mwanyaluke
JF-Expert Member
- Jan 22, 2015
- 704
- 2,435
Kama uko njema saana...tafuta Pozzolana Cement( cement wanayojengea madaraja sehemu za maji chumvi).....hapo hata aje fungus gani hapenyi.Nimetumia materia zote tajwa hapo juu ,linapokuja swala la ukuta kuvamiwa na fungus naona kama chokaa Ina afadhali , ila suala la ukuta kupendeza chokaa inashika nafasi ya mwisho unless upate fundi kweli , wewe umeonaje
Mi sijaona hujatuwekea pichaNimetumia materia zote tajwa hapo juu ,linapokuja swala la ukuta kuvamiwa na fungus naona kama chokaa Ina afadhali , ila suala la ukuta kupendeza chokaa inashika nafasi ya mwisho unless upate fundi kweli , wewe umeonaje
Inasimamia bei gani hiyo madukani? Na inafungashwa kwa ujazo wa kilo ngapi kwa mfuko mmoja?Kama uko njema saana...tafuta Pozzolana Cement( cement wanayojengea madaraja sehemu za maji chumvi).....hapo hata aje fungus gani hapenyi.
Ngoja nimuite mzee mwenzangu Fundi Mchundo aweke neno.Nimetumia materia zote tajwa hapo juu ,linapokuja swala la ukuta kuvamiwa na fungus naona kama chokaa Ina afadhali , ila suala la ukuta kupendeza chokaa inashika nafasi ya mwisho unless upate fundi kweli , wewe umeonaje
Nimelichukua hili Fundi Mchundo. Ubarikiwe na Asante kwa Ufafanuzi kwetu tunaojua ukiweka Tiles umemaliza ππππππππFungus inatokana na unyevunyevu ndani ya ukuta na kushindwa kutoka nje kwa urahisi. Huu unyevunyevu unaweza kuwa unatoka na maji kupanda ndani ya ukuta bila kizuizi kama hukuweka damp proof course na membrane.
Au unyevunyevu unaotokana na sehemu tunazoogea. Nyumbani hatuna kawaida ya ku waterproof mabafu yetu kwa kuamini kuwa tiles zinatosha. Tiles hazitoshi kwa sababu maji yanapenya kwenye maungio. Dawa ni kuweka waterproof membrane kwenye sakafu na kuta za bafu kabla ya kuweka tiles.
Kwa kuta za nje, badala ya kutumia rangi tulizozea tumia "masonry paint". Masonry paint inazuia maji kuingia wakati inaruhusu ukuta kupumua na hivyo unyevunyevu wowote unatoka nje ya kuta na unadondoka kama punje punje za maji.
Rangi ya weatherguard kwa nje inasaidia kwa kiasi fulani kuzuia fungus. Wash n wear haimudu hali ya nje.
Chokaa inaruhusu ukuta kupumua lakini kwa sababu sio waterproof itakubidi kuipaka mara kwa mara.
Kitu muhimu ni kuhakikisha kuwa nyumba yako haipenyezi maji. Aidha, hakikisha mabafu yanapata hewa fresh ya kutosha. Hakikisha paa halivuji.
Kitu kingine cha kuzingatia ni maintenance. Ukiona fungus zinajitokeza, ziondoe kwa kutumia dawa itakayoiua. Kagua kuta zako kila baada ya miaka mitano. Rangi zina muda wa kuwa effective.
Ongea na dealer wa rangi kwa ushauri zaidi. Au nenda hata kiwandani kwao ili upate ushauri.
Nakutakia kila la heri.
Amandla...
Masanja
Wengi hatuweki. Sika wana products nzuri za kufanyia waterproofing. Sika Cemflex ni nzuri kwa bafuni. Kama tayari umeishaweka tiles basi tumia Sika Sanisil silicone sealant kwenye joints. Ila mpigia simu mtaalamu wao kwa ushauri zaidi. Nimekushauri Sika kwa sababu vitu vingi hapa nyumbani ni fake. Kwa vile hawa jamaa wana duka lao unaweza kwenda kununua kwa urahisi na uhakika.Nimelichukua hili Fundi Mchundo. Ubarikiwe na Asante kwa Ufafanuzi kwetu tunaojua ukiweka Tiles umemaliza ππππππππ
Ki ukweli kwa sasa sifahamu, nna kamuda asee kujihusisha na malighafi za ujenzi.Inasimamia bei gani hiyo madukani? Na inafungashwa kwa ujazo wa kilo ngapi kwa mfuko mmoja?
Sent using Jamii Forums mobile app