Chimbuko la kabila la wairaqw

Chimbuko la kabila la wairaqw

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,743
Reaction score
25,564
Kitaaluma. Ukisoma peopling of East Africa utajua kuwa sisi ni Cushite. Ukisoma Itandala (1997) katika kitabu chake East Africa and its Invaders anasema, Afrika kuna makabila 3. Negros, Hamites and Bushmen. Sisi Cushite tumezaliwa baada ya kuwaoa Hamite. Asili yetu ni South East Asia (Mesopotamia Iraq.). Katika kutafuta unafuu wa kiuchumi ndo imetufanya kuwa Mbulu. Tulipitia Ethiopia, Egypt na serengeti mpaka mbulu. Kuacha Ngorongoro siwezi kusema kitu kwasababu walikuwa wanappita tu.

Reference Charles G Seligman (1930) He is colonial anthropologists. Ukisoma GW Huntingford (1963) colonial anthropologist naye anamawazo yanayofanana. Kutoka University of Dar es salaam Itanda (1997) naye kaandika. Jana Sutton (1969). Cushite waliingia East Africa 2000BC (Before common error) tukitokea southern Ethiopia Highlands. Wakaenda kuishi wakaenda kuishi katika nyanda za juu mpaka wa bonde la ufa la magharibi ya kenya na kaskazini mwa Tanzania. Tunaposema Cushite tunamaanisha watu wenye asili moja yaani, Iraqw, Goroa, Alawa, Burungi, Ngovia na Qwadza. Wote wapo Wilaya ya Mbulu, Babati, Kondoa na Dodoma.

Kiutafiti. Wairaqw ni miongoni mwa rnakabila yanayoishi katika Mkoa wa Manyara Wilaya za Mbulu, Babati, Hanang na Mkoa wa Arusha Wiiaya ya Karatu. Kwa asili Wairaqw walitokea Mesopotamia Iraq. Uhamiaji wao ulianza katika karne ya 4 - 6 baada ya kuzaliwa kwa Kristo. Asili ya kabila la Wairaqw Kwa asili Wairaqw walitokea Mesopotamia Iraq. Uhamiaji wao ulianza katika karne ya 4 - 6 baada ya kuzaliwa kwa Kristo.

Wairaqw ni jamii ya Wakushi ambao Walivuka bahari ya Sham kwa mashua na kutua Ethiopia, waliishi hapo kwa muda kutokana na vita vya mara kwa mara, waiiendelea kuhama kuelekea kusini magharibi waiipitia bonde la ufa kando ya ziwa Victoria. Katika kuhama hama huko na kukaa mahali kwa muda vita vikaanza wakakimbilia na waiiendelea hivyo hivyo kupitia njia ya kati kupitia Singida Iramba hadi mpakani mwa Dodoma na Iringa. Kwa upande wa kusini kuiikuwa na mapambano ya Wahehe, Wangoni na Wazimba wakarejea kuelekea kaskazini hadi sehemu ya Kondoa mahali panapoitwa Guser Tuwalay. Waliishi hapo wakiwa wafugaji na kilimo kidogo.

Ndipo walipoanza mapambano kati yao na Wabarbaig. Waliposhindwa vita walikirnbilia karibu na mlima Hanang. Wakagawanyika wengine wakaelekea, Gallapo (Tsea Daaw). Hawa waliitwa Wagorowa na Wairaqw walipandisha mlima Dabil hadi Guser, Gangaru ambapo walifanya maskani. Baada ya muda Kiongozi wao aiiyeitwa Haymu Now wa ukoo wa Haytipe aliwaongoza hadi Nou na walifanya rnaskani yao katika maeneo ya Mama Isara. Aidha inasemakana kuwa eneo lote la Mama Isara lilikuwa ni ziwa wakati ule, hivyo Haymu na watu wake walifanya maskani katika maeneo ya milima.

Kiongozi huyo alikuwa na mtumishi wake aiiyeitwa MOYA. Hi kuongeza maeneo ya kilimo kiongozi huyo alitumia uganga wake kuhamisha ziwa katika eneo la Mama Isara kwa kumwagiza mtumishi wake kurusha mshale katikati ya ziwa hilo. mtumishi alipofanya hivyo ziwa lilihama pamoja naye hadi katika bonde la ufa ambalo linajulikana kwa jina la ziwa manyara kwa sasa na Kiiraqw hujulikana kama " Tlawta Moya". Baada ya ziwa kuhama kiongozi huyo aliendelea kuishi hapo na watu wake na kuendelea kutawanyika katika maeneo ya Muray, Kuta, Amoa, Kainam, Suum, Datlaa, Tsaayo Wilaya ya Mbulu.

Baadaye Wairaqw wakatawanyika taratibu sehemu za Karatu, Babati na Hanang kama makao makuu yao mpaka leo. Baadhi ya miia na desturi za Wairaqw zinafanana na za Wayahudi kama matumizi ya kondoo katika jamii.
 
Asante kwa Bandiko Mkuu.

Wairaqw ni moja ya makabila yenye mabinti wazuri Tanzania.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Historia ya makabila na asili zao haieleweki.mfano kama historia ya kabila la warangi haieleweki hata pale kondoa walipo siyo sehemu ya asili yao kwa maana hakuna hata sehem au hata kijiji kimoja chenye jina la kirangi majina ya maeneo ya pale yote ni ya makabila ya jamii ya wambulu ambayo ni kama wafyomi waburunge wagorowa waalawa au wasi na wasandawe sasa hao warangi wametokea wapi maana hata kwenye kufanya matambiko kama eneo linatatizo lazima wawaite wenyeji wao mfano waalawa ndio watalifanya hilo tambiko
 
Eneo la manyara na kondoa ndio maeneo ambayo hawana makabila ya kibantu
mfano wairaqwi
qwadza
ngovia
gorowa
alawa
burunge
hadzabe
sandawe
masai
barabaiq au mang'ati
labda warangi pekee ndio lugha yao inamchanganyiko wa kikushi na kibantu
 
Historia ya makabila na asili zao haieleweki.mfano kama historia ya kabila la warangi haieleweki hata pale kondoa walipo siyo sehemu ya asili yao kwa maana hakuna hata sehem au hata kijiji kimoja chenye jina la kirangi majina ya maeneo ya pale yote ni ya makabila ya jamii ya wambulu ambayo ni kama wafyomi waburunge wagorowa waalawa au wasi na wasandawe sasa hao warangi wametokea wapi maana hata kwenye kufanya matambiko kama eneo linatatizo lazima wawaite wenyeji wao mfano waalawa ndio watalifanya hilo tambiko
Kuna kabila linaitwa wambulu?
 
Asante kwa Bandiko Mkuu.

Wairaqw ni moja ya makabila yenye mabinti wazuri Tanzania.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
achana na hoa wairaqwi au warangi
kuna hao watu wanaitwa wasi au waalawa sidhan kama nchi hii kuna watu wa kuwafikia kwa uzuri
 
mbulu ni eneo walipo wairaqw wengi,wairaq watu wamezoea kuwaita wambulu.
unataka kusemaje kwani au huelew nin ufafanuliwe .
Nimeuliza swali umetoa jibu kuwa mbulu ni eneo si kabila.
 
Back
Top Bottom