Chombezo………….BAO TATU ZA MGENI!
Umri…………………..18+
Sehemu ya 2
Ngurumo za radi zilisikika ishara ya kwamba mvua kubwa itanyesha muda si mrefu,mpaka wakati huo anilikuwa sijapata sehemu ya kulala!
Walianza kufunga hoteli huku wakiwa wanaongea lugha ambayo sikuielewa,ila kabla hawajafunga kabisa kuna mzee alikuja kutafuta chakula!
“Vipi huo ukoko haujaungua kama wa jana?”
“Leo uko vizuri babu!”
“Niletee si bei yetu ile?”
“Ndiyo babu!”
Yule mzee ilionekana ndiyo kawaida yake kuja kula ukoko kila siku wale wadada wakimaliza kuuza chakula!
Alikabidhiwa lile sufuria akaanza kulifakamia jungu lilikuwa na makoko mengi sana!
“Kijana karibu!”
“Ahsante mzee mimi tayari!”
Ulipita ukimywa kilichosikika ni sauti ya yule mzee akitafuna tu ukoko wake,baada ya nusu saa jungu lilikuwa jeupe kabisa!
Wale wadada walikuwa wamemaliza kuosha vyombo na kufunga,wakati yule mzee amemaliza akalipa anataka kuondoka mi bado nilikuwa pale,kitendo kile kiliwachanganya wale wadada ambao walianza kunifikiria labda nataka kuwatongoza,ila kilichowapa maswali ni begi nililokuwa nimebeba!
“Kaka si tunataka kufunga!”
Kauli ile ilikuwa kama msumari iliuchoma moyo wangu na kunipa mawazo mengi sana,ilibidi niseme ukweli kuliko kulala nje bora wanipe ruhusa nilale mle kwenye kile kibanda!
“Jamani mimi ni mgeni hapa!”
“MGENIIII?”
Walishtuka hadi yule mzee wa ukoko naye akageuka na kuniangalia kwa makini,bado sikujua kwanini watu wa kijiji hiki wanashtuka sana wakisikia neno “MGENI”.
“Ndiyo mi ni mgeni nimekuja hapa kufanya utafiti kuhusu tamaduni na maisha ya hapa,ni muandishi wa vitabu,naitwa Jack Mambo!
“Wewe kaka hiki kijiji hakipokei wageni kama nyie,tupishe tufunge sisi!”
Wale wadada walisema wakionekana kuwa hawana masikhara,nilijitetea lakini hakuna aliyenisikiliza kabisa,sikuwa na jinsi mpaka muda huo yule mzee wa ukoko alikuwa kimya hajasema kitu!
Nilijizoazoa taratibu na kibegi changu nikakiweka mgongoni,taratibu nkazipiga hatua zangu nikatoka nje!
Sikuwa najua pa kuelekea,sijui mtaa wowote sina mwenyeji wala mtu ninayemfahamu,nilishawahi kufanya tafiti mbali mbali ila kwa hii stori duh!
Nilianza kutembea nikiwa sijui naelekea wapi,wakati huo giza limeshaingia na mvua imeanza kunyesha taratibu!
Nilitamani kulia ila nilijikaza nikiamini ni changamoto ,japo kilichonipa hofu ni zile stori nilizosikia kuhusu Sumbawanga!
Nikiwa kwenye kuwaza ghafla nilishikwa mkono begani nikastuka sana,niligeuka nikakutana na yule mzee wa ukoko!
“Kijana unaenda wapi?”
“Sijui mzee wangu!”
“Nifuate!”
Alisema yule mzee kisha akaanza kuondoka,nilibaki nimesimama nikiwa na hofu kubwa lakini niliona hakuna jinsi!
Taratibu nilianza kuzivuta hatua zangu kumfuata yule mzee wa ukoko,haikuwa safari ndogo wala ndefu sana!
Mwisho tulifika sehemu ambayo kulikuwa na nyumba nyingi huku chache zikiwa zimeezekwa kwa bati!nyingi ziliezekwa kwa nyasi huku zingine zikiwa zimejengwa kwa nyasi kuanzia chini mpaka juu!
Safari ilitupeleka mpaka kwenye vijumba viwili vya udongo vilivyoezekwa kwa nyasi na vyote vilikuwa sehemu moja!
“Karibu kijana!”
“Ahsante sana mzee!”
“Ngoja nimgongee binti yangu atupe chakula!’
Nilishtuka kusikia yule mzee anataka chakula na huku ametoka kupakia jungu la ukoko tena mwingi tu!
Sikutaka kumuonyesha kuwa nimeshangaa nilitaka kiletwe hicho chakula nione yule mzee atakulaje na makoko aliyoyajaza tumboni!
Yule mzee alienda kwernye moja ya vile vijumba akagonga mlango,alitoka binti mmoja ambaye mwanga wa mbalamwezi ulisaidia kunionyesha urembo wa binti yule!
Alikuwa ni mrembo haswa!nakiri ni mmoja wa wanawake warembo niliyowahi kuwaona maishani!
Alifika akamsalimia ule mzee kwa kilugha chao kisha akanisalimia mimi pia kwa kilugha chao nikabakli nimeduwaa!
“Shikamoo!”
“Marahaba!”
Alipoona tu simuitikii akanisalimia kiswahili,kisha yule mzee akampa maelekezo akarudi kwenye kile kijumba chake!
Yule mzee alinichukua mpaka kwenye kile kijumba kingine,akawasha chemli,punde yule binti alikuja na chakula ambacho kilikuwa ni ugali na nyama!Nilikula kidogo tu nikawa nimeshiba,ila yule mzee alikula kama hajala ukoko nikabaki namshangaa tu,nikajiuliza au wako wawili!
Baada ya kumaliza kula ndipo akatoa kauli ambayo iliniacha kwenye wakati mgumu sana!
“Kijana mimi leo nalala na mama yako hapa,wewe kalale na binti yangu ila usimguse,kati ya vitu sitaki ukosee ni kufanya mapenzi na binti yangu!”
Kauli ile ilinishtua sana,kama ni mtihani ni ule,nilijiuliza nawezaje kulala na binti yule alivyo mrembo na nisimguse?
Iko vizuri sana ngoja tuone inavyoendelea