Chelsea kuendelea kumlipa Lampard Pauni 75,000 kwa wiki

Chelsea kuendelea kumlipa Lampard Pauni 75,000 kwa wiki

Shadida Salum

Journalist at JamiiForums
Joined
Sep 11, 2020
Posts
69
Reaction score
105
20210215_134120.jpg

Lampard alipotimuliwa na Chelsea mwezi uliopita klabu haikulipa mkataba wake uliobaki baada ya mabadiliko ya sera ambayo yalikuja baada ya kulazimika kutoa pesa nyingi wakati walimpomuondoa Jose Mourinho

Badala yake wameweka mshahara wake wa Pauni 75,000 kwa wiki kwenye muswada wa mshahara - na makubaliano ni kwamba ataendelea kulipwa hadi Julai ikiwa tu hatochukua kazi kwenye timu nyingine.

Na hiyo inamwacha Lampard katika nafasi ambapo ofa yoyote ya ajira inayokuja inaweza kumgharimu pesa nyingi.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 42 anafahamika kuwa anafurahi kuchukua mapumziko kwa kipindi kifupi kufuatia kutimuliwa, baada ya kuwa na misimu mitatu yenye shinikizo kubwa tangu kuwa meneja huko Derby County.

Ingawa Lampard alikuwa na uwezo kuiendea ofa ya kukinoa kikosi cha Bournemouth lakini hakufanya hivyo kwa kuwa kwa sasa anatumia muda wake na familia yake.

Lakini pia ni ukweli kwamba kama angechukua ofa hiyo ingemaanisha mara moja pesa ambazo Chelsea inaendelea kumlipa zingekoma, ambayo ingemgharimu chini ya pauni milioni 2.
 
Huyu lampard ana roho mbaya. Aliyekuwa mama mkwe wake alimlaani baada ya kumfukuza kwenye nyumba ya kifahari kama mbwa aliyomzawadia aishi kisa kukosana na binti yake. Ndio maana mambo yake hayaendi vizuri.
 
Back
Top Bottom