Chelsea ,Man city kipimo kikibwa kwa Matteo Guendouzi

Chelsea ,Man city kipimo kikibwa kwa Matteo Guendouzi

Dkileo

Member
Joined
May 23, 2017
Posts
51
Reaction score
46
Katika mechi mbili za mwanzo za msimu huu wa 2018/2019 za Arsenal kuna kijana wa Unai Emery alinivutia sana…Anaitwa Matteo Guendouzi…Kijana mdogo wa miaka 19 kutoka timu ya league 2 ya Lorient huko France

Wakati nilipo mwangalia pre season niliamini Matteo hatoweza kuingia moja kwa katika kikosi cha Arsenal mapema hivi..Niliamini mwalimu Unai angeweza kungojea au kumpa dakika chache katika mechi hizi za mwanzoni lakini imekuwa tofauti sana

Matteo alicheza dakika zote 90 dhidi ya Man city na Chelsea…Alicheza vizuri sana …Matteo anapiga pasi na anakaba vizuri..Anaisukuma timu mbele vizuri sana..

Katika mechi hizi mbili alionekana kuchoka sana second half…Alicheza dhidi ya safu imara sana za viungo..Fernandinho,Gundogan na Benardo Silva halafu Jorginho,Barkley na Kante..Hawa ni viungo wazoefu sana…Hivyo walikuwa kipimo kikubwa sana kwa Matteo



Matteo anahitaji kupewa muda wa kuzoea ligi ya England…Kutoka league 2 hadi premier league na kuingia moja kwa moja katika kikosi cha Arsenal si jambo dogo..Anahitaji kuzoea speed ya EPL

Nafikiri baada ya mechi 7 mapaka 10 tunaweza kumshuhudia Matteo akiwa katika ubora kabisa…Dhahabu mpya ndani ya arsenal mpya ya Unai Emery..

Ni suala la muda tuu
 
Back
Top Bottom