Asa mkuu nawe nakuona hauko sawa suala la kante kuondoka hizo no rumors tu na hakuna ukweli wowote yeye mwenyewe kante alishasema haondoki na Chelsea haina mpango wa kumuuza.
Suala la Willian, Chelsea wanataka kumpa miaka miwili lakini yeye anataka miaka mitatu, lakini siku zinavyoenda uwezekano wa Willian kupewa huo mkataba upo maana, na week kadhaa zilizopita kulikuwa na mazungumzo Kati Willian na Chelsea.
Suala la kumuuza salah, Kevin kama wewe ni mtu wa soka hauwezi kulaumu hata kidogo, kipindi hicho akina salah na Kevin viwango vyao vilikuwa chini Sana ndio maana walitolewa kwa mkopo na baadae kuuzwa jumla. In fact Kila mchezaji ana muda wa kufikia peak yake kisoka, Je unadhani Chelsea ilipaswa kuwabakisha kikosini kwa kipindi hicho wakiwa na viwango vyao vya chini!?, Jibu ni hapana maana ni lazima ifanye maingizo mapya ya wachezaji mkuu.
Mwisho kama unaona Chelsea ni timu ya kishenzi then hama mkuu, kwanza utasemaje Chelsea ni timu ya kishenzi ambapo Kila msimu Ina guarantee ya kuchukua kombe uh!
Basi hamia arsenal, man United au Spurs timu ambazo hazina guarantee ya kuchukua kombe lolote ndani ya msimu.