Chato: Wauguzi wahamishwa kituo madai kuomba wagonjwa rushwa 90,000/-

Chato: Wauguzi wahamishwa kituo madai kuomba wagonjwa rushwa 90,000/-

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
WAUGUZI wawili wa Kituo cha Afya cha Bwanga wilayani Chato mkoa wa Geita, wamehamishwa, kwa kutuhumiwa kuomba Sh. 90,000 kwa wagonjwa waliokuwa wamelazwa.

PINGU.jpg


Wanadaiwa kuomba fedha hizo kwa wagonjwa ili kuitumia kama nauli kwenda kufuata damu katika vituo vingine vya afya kutokana na kituo kukosa huduma ya damu.
Wauguzi wanaotuhumiwa ni George Makoye na Godfrey Willison, ambao wanadaiwa kuchukua fedha hizo kwa ndugu wa wagonjwa.

Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, Leonidas Felix, alisema baada ya kufanya uchunguzi walibaini kuwatoza wagonjwa Sh. 90,000 kama nauli waliyotumia kwenda kutafuta damu kwenye kituo kingine cha afya.

“Kufanya hivyo walikiuka kanuni na taratibu za utumishi wa umma, kwa sababu hata uongozi wa kituo hicho haukupewa taarifa,” alieleza Felix.
Alisema wauguzi hao wamerejesha fedha hizo kwa wagonjwa.

“Tayari wauguzi hao wamelipa faini na hawatashitakiwa tena kwa sababu kufanya hivyo ni sawa na kuwapa adhabu mara mbili,”alisema Felix.
“TAKUKURU tunaitaka mamlaka ya nidhamu iwahamishe wauguzi hao na iwapeleke katika vituo ambavyo havihusiki na damu salama,” alisema Felix.

“Watu wakibainika na makosa, huwa tuna mambo mawili; kuwapeleka mahakamani au kuwachukulia hatua za nidhamu, lengo ni kutoa fundisho kwao na kwa watumishi wengine wenye tabia kama zao.”

Felix, alisema wauguzi hao kwa sasa wameshamishiwa katika vituo vingine, ambavyo havina huduma ya damu salama.

NIPASHE
 
Mafanikio ya Samia ni habari mbaya sana kwa Lisu maana 2025 hana chake tena.

Ccm itaendelea kupeta.

Chadema wote wanashangilia ccm sasa hivi
 
Akili hizi sijui za wapi,

"Wamehamishiwa vituo ambavyo havijihisishi na masuala ya damu"

Swali langu, aliyewaambia Hawa rushwa wataomba kwa wanaoongezewa damu tu ni Nani, hawawezi kuuza madawa au kuomba rushwa kwa wagonjwa wengine......!
 
Ingekua kipindi cha mwendazake stori ingekua tofauti
 
Akili hizi sijui za wapi,

"Wamehamishiwa vituo ambavyo havijihisishi na masuala ya damu"

Swali langu, aliyewaambia Hawa rushwa wataomba kwa wanaoongezewa damu tu ni Nani, hawawezi kuuza madawa au kuomba rushwa kwa wagonjwa wengine......!
kaombe kwa wengine wakupige chini kwa uzoefu wa tabia mbaya[emoji16]
 
Nimesikia Chato nikashtuka paah nilifikiri....
 
WAUGUZI wawili wa Kituo cha Afya cha Bwanga wilayani Chato mkoa wa Geita, wamehamishwa, kwa kutuhumiwa kuomba Sh. 90,000 kwa wagonjwa waliokuwa wamelazwa.

PINGU.jpg


Wanadaiwa kuomba fedha hizo kwa wagonjwa ili kuitumia kama nauli kwenda kufuata damu katika vituo vingine vya afya kutokana na kituo kukosa huduma ya damu.
Wauguzi wanaotuhumiwa ni George Makoye na Godfrey Willison, ambao wanadaiwa kuchukua fedha hizo kwa ndugu wa wagonjwa.

Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, Leonidas Felix, alisema baada ya kufanya uchunguzi walibaini kuwatoza wagonjwa Sh. 90,000 kama nauli waliyotumia kwenda kutafuta damu kwenye kituo kingine cha afya.

“Kufanya hivyo walikiuka kanuni na taratibu za utumishi wa umma, kwa sababu hata uongozi wa kituo hicho haukupewa taarifa,” alieleza Felix.
Alisema wauguzi hao wamerejesha fedha hizo kwa wagonjwa.

“Tayari wauguzi hao wamelipa faini na hawatashitakiwa tena kwa sababu kufanya hivyo ni sawa na kuwapa adhabu mara mbili,”alisema Felix.
“TAKUKURU tunaitaka mamlaka ya nidhamu iwahamishe wauguzi hao na iwapeleke katika vituo ambavyo havihusiki na damu salama,” alisema Felix.

“Watu wakibainika na makosa, huwa tuna mambo mawili; kuwapeleka mahakamani au kuwachukulia hatua za nidhamu, lengo ni kutoa fundisho kwao na kwa watumishi wengine wenye tabia kama zao.”

Felix, alisema wauguzi hao kwa sasa wameshamishiwa katika vituo vingine, ambavyo havina huduma ya damu salama.

NIPASHE
Ifahamike pia ONYO pia ni adhabu tosha, sio lazima kila kosa basi lazima wapelekwe mahakamani, kama tukisema kila kosa lazima wapelekwe mahakamani basi magereza zetu zitajaa.
wakati mwengine lazima vyombo vyetu vitumie tu busara.
kuteleza sio kuanguka!
hakuna malaika kila mmoja anakosea japo kwa bahati mbaya.
sio vibaya wakapewa nafasi nyingine ili wajirekebishe.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
WAUGUZI wawili wa Kituo cha Afya cha Bwanga wilayani Chato mkoa wa Geita, wamehamishwa, kwa kutuhumiwa kuomba Sh. 90,000 kwa wagonjwa waliokuwa wamelazwa.

PINGU.jpg


Wanadaiwa kuomba fedha hizo kwa wagonjwa ili kuitumia kama nauli kwenda kufuata damu katika vituo vingine vya afya kutokana na kituo kukosa huduma ya damu.
Wauguzi wanaotuhumiwa ni George Makoye na Godfrey Willison, ambao wanadaiwa kuchukua fedha hizo kwa ndugu wa wagonjwa.

Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Geita, Leonidas Felix, alisema baada ya kufanya uchunguzi walibaini kuwatoza wagonjwa Sh. 90,000 kama nauli waliyotumia kwenda kutafuta damu kwenye kituo kingine cha afya.

“Kufanya hivyo walikiuka kanuni na taratibu za utumishi wa umma, kwa sababu hata uongozi wa kituo hicho haukupewa taarifa,” alieleza Felix.
Alisema wauguzi hao wamerejesha fedha hizo kwa wagonjwa.

“Tayari wauguzi hao wamelipa faini na hawatashitakiwa tena kwa sababu kufanya hivyo ni sawa na kuwapa adhabu mara mbili,”alisema Felix.
“TAKUKURU tunaitaka mamlaka ya nidhamu iwahamishe wauguzi hao na iwapeleke katika vituo ambavyo havihusiki na damu salama,” alisema Felix.

“Watu wakibainika na makosa, huwa tuna mambo mawili; kuwapeleka mahakamani au kuwachukulia hatua za nidhamu, lengo ni kutoa fundisho kwao na kwa watumishi wengine wenye tabia kama zao.”

Felix, alisema wauguzi hao kwa sasa wameshamishiwa katika vituo vingine, ambavyo havina huduma ya damu salama.

NIPASHE
Wahamishiwa sehemu nyingine, inamaana Chato hamna TAKUKURU wakuwafungulia kesi ya uhujumu uchumi?
 
Back
Top Bottom