutoka Mtaa wa Kanindo Kata ya Kishiri Nyamagana Mwanza ni suala la maji hakuna kabisa.
Wakazi wa maeneo haya wanapata sana tabu ya kupata maji hata ya kunywa. Mradi wa maji ushakamilika huu mwaka sasa wananchi hawajui ni nini changamoto haswa bomba za maji kutosambazwa mitaani.
Ilifika hatua baadhi ya wananchi walikusanyika na kutaka kuchanga pesa wasogozewe maji ila wakasema maji yapo karibuni kuwafikia, sasa ni zaidi ya miaka miwili
Hivi ni baadhi ya vyanzo nya maji wanayotegemea.
=======================
Hapa kwetu Mwanza kuna miradi ya maji kadhaa lakini ninachojiuliza mbona kero za uhaba wa maji bado ni nyingi? Mfano kwa Wananchi wa Mtaa wa Kanindo, Kata ya Kishiri Wilayani Nyamagana.
Wananchi wa huko wengi wao hawana huduma ya maji ya bomba (MWAUWASA), hali hiyo inawafanya kutumia maji ya kisima kama mbadala.
Hali ya ukosefu wa maji si tu kwa wasio na mabomba bali hata kwa wenye mabomba kwani nao wameyaacha mabomba yao yakiwa makavu na kupanga foleni kisimani kusubiri maji ya kununua ambayo si salama.
Ameeleza kwa muda mrefu sasa toka wameanza kupaza sauti zao kuhusu kero hiyo lakini wamepewa majibu yasiyoleta utekelezaji huku wakizidi kuumia kwa kutumia maji yasiyo safi na salama ambayo hata wanyama wamekuwa wakitumia pia.
Pia, soma: MWAUWASA: Tumeandaa Mradi wa Tsh. Bilioni 8.4 kufikisha Huduma ya Maji maeneo ya Kishiri na jirani ambayo hayana huduma hiyo.
Wakazi wa maeneo haya wanapata sana tabu ya kupata maji hata ya kunywa. Mradi wa maji ushakamilika huu mwaka sasa wananchi hawajui ni nini changamoto haswa bomba za maji kutosambazwa mitaani.
Ilifika hatua baadhi ya wananchi walikusanyika na kutaka kuchanga pesa wasogozewe maji ila wakasema maji yapo karibuni kuwafikia, sasa ni zaidi ya miaka miwili
Hivi ni baadhi ya vyanzo nya maji wanayotegemea.
=======================
Hapa kwetu Mwanza kuna miradi ya maji kadhaa lakini ninachojiuliza mbona kero za uhaba wa maji bado ni nyingi? Mfano kwa Wananchi wa Mtaa wa Kanindo, Kata ya Kishiri Wilayani Nyamagana.
Wananchi wa huko wengi wao hawana huduma ya maji ya bomba (MWAUWASA), hali hiyo inawafanya kutumia maji ya kisima kama mbadala.
Hali ya ukosefu wa maji si tu kwa wasio na mabomba bali hata kwa wenye mabomba kwani nao wameyaacha mabomba yao yakiwa makavu na kupanga foleni kisimani kusubiri maji ya kununua ambayo si salama.
Ameeleza kwa muda mrefu sasa toka wameanza kupaza sauti zao kuhusu kero hiyo lakini wamepewa majibu yasiyoleta utekelezaji huku wakizidi kuumia kwa kutumia maji yasiyo safi na salama ambayo hata wanyama wamekuwa wakitumia pia.
Pia, soma: MWAUWASA: Tumeandaa Mradi wa Tsh. Bilioni 8.4 kufikisha Huduma ya Maji maeneo ya Kishiri na jirani ambayo hayana huduma hiyo.