Chelsea ni timu ya kishenzi sana.

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Kama uliamua kushabikia Chelsea,ni bora ubadili maamuzi mapema kwani ni moja ya timu za kishenzi sana na hawajali sana maslahi ya washabiki.

Nina sema hivi kwa kuwa wamekuwa wakiuza wachezaji wazuri wakati bado wanahitajika sana katika timu.

Unakumbuka akina Matic,Mo Salah,Kelvin de Bruyne,na wengine wengi bora kabisa.
Sasa hivi eti Willian ameambiwa aondoke,sasa tena Ngolo Nkante eti pia wanaongea na Inter Milan ili ikibidi wamuuze!
Hawa watu wanataka nini?Wameniudhi sana kwa hizi Sera za kishenzi
 
Chelsea ni timu iliyotulia na kila mwaka inamaliza top 5,inauza wachezaji na kununua wachezaji sasa nini kingine unahitaji kwenye usajili
 
Biashara ya mpira huijui.
Sipendi ngole Kante auzwe lakini watu wanaangalia thamani yake miaka mitatu ijayo. Umri umekwenda. Umri ukishakwenda injury nazo zinakuwa rafiki ya mchezaji. Muangalie sasahivi kante majeruhi yanavyomuandama. Kwa mchezaji mwenye umri miaka 30+ kama bei nzuri inafikiwa na ulimpata kwa bei poa why usimuuze?
Willian nae ni kama kiwango kinaelekea ukingoni. Ndio maana unaona vijana ambao wanakuja poa wanasajiliwa na wengine wapo. Odoi, ziyech & purisic. Purisic kasha prove. Odoi ana nafasi ya kuprove bado bwana mdogo sana. Ziyech anafajamika. Kati pale kuna yule dogo grimour, Mount etc.
 
Asa mkuu nawe nakuona hauko sawa suala la kante kuondoka hizo no rumors tu na hakuna ukweli wowote yeye mwenyewe kante alishasema haondoki na Chelsea haina mpango wa kumuuza.

Suala la Willian, Chelsea wanataka kumpa miaka miwili lakini yeye anataka miaka mitatu, lakini siku zinavyoenda uwezekano wa Willian kupewa huo mkataba upo maana, na week kadhaa zilizopita kulikuwa na mazungumzo Kati Willian na Chelsea.
Suala la kumuuza salah, Kevin kama wewe ni mtu wa soka hauwezi kulaumu hata kidogo, kipindi hicho akina salah na Kevin viwango vyao vilikuwa chini Sana ndio maana walitolewa kwa mkopo na baadae kuuzwa jumla. In fact Kila mchezaji ana muda wa kufikia peak yake kisoka, Je unadhani Chelsea ilipaswa kuwabakisha kikosini kwa kipindi hicho wakiwa na viwango vyao vya chini!?, Jibu ni hapana maana ni lazima ifanye maingizo mapya ya wachezaji mkuu.
Mwisho kama unaona Chelsea ni timu ya kishenzi then hama mkuu, kwanza utasemaje Chelsea ni timu ya kishenzi ambapo Kila msimu Ina guarantee ya kuchukua kombe uh!

Basi hamia arsenal, man United au Spurs timu ambazo hazina guarantee ya kuchukua kombe lolote ndani ya msimu.
 
Wewe unatarajia kubeba kombe gani? πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…