Chanjo ya kichocho ilinishangaza ndiyo maana hata ya Corona naiogopa

Chanjo ya kichocho ilinishangaza ndiyo maana hata ya Corona naiogopa

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
21,643
Reaction score
51,642
Mimi sijui chanjo nilizopigwa enzi bado ni mtoto mchanga au chini ya miaka mitano. Chanjo ninayoikumbuka vizuri ni ile ya kichocho ambayo tulichomwa mashuleni nilikuwa shule ya msingi nimesahau darasa la ngapi ila ni Kati ya 2006-2008. Tena nakumbuka tulipikiwa wali shuleni.

Sasa chanjo ile iliniletea hali ya kuchanganyikiwa kichwani mpaka kufikia hatua kusahau muenendo wa siku na tarehe yaani zile siku mbili baada ya chanjo ungeniuliza ni juma ngapi mimi nisingeweza kusema yaani ni hali flani kama unakuwa huna akili kabisa ndo maana toka siku ile nikahisi mechanism ya chanjo kufanya kazi ni hatari kidogo sio Kama dawa.

Kwa hiyo, me chanjo ya corona hamnchanji bora niendelee kula masumu mengine ya pombe Kali n.k ila hii sumu mpya ya chanjo ya corona hapana Hapo pamoto sio pa kucheza nako.
 
Kachanjwe tu ndugu yangu, Mimi nilipigwa chanjo ya Ndui, surua, pepopunda n.k kichanjo hiki tu wakilete nimalizie
 
Hakuna chanjo ya kichocho mkuu. Itakua ulichanganya madesa.

Tuambie pia ulivyojisikia ulivyochomwa chanjo za Surua, polio, ndui, pepopunda, TB,Kuhara na chanjo ya homa ya ini.
 
Me mwenyewe naikumbuka hata sie tulipikiwa ubwabwa skuiyo skuli na tukachanjwa ila ilitudhoofisha almost watoto wote kama mie nlifika nyumbani hoi! Mpk leo sjasahau yan dish linakua kama limeyumba hivi
 
hzi chanjo zingine tuwe makini zinaleta upunga shauri zetu..
 
Back
Top Bottom