chonde chonde serikali..elimu ya darasa la saba musiiletee siasa

chonde chonde serikali..elimu ya darasa la saba musiiletee siasa

figganigga

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
25,724
Reaction score
55,906
Heshima mbele.

natumia nafasi hii kuwaasa serikali waachane na siasa kwenye maswala ya elimu.mitihani ya darasa la 7 imekuwa rahisi sana kiasi kwamba hata mtoto wa darasa la 5 akiifanya anaweza kufaulu.

mwisho wa siku utaskia ufaulu wa std vii umeongezeka kutoka % fulani.hii siyo njia ya kutatua matatizo ya Tanzania.muhimu ni kuwajali walimu na kuwawezesha nyenzo za ufundishaji.la sivyo elimu yetu itaendelea kua duni.

nasubmit.
mia
 
Bwanawe!Kama unajua kuliko na siasa za ubabaishaji ni huko elimu ya msingi.Halmashauri za mitaa na vijiji ndio wasimamizi wa shule,walimu wakuu hawana chao kule.Diwani akiamua mratibu elimu hana chakushauri,kwa sasa maafisa elimu wa wilaya ni watumwa wa madiwani kila kitu "sawa mheshimiwa"akileta utaalamu wake anarudi kwenye chaki na wengi wanaogopa chaki kama ukoma.
Kwenye mtihani ya darasa la saba huko ndio basi kila siku ina boreshwa ili wanafunzi waweze kushinda na baada kuona wanashindwa hesabu sasa ni mtihani wa kuchagua.Maboresho mengi ni ya kisiasa zaidi.
 
Back
Top Bottom