Jana tumeshuhudia fainali ya ulaya kati ya ureno na ufaransa ambapo Christian ronaldo alicheza kwa dakika takribani 24 na kuumia,hivyo akashindwa kuendelea na mchezo kwa bahati ureno wakaibuka na ushindi wa goli moja na mpira kumalizika cha ajabu mpira ulivyoisha ikawa tunaonyeshwa Ronaldo muda wote na kila afanyalo zaidi hata kuonyeshwa mfungaji bao pekee wa ureno ambae angalau angestahili hata kuongelewa na kuonyeshwa zaidi lakini ikawa sasa baada ya mechi ni ronaldo ronaldo tu wakati kacheza chini ya nusu saa na hakufanya kashkashi zozote mpaka anatoka dah jamaa anabebwa aisee itakua kama david beckam sasa looh!