Chapati za maji

rasai

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2013
Posts
230
Reaction score
341
Habari zenu wanajf, jaman naomba maarifa juu ya chapati za maji kuganda kwenye chuma, husababishwa na nini, na litokeapo nifanyeje ili chapati znazofata zitokee vizuri?
 
Jamani wengine hatujui hata pakuanzia hizo chapati za maji, tujulishane hatua muhimu wadau.
 
Chapati za maji sana sana huganda kwenye chuma ambacho hukaangiwa sana samaki....kuepuka kuganda saafisha vizur chuma chako then weka maji kiasi weka jikoni yachemke ili kuondoa uchumvi wa samaki uliogandia then mwaga kabla hujaweka mchanganyiko wa chapati za maji weka mafuta kiasi ili sizigandie....au unaweza kuweka chuma maalum kwa ajili ya chapayi tu ila mafuta muhimu weka kabla ya kukaanga kila chapati ya maji
 
Habari zenu wanajf, jaman naomba maarifa juu ya chapati za maji kuganda kwenye chuma, husababishwa na nini, na litokeapo nifanyeje ili chapati znazofata zitokee vizuri?

Hakikisha chuma ni kisafi. Katika mchnganyo wako tia na yai moja au mawili kutegemea na uwingi wa uji
 
dah, asante nmefaham ila chuma changu cha samaki ni tofauti na cha kupikia chapati na mara nyengine hili tatizo hunitokea. Kuhusu kueka mafuta, huwa sieki kabla ndo maana!! Umenisaidia sana shukran
 
Hakikisha chuma ni kisafi.
Katika mchnganyo wako tia na yai moja au mawili kutegemea na uwingi wa
uji

sawa nashkuru umenipa technique. Asante sana.
 
Pia usiweke maji mengi sana mchanganyiko wako hii atasababisha kukatika katika kwa chapati

ni kweli maji mi hukadiria, basi skunyengine huniponyoka yakawa yashazidi. Asante tena, na naomba utuletee recipe ya meatcake pliz
 
dah, asante nmefaham ila chuma changu cha samaki ni tofauti na cha kupikia chapati na mara nyengine hili tatizo hunitokea. Kuhusu kueka mafuta, huwa sieki kabla ndo maana!! Umenisaidia sana shukran

Karibu sana rasai
 
Last edited by a moderator:
Ukitumia pan ya non.stick chapati za maji unazisanif upendavyo. Unaweza kuzifanya zikawa nyepesi hata km karatasi
 
Ukitumia pan ya
non.stick chapati za maji unazisanif upendavyo. Unaweza kuzifanya zikawa
nyepesi hata km karatasi

eti! ,asante sana itabidi nitafte chuma cha hivyo, maana nlonacho ni cha muda mrefu sasa
 
Kuna frying pan nyeusi zinaitwa non stick. Hizo ukipikia chochote unaosha tu na dodoki na sabuni kinatakata. Moe nakaangia mboga, chapati, samaki, nyama! Tafuta hiyo.

Wakati wa kukoroga unga usitie maziwa, na utumie maji ya baridi kabisa. Unga uwe mzito kama alivyokwishasema farkhina
 
Last edited by a moderator:

Non stick zipo za kichina, tafuta brand ya Tefal hata kama hujuw kupika uta enjoy
 
Last edited by a moderator:
Kila kitu kipo cha kichina. Ni juu yake kuangalia anachomudu kununua. Frying pan yangu ina miaka maybe 4?
Non stick zipo za kichina, tafuta brand ya Tefal hata kama hujuw kupika uta enjoy
 
Ni kweli, tatizo jingine hasa kwa nchi zetu ni ubora wa frying pans

nyingi bado ni "sticky" if you get a non-sticky pans unaweza kukaanga chapati hata bila ya mafuta
 
Ni kweli, tatizo jingine hasa kwa nchi zetu ni ubora wa frying pans

nyingi bado ni "sticky" if you get a non-sticky pans unaweza kukaanga chapati hata bila ya mafuta

Yeah ni hivo mana hata pancake haiwekwi mafuta na inakua poa tu sema tu ndio hivo pan iwe non stick
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…