Chipsi masala

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363


Chipsi ni chakula kinachopendwa na watu wa rika zote.Ni moja ya vyakula maarufu sana Duniani.

Chipsi hupikwa na kuliwa katika namna mbambali,kwa kawaida huliwa na vyakula vyenye asili ya protini

kama nyama na mayai,Hata ivyo unaweza kula chipsi na mboga za majani.

Naamini wengi mmewahi sikia pishi la Chipsi masala,na pengine mmekula mara nyingi na mnafahamu

namna ya kuliandaa.Kawaida pishi hili huchanganya chipsi na mboga za majani katika kikaango na kuongezwa vionjo vya viungo mbalimbali.



Hapa jikoni napenda kufanya mambo tofauti ,Ubunifu jadi yangu.


Mahitaji.


Moja


  • Mafuta ya majarini kwa kiasi upendacho (nashauri Blue Band)
  • Vitunguu maji 3 vikubwa-kata kwa urefu
  • Karoti 3 kubwa–kata vipande virefu Vyembamba
  • Hoho 3 kubwa -kata vipande virefu vyembamba
  • Vitunguu saumu vijiko 2 vya chakula-kata vipande vyembamba
  • Carry powder kijiko 1 cha chai
  • Chips masala vijiko 4 vya chai
  • Pilipili manga ½ kijiko cha chai

Mbili


  • Nyanya ya kopo-vijiko 3 vya chakula
  • Giligiliani 1/2 kikombe –kata vipande vikubwa
  • Sukari kijiji 1 cha chai
  • Chumvi Robo kijiko cha chai

Tatu


  • Maji nusu kikombe

Nne


  • Kaanga chipsi

Njia


1.Katika sufuria,weka mahitaji yote ya namba moja.Tanguliza mafuta chini.Kaanga kwa moto mdogo adi karoti isinyae.


  • Ukitumia moto mkali,viungo vitaungua kabla mboga hazijaiva

2.Ongeza viungo vyote vya namba mbili.kaanga pamoja uku ukichanganya adi uone nyanya na mboga vimeshikana na kua kitu kimoja


3.Ongeza maji nusu kikombe,changanya kisha acha vichemke kwa muda kidogo ili maji yapungue na kuacha mboga zikiwa na rojo zito


4.Kaanga chipsi


5.Weka chipsi kwenye sahani kisha weka mboga za chipsi masala juu yake.Tayari kwa kula



Maelezo ya ziada


Unaweza kutenga chaakula hiki kwa namna yoyote uipendayo.Hapa jikoni Niliamua kuweka juu ya jani la

sukuma wiki na kupamba na Tomato sosi.


Ukipenda kutenge hivyo.chukua jani la sukuma wiki,osha vizuri.Chemsha maji ya moto yanayotokota

kwenye sufuria pana, tumbukiza jani hilo kwa sekunde 25,kisha toa na ulitumbukize kwenye maji ya baridi

yenye barafu kwa sekunde 25.Toa kwenye maji,acha likauke au kausha kwa kutumia karatasi za

jikoni.Adi
hapo waweza litumia kutenga chakula.


  • Lengo la kutumia sufuria pana ni kuhakikisha jani halijikunji

Kama familia ina watoto wadogodo,ni vyema ukakata mboga vipande vidogo,twanga au ponda vitunguu saumu na epuka kutumia pilipili manga.
 
Nzuri sana hii...Nimepigwa marfuku kula viepe ila hii ntaanda alafu nijifiche uvunguni nijilie mie MziziMkavu all recipes uloweka leo maashaallah superb

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
zimewaumiza sana watoto wa kike hizo..! mimba za utotoni nyingi zimechangiwa na utamu wa chipisi
 
chipsi ni noma asa chipsi kuku chipis yai :smile-big:
 
Last edited by a moderator:
Hii mie napenda zaidi chips zikiwa kiporo from friji naipasha kwa microwave then napika mchanganyiko namwagia juu yake mweee
 
Hii mie napenda zaidi chips zikiwa kiporo from friji naipasha kwa microwave then napika mchanganyiko namwagia juu yake mweee

amu ila tegemea vijambo na mashuzi kibwena
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…