"Chonji" akutwa na sare za JWTZ

"Chonji" akutwa na sare za JWTZ

EMT

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2010
Posts
14,477
Reaction score
15,325
attachment.php


Sare mpya za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zilizokamatwa nyumbani kwa Billionea huyo.

Moja ya tukio ambalo limewatikisa polisi baada ya kumkamata Mharami Mohamed Abadallah ‘Chonji’ ni kumkuta na sare mpya za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) baada ya kufanya upekuzi wa kina nyumbani kwake Magomeni Kondoa, jijini Dar.

Sare hizo zinafanana kwa sehemu kubwa na zile zilizomwingiza Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenye mzozo na jeshi hilo.

Mbali na sare kwa maana ya mavazi, pia mtuhumiwa huyo alikutwa na viatu vya jeshi hilo maarufu kwa jina la buti nazo zikiwa mpya!

Katika hali iliyowatia shaka zaidi askari ni pale Mharami alipopekuliwa zaidi na kukutwa na bastola ambayo jeshi la polisi halijaitolea ufafanuzi inaitwaje na ilitengenezwa nchi gani!

Vitu vingine vilivyokutwa kwa mtuhumiwa huyo ni jiko dogo la gesi na gundi ya plastiki, vyote vinaaminiwa kutumika wakati wa kutengeneza kete za unga tayari kwa kusafirisha.
 
Hizo ni materials tu bado information aliyonayo kuhusu mtandao mzima wa biashara yao hiyo haramu..
 
mwisho wa uovu ni aibu kubwa. huenda ni sare za diamond polis waendelee kumbana watagundua huenda wanaushirikiano na daimond kwenye biashara hy.ngoja tusubiri.
 
attachment.php


Sare mpya za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zilizokamatwa nyumbani kwa Billionea huyo.

Moja ya tukio ambalo limewatikisa polisi baada ya kumkamata Mharami Mohamed Abadallah ‘Chonji’ ni kumkuta na sare mpya za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) baada ya kufanya upekuzi wa kina nyumbani kwake Magomeni Kondoa, jijini Dar.

Sare hizo zinafanana kwa sehemu kubwa na zile zilizomwingiza Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwenye mzozo na jeshi hilo.

Mbali na sare kwa maana ya mavazi, pia mtuhumiwa huyo alikutwa na viatu vya jeshi hilo maarufu kwa jina la buti nazo zikiwa mpya!

Katika hali iliyowatia shaka zaidi askari ni pale Mharami alipopekuliwa zaidi na kukutwa na bastola ambayo jeshi la polisi halijaitolea ufafanuzi inaitwaje na ilitengenezwa nchi gani!

Vitu vingine vilivyokutwa kwa mtuhumiwa huyo ni jiko dogo la gesi na gundi ya plastiki, vyote vinaaminiwa kutumika wakati wa kutengeneza kete za unga tayari kwa kusafirisha.

na idd azan pia asiachwe.
 
Wampige bomba tu watu kama hawa hawafai hata kuishi wamtungue tu.
 
huyo wamemkomesha maana aliingikia anga za mtu
hawana
lolote zuga tu hatuna imani na nyinyi mpaka wakamatwe vigogo
 
Wafatilie hao hadi watawajua wakubwa wao
 
huyo wamemkomesha maana aliingikia anga za mtu
hawana
lolote zuga tu hatuna imani na nyinyi mpaka wakamatwe vigogo
Kwako wewe kigogo ni MTU wa na na gani???!!!! Umeambiwa huyu ni boss wa mateja, unadhani ni Nani zaidi yake???!!!!. Sema tu huyu amekamatwa sababu amemdhuru mwenzake physically, ni kisasi na huyu hachomoki. Orodha ya akina papa msofe waliodhani wako juu ya sheria inazidi kuwa ndefu
 
Katika hali iliyowatia shaka zaidi askari ni pale Mharami alipopekuliwa zaidi na kukutwa na bastola ambayo jeshi la polisi halijaitolea ufafanuzi inaitwaje na ilitengenezwa nchi gani!
Sasa kama hatujaambiwa inaitwaje na imetengenezwa wapi ni nini kinachofanya hali hiyo iwatie "shaka zaidi"? In other words, nini cha ajabu??? Na umejuaje imewatia polisi "shaka zaidi" wakati wamekataa kukwambia ni bastola gani na imetengenezwa wapi? In other words, waliposema bastola hii inatutia shaka zaidi, walisema ni kwa nini????? Hahahaha... waandishi wa Tanzania bana
 
Tutapata mengi zaidi toka kwa huyo mtu mradi tu wasimmalize mapema kama yule wa Arusha.
 
Back
Top Bottom