Chanzo cha Maji Mji wa Arusha chafungwa!

Ibrah

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2007
Posts
2,730
Reaction score
530
Chanzo muhimu cha maji kwa wakazi wa Manispaa ya Arusha kimefungwa. Chanzo hicho chenye uwezo wa kutoa lita za maji 110,000 ( Mita za ujazo 110) kwa saa kimefungwa baada ya maji yanayotoka hapo kuwa na madini mengi ambaye yanaathiri mifupa.

Source: ITV

Hata hivyo, maji hayo yamekuwa yakitumika kwa muda mrefu na wakazi wa Mji wa Arusha. Wakazi wengi wa Arusha huwa na meno yenye rangi ya brown ambayo ni moja ya athari za madini hayo. Athari nyingine za amdini yaliyo kwenye maji hayo ni kupinda kwa mifupa tatizo ambao baadhi ya wakazi wa Arusha huwa nalo na kusababisha wengine kufanyiwa upasuaji kuvunjwa miguu.

Miji wa Arusha, hasa sa maeneo ya Njiro kwa kawaida huwa na upungufu mkubwa wa maji na hufikia hata miezi mitatu bila kupata maji ya bomba; kufungwa kwa chanzo hicho kunaweza kusababisha wakazi wa baadhi ya maeneo hasa Njiro kutopata maji ya bomba kabisa.

Ajabu ni kuwa haikuelezwa hatyua mbadala za kukabiliana na upungufu utaojitokeza kwa kufungwa kwa chanzo hicho.
 
More information please. Chanzo hicho ni kipi maana vyanzo vyote vya Arusha vina hiyo floride
 
Sasa hawa ndio wamekumbwa na balaaaaa usipime Maji hakuna na mgao wa umeme kama kawa wanaupata
 

Nani kakwambia ni Ilboru mkuu hata sie wakupita twajua Ilboru ilipo na kule mlimani juuu kabisa huko nako kunaitwa ilboru ukipandishia njia ya sekei ambako me nadhania maji ndiko yatokeako na ninasikia kuna bomba laenda mpaka Monduli Jeshini sasa inamaaana hata huko Kambi ya jeshi maji nako hawapati??

au kukaaa kampala ndiko kumekupotezea mji wa Arusha mkuu

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…