Christiano Ronaldo anabebwa mno na vyombo vya habari

ibanezafrica

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2014
Posts
7,261
Reaction score
6,553
Jana tumeshuhudia fainali ya Ulaya kati ya Ureno na Ufaransa ambapo Cristian Ronaldo alicheza kwa dakika takribani 24 na kuumia,hivyo akashindwa kuendelea na mchezo kwa bahati Ureno wakaibuka na ushindi wa goli moja na mpira kumalizika.

Cha ajabu mpira ulivyoisha ikawa tunaonyeshwa Ronaldo muda wote na kila afanyalo zaidi hata kuonyeshwa mfungaji bao pekee wa Ureno ambae angalau angestahili hata kuongelewa na kuonyeshwa zaidi lakini ikawa sasa baada ya mechi ni Ronaldo...Ronaldo tu wakati kacheza chini ya nusu saa na hakufanya kashkashi zozote mpaka anatoka.

Dah jamaa anabebwa aisee itakuwa kama David Beckam sasa looh!
 
Amelipa deni kubwa sana mlokuwa mnamdai miaka kibao,yaani kuipa kombe timu ya taifa...nafkir ilo swali hamtauliza tena....by the way,haka kamchezo hakaitaji hasira...stay calm and watch....
 
Hata ingekuwa Messi ndo ambacho kingetokea....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…