Chato: Waziri Aweso asikitishwa na Mkurugenzi mtovu wa nidhamu, amuweka pembeni

Chato: Waziri Aweso asikitishwa na Mkurugenzi mtovu wa nidhamu, amuweka pembeni

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso amesikitishwa na tabia ya isiyo njema ya kinidhamu ya ulevi ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira ya Chato Eng.Mari Misango ambaye amefika kwenye mkutano wake leo akiwa katika hali ya ulevi na kwa ujumla akiwa ameshindwa kutekeleza majukumu yake vyema kutokana na kukithiri kwa tabia hii na kulalamikiwa na watumishi anaowaongoza katika Mamlaka ya Maji Chato.

Waziri Aweso amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Eng Mwajuma Waziri kumuweka pembeni katika nafasi ya uongozi Bwana Misango na ametuma salamu kwa watendaji wote wa sekta ya Maji nchini kuzingatia Nidhamu katika kazi kwani sekta hii ji sekta ya huduma kwa wananchi.

Katika hatua nyingine Waziri Aweso amemteua Eng. Isaack Joseph Mgeni kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji ya Chato ambapo awali a Eng. Isaack aliekua Meneja wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Mamlaka ya Maji Geita (GEUWASA)

Pia soma: Shida kubwa ya maji Chato. Waziri Kalemani hajali kitu, anachojali ni kusambaza taa za mitaani

Waziri Aweso amefanya maamuzi haya alipotembelea Mradi wa Maji wa Miji28 wa Chato unaogharimu kiasi cha Bilion 38 baada ya Maelekezo ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Taifa Dkt Emmanuel Nchimbi na kusisitiza mradi huu unahitaji uangalizi wa karibu.

IMG-20240909-WA0036.jpg
Mhandisi Isaack Joseph Mgeni alieteuliwa na Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Chato.

=====

Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso ametembelea na kukagua Mradi wa Miji 28 Chato mkoani Geita.
Mradi huu una Thamani Bil 38 na unatekelezwa na Mkandarasi Afcon wa India.
Katika ziara hii Waziri Aweso ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri.

Aidha Waziri Aweso ameelekeza kazi ya utekelezaji wa Mradi huu ifanyike usiku na mchana na kwa kasi kwani ni Mradi tegemeo kwa wananchi wa Chato na Mkoa wa Geita kwa ujumla zaidi akisisitiza usimamizi na ufuatilaji toka kwa watendaji wa Wizara ya Maji waliopewa wajibu huo.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Mwajuma Waziri amewahakikishia wananchi waliojitokeza kwa wingi kwamba wataalamu wa Wizara ya Maji wataifanya kazi ya utekelezaji wa Mradi huu kwa weledi, wakati na thamani ya fedha.
 
Wakati mwingine watu wana stress za kifamilia
 
Huyu aweso hapa dar Huwa hajui kuwa Kuna maeneo kama msakuzi wilaya ya ubungo hakuna maji Toka tupate uhuru?Huko mwingine anajifanya mchapa kazi
 
Back
Top Bottom