Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Waziri Aweso amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Eng Mwajuma Waziri kumuweka pembeni katika nafasi ya uongozi Bwana Misango na ametuma salamu kwa watendaji wote wa sekta ya Maji nchini kuzingatia Nidhamu katika kazi kwani sekta hii ji sekta ya huduma kwa wananchi.
Katika hatua nyingine Waziri Aweso amemteua Eng. Isaack Joseph Mgeni kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji ya Chato ambapo awali a Eng. Isaack aliekua Meneja wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Mamlaka ya Maji Geita (GEUWASA)
Pia soma: Shida kubwa ya maji Chato. Waziri Kalemani hajali kitu, anachojali ni kusambaza taa za mitaani
Waziri Aweso amefanya maamuzi haya alipotembelea Mradi wa Maji wa Miji28 wa Chato unaogharimu kiasi cha Bilion 38 baada ya Maelekezo ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa Dkt Emmanuel Nchimbi na kusisitiza mradi huu unahitaji uangalizi wa karibu.
=====
Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso ametembelea na kukagua Mradi wa Miji 28 Chato mkoani Geita.
Mradi huu una Thamani Bil 38 na unatekelezwa na Mkandarasi Afcon wa India.
Katika ziara hii Waziri Aweso ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri.
Aidha Waziri Aweso ameelekeza kazi ya utekelezaji wa Mradi huu ifanyike usiku na mchana na kwa kasi kwani ni Mradi tegemeo kwa wananchi wa Chato na Mkoa wa Geita kwa ujumla zaidi akisisitiza usimamizi na ufuatilaji toka kwa watendaji wa Wizara ya Maji waliopewa wajibu huo.
Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewahakikishia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwamba wataalamu wa Wizara ya Maji wataifanya kazi ya utekelezaji wa Mradi huu kwa weledi, wakati na thamani ya fedha.