Chirwa, Ngoma wanaisaidia Azam?

Siku zote tunasema mwisho wa ubaya ni aibu,kina Ngoma na Chirwa wanavuna dhambi waliyoipanda Yanga,waliondoka kwa mbwembwe sana na Ngoma akajifanya bonge na mchezaji na kudeka deka mpaka wakatukosesha Ubingwa msimu uliopita lakini kwa sasa hawana lolote,ni zaidi ya hovyo,hawaisaidii Azam kwa lolote zaidi ya kuruka ruka uwanjani kama ndege john.

Unaposema Azm ni mabingwa wa kombe la Mapinduzi,litawasaidia kushiriki michuano gani ya Kimataifa Mwakani?,nani alisifiwa kwa kuibuka Bingwa wa Bonanza?,
 
Unaweza kusema Azam kwa msimu huu wamepotea kuwania ubingwa sawa.. Ila kuhusu kuwakilisha nchi kimataifa inawezekana kwani bado wamo FA CUP ambayo Simba ametolewa na ukumbuke Yanga anamzid Azam point 9/10.. LIGI BADO.
 
Jina na hamasa labda ndio vinaiangusha Azam. Timu inahela, haina migogoro lakini bado haizipi changamoto timu kongwe hizi, ndani ya misimu mitano iliyopita Azam angalau ingechukua ligi Mara 2 , shida wachezaji wanapovaa jezi za Azam hawazichukulii uzito kama wakivaa za Simba au Yanga, mfano wakina Manula,Bocco, Nyoni, Kapombe, wameenda Simba tuu ligi wamechukua na Makundi Africka wamefika, najiuliza walishindwa nini wakiwa na jezi za Azam??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Chirwa, Ngoma wamewatimua makocha Azam. Shida ya Azam wanafanya mambo yao Kwa kuungana na Simba kuikomoa Yanga. Kitendo cha Azam kumchukua Plujim, Mwambusi, Ngoma na Chirwa ni sehemu ya kuiunga mkono Simba kwenye ushindani wake na Yanga.

Azam ikiendelea hivi na ushabiki wa Simba na Yanga haitafika kokote mbali
 
Hapo kuna kitu aise, isijekuwa wachezaji wanafanya makusudi wafungwe, na hasa wanapokutana na hizi timu mbili simba na yanga, Bakhresa/Azam awe makini sana kama sio wachezaji basi viongozi wa timu.
 

Huenda wanafanya makusudi tu, wanaona bora ichukue ubingwa yanga au simba tim ambazo washawahi kuchezea/kusajiliwa hapo nyuma kuliko Azam.

Namshauri Azam asajili wachezaji kutoka nje, aachane na wazawa wenye damu na usimba na uyanga. Wanakula pesa za bure tu
 

Asajili wachezaji kutoka nje, aachane na hawa waliowahi kucheza tim za yanga na simba hawafai.
 
Kwani Chirwa, Ngoma, kutinyu, abarora, nkangwa, nk ni watanzania? Mbona hawafanyi kweli?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…