jogoolashamba
JF-Expert Member
- Nov 18, 2012
- 348
- 71
Paka ukimpa samaki, hata mkavu, humla kuanzia kichwani. Jaribu uone anytime.
Jaji Waryoba anaongoza Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Ukubwa wa tatizo la Mungano wa Tanganyika na Zanzibar na ukubwa wa kuunda Katiba Mpya hayapishani sana. Tuwe wakweli, Tume yako Jaji Waryoba ni Tume ya Katiba siyo ya Kero za Mungano.
Nimetumia "Kero za Muungano" kwa sababu inadhaniwa kuwa Mungano hauridhishi kwa sababu ya kero hizo. Na Katiba kuwa makini ni lazima itokane na Nchi isiyo na kero kama hizo. Hii ni logic tu kuwa kero za Mungano zijadiliwe kwanza halafu ndiyo iundwe Katiba inayoendana na mwafaka wa Mungano.
Kipengere cha Kwanza cha Katiba yeyote kinatamka wazi Katiba imeandikwa kwa ajili ya nani, kukidhi mahitaji yepi!
Jaji Waryoba Unapojadili Katiba bila kujua Muungano ni sawa na paka sasa kuanza kula samaki kuanzia mkiani. Paka wa namna hiyo hakuna, vipi wanadamu tunakosa uadilifu wa kujua lipi litangulie lipi!
Kama siyo noma basi mtakeni Mheshimiwa Mkuu wa Nchi awaruhusu mkamilishe kwanza maoni kuhusu Mungano na uundwe Mungano huo ili tutakapokuwa tukichangia mawazo kuhusu Katiba tuwe wazi akilini tunachangia mawazo ya kukidhi aina gani ya Utawala. Sasa hivi hakuna anayejua Zenj wataibuka na nini (Bara wamezoea kusukumwa hata na uongo).
Chonde chonde Jaji Waryoba, Katiba na Mungano haviwezi kukusanyiwa mawazo kwa pamoja, Mungano ni lazima ukamilike kwanza ndiyo tuandike Katiba yake.
Jaji Waryoba anaongoza Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Ukubwa wa tatizo la Mungano wa Tanganyika na Zanzibar na ukubwa wa kuunda Katiba Mpya hayapishani sana. Tuwe wakweli, Tume yako Jaji Waryoba ni Tume ya Katiba siyo ya Kero za Mungano.
Nimetumia "Kero za Muungano" kwa sababu inadhaniwa kuwa Mungano hauridhishi kwa sababu ya kero hizo. Na Katiba kuwa makini ni lazima itokane na Nchi isiyo na kero kama hizo. Hii ni logic tu kuwa kero za Mungano zijadiliwe kwanza halafu ndiyo iundwe Katiba inayoendana na mwafaka wa Mungano.
Kipengere cha Kwanza cha Katiba yeyote kinatamka wazi Katiba imeandikwa kwa ajili ya nani, kukidhi mahitaji yepi!
Jaji Waryoba Unapojadili Katiba bila kujua Muungano ni sawa na paka sasa kuanza kula samaki kuanzia mkiani. Paka wa namna hiyo hakuna, vipi wanadamu tunakosa uadilifu wa kujua lipi litangulie lipi!
Kama siyo noma basi mtakeni Mheshimiwa Mkuu wa Nchi awaruhusu mkamilishe kwanza maoni kuhusu Mungano na uundwe Mungano huo ili tutakapokuwa tukichangia mawazo kuhusu Katiba tuwe wazi akilini tunachangia mawazo ya kukidhi aina gani ya Utawala. Sasa hivi hakuna anayejua Zenj wataibuka na nini (Bara wamezoea kusukumwa hata na uongo).
Chonde chonde Jaji Waryoba, Katiba na Mungano haviwezi kukusanyiwa mawazo kwa pamoja, Mungano ni lazima ukamilike kwanza ndiyo tuandike Katiba yake.